zitto junior
JF-Expert Member
- Oct 7, 2013
- 19,006
- 28,629
Mbona hoja yako ipo biased sana, TANESCO ikitaka kuendeshwa kibiashara mtamudu gharama? Yaani wauze Unit moja kwa bei ya zaidi ya sokoni ili wacover operating expenses zote!!?Mahitaji ya umeme yataongezeka hadi kufikia megawatts 4,000 mwaka 2025 huku uwezo wa TANESCO ukiwa ni kuzalisha megwatts 1,600 kukiwa na tofauti ya Megawatts 2,400 ambayo ni Upungufu wa 60%.
WAkati huo mradi wa Mwalimu Nyerere uliotarajia kuzalisha Megawatts 2,115 ukiwa ni kizungumkuti kutokana na kukumbana na cha ngamoto ya mabadiliko ya tabia nchi , hali inayoleta mashaka kwa Tanzania kuwa na uwezekano wa kukumbana na uhaba mkali wa nishati ya umeme kwa miaka minne ijayo.
KAtika mpango mkakati wa miaka mitano ijayo TANESCO wamejipanga kutumia Tsh. Trilioni 26.17 ili kuongeza uzalishaji wa nishati ya umeme. Gharama hizi zinawasilisha hasara ya Tsh. Trilioni 13. 34 kwa kuwa jumla ya mapato wanayokadiria kukusanya kwa miaka mitano ni Tsh. Trilioni 12.83.
View attachment 2020486
Hasara inaweza kuwa kubwa zaidi kwa kuwa haijaweka gharama za uendeshaji za kila siku kama malipo ya mishahara, nishati ya maji nk, kwa kuwa hela iliyotajwa hapo ni ya kuongeza uzalishaji wa umeme tu!
TANESCO wamejipanga kupata mapato ya Trilioni 1.9 kwa mwaka wa fedha 2020/21 ambapo katika mpango mkakati wa TANESCO wanatarajia kuongeza mapato kila mwaka wa fedha. Mwaka 2021/22 wamepanga kupata mapato ya Tsh. Trilioni 2.
Katika mpango Mkakati wa 2021/22 hadi 2025/26 TANESCO itakuwa imefanikiwa kuongeza mapato kwa 25% ambapo mwaka 2025/26 watakusanya Tsh. Trilioni 2.39.
Kingine faida ya TANESCO ni mtambuka haipimwi kwa taasisi bali kwa uchumi mzima. Mfano kwa wao kuuza umeme chini ya market value wameokoa biashara ngapi mtaani ama wamepunguza operating expenses ya viwanda vingapo Tanzania?
Taasisi za serikali ziko pale kutoa huduma ila wakisema waende kibiashara nyie nyie mtarudi hapa kulia bei kupanda.
Then upo Biased kusema mahitaji ya umeme yataongezeka ila husemi hata vyanzo vya umeme mfano kupita Gesi, upepo, Joto-Ardhi ipo kwenye mpango wa taifa wa miaka 5!?
JF tunaweza kuwa critique wazuri kama tutapunguza biasness.