TANESCO wahukumiwa kuilipa IPTL Tshs Billion 700 ikiwemo Tshs Billion 306 zilizochotwa katika Account ya Escrow

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Hukumu imetolewa wiki Jana iliyoishia August 24, 2018.

Ahadi hewa za mahakama ya mafisadi mnazikumbuka?

Lini ngedere amhukumu nyani? Yaani ccm iwashitaki mafisadi wenzao waliowaweka madarakani? Na wahukumiwe? Na wafungwe?

Mafisadi wa Escrow waliteuliwa uwaziri, ni viongozi bungeni, wengine wamegombea ubunge kwa tiketi ya ccm wakashinda kwa nguvu ya dola.

Ufisadi ccm ni sawa na mwili na damu..

========================

Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) limeshindwa kwenye kesi yake IPTL -Independent Power Tanzania Limited.

Hukumu hiyo imetolewa na mahakama ya inayoshughulika na migogoro ya uwezekaji, ICSID yenye makao yake mjini Washington DC, Marekani na ipo chini ya benki ya dunia.Tanesco ilikuwa ikiwakilishwa na makampuni mawili ya wawanasheria R.K. Rweyongeza & Co. Advocates na Crax Law Partners ya Tanzania, pamoja na lile la Zurich, Kellerhals Carrard. Pesa hizo zinatakiwa kulipwa kwa Standard Chartered Bank-Hong Kong (SCB-HK).SCB-HK ililinunua deni la IPTL kwa punguzo la bei ya milioni 76.1 kutoka Danaharta Bankin ya Malaysia, August 2005 baada ya Danaharta kushindwa kuchukua mkopo wake kutoka kwa IPTL.

Hiyo ina maana kuwa SCB-HK imepata faida ya dola milioni 172. IPTL ilikopa dola milioni 100 mwaka 1998 kutoka kwenye kundi la benki za Malaysia ili kujenga mtambo umeme Tegeta wenye megawatt 100.

TANESCO ilifungua kesi ICSID baada ya kubaini kuwa imekuwa ikitozwa zaidi na IPTL. Kesi hiyo inahusiana na ripoti ya uchunguzi wa kashfa ya IPTL iliyohusisha uchotwaji wa shilingi bilioni 306 za kitanzania.

Hukumu hiyo imefikiwa mwisho wa wiki iliyopita ambapo World Bank tribunal (international centre for settlement of investment disputes.

ICSID imeamuru TANESCO kuilipa Standard Chartered Bank Hong Kong (SCB HK) kiasi cha dola za kimarekani milioni 148.40 pamoja na tozo riba.

SCB HK ndio walionunua mkopo wa IPTL kutoka bank ya Malaysia Danaharta kwa gharama ya dola za kimarekani milioni 76.1

Kutokana na gharama za riba na nyinginezo sasa TANESCO inatakiwa kulipa Bilioni 700 ZAKITANZANIA.

BILA SHAKA TANESCO WANAYAANGAZA MAISHA YETU
 

Attachments

  • Annulment Proceeding between Standard Chartered Bank and TANESCO.pdf
    1.8 MB · Views: 94
Leo anapigiwa makofi kama JEMBE na watu wa upinzani.
Mkuu wote wanaomshabikia JK walikuwa na maslahi yao binafsi na siyo kwa taifa tena....

Mh. JPM alikabidhiwa nchi ikiwa imeoza kwelikweli kidogo ndio anajitahitahidi kuirudisha katika mstari wanabaki kumuita dikteta....

Natamani tena 2025 asimame tena kuwania kiti cha URAIS maana bila hivyo hii nchi itarudi kulekule....





Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chini ya uongozi wa CCM a.k.a wapiga dili hatuta songa mbele,maana shamba ni lile na walaji ni walewale wanapokezana na kuachiana nafasi tu, tuliambiwa kuna mahakama ya mafisadi ila hatujawahi kuona fisadi hata mmoja akihukumiwa
 
Wachukue ile 1.5T, chenji itabaki. Au safari za boeing kuvuka boda ndio basi tena. Hata zile ndege za kuambiwa zitakuja sasa zaweza zuiliwa na wanaoidai serikali. Ccm hoyeeeeeeee, Kikwete tumekumiss babaa.
Kweli watanzania majuha. Sasa kumshangilia huko kikwete vipi, yani unasahau haya madeni yote kasababisha kikwete leo et unamshangilia na kummiss kweli watanzania wapuuzi kiwango cha kimataifa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chini ya uongozi wa CCM a.k.a wapiga dili hatuta songa mbele,maana shamba ni lile na walaji ni walewale wanapokezana na kuachiana nafasi tu, tuliambiwa kuna mahakama ya mafisadi ila hatujawahi kuona fisadi hata mmoja akihukumiwa
Utawala wa CCM chini ya JK ndio ulikua wa wapigaji.....

Ila CCM ya JPM hutosikia serikali inaingia hasara za kipumbavu kama enzi za JK...

Ilitakiwa tupate Rais kariba ya JPM baada ya Hayati Mwalimu JK Nyerere....

Awamu ya pili, tatu na nne ndio imetufikisha huku ila kwa sasa yatupasa kumshukuru Mungu maana ametuletea Rais ambaye ni mzalendo zaidi na mwenye uchungu wa nchi hii tofouti na hao waliomtamgulia ukimtoa Nyerere

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali kama ipo serious na makini wawabane wale wote waliochukua hela za 'mboga' na 'vijisenti' vya mamilioni ya Tshs.za ESCROW TEGETA account , Lugumi n.k ili kufidia pesa hizo wanazodaiwa TANESCO.
Tujikumbushe :
27 Nov 2014
Tundu Lissu ameibuka na kuijia juu ripoti iliyotolewa na Waziri Muhongo kuhusu mgawo wa fedha za Escrow Tegeta kwa wabunge, majaji, maaskofu na watumishi waandamizi wa serikali /umma akidai ni ya uongo na akaenda mbali kwa kuwataja wahusika

Source : Saad Ebrahim
 
Back
Top Bottom