Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,480
- 9,241
Meneja Uhusiano wa TANESCO Johari Kachwamba, amesema kuwa uwepo wa Kunguru ndiyo chanzo kikubwa cha umeme kukatika mara kwa mara katika wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, kwani Kunguru hao wanachangia kuharibu miundombinu hususani nyaya za umeme.
Kauli hiyo ameitoa hii leo Januari 5, 2021, kwenye kipindi cha SupaBreakfast cha East Africa Radio, hii ni baada ya East Africa Radio kupokea malalamiko ya wananchi wengi kuhusu tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara katika maeneo yao hapa nchini.
"Kinondoni tuna tatizo la Kunguru kuathiri sana miundombinu yetu, tunatumia nyaya zenye magamba ya 'silver' ambazo zinaathirika sana na katika kutatua hili tumeanza kubadilisha nyaya, tunazoziweka sasa hivi hazitakuwa zinaathirika kiurahisi na Kunguru, ni tatizo linalotokea mara kwa mara na si sehemu ya tatizo kubwa ambalo tunaweza kusema watu wa Kinondoni wanashindwa kufanya kazi zao", amesema Johari
Aidha Johari ameongeza pia, "Uwepo wa Kunguru wengi wanaonyanyua nyaya kwenye madampo ya taka na kwenye viwanda vya nyaya vilivyoko maeneo mengi ya Kinondoni ikiwepo machinjio, inafanya Kunguru kutua kwenye nyaya za umeme wa msongo mkubwa (33KV na 11KV) na kusababisha milipuko kati ya waya na waya, pia wakitutua kwenye 'Transformer' husababisha milipuko na hizo nyaya wanazobeba kwa ajili ya kutengeneza viota vyao".
Akizungumzia kuhusu suala la gharama ya kuwekewa nguzo, Johari amesema kuwa, mwananchi hatakiwi kulipa gharama ya nguzo yoyote ya umeme, huku akiwasisitiza Watanzania kuacha kufanya shughuli za kibinadamu karibu na miundombinu ya umeme ili kutoiathiri.
Kauli hiyo ameitoa hii leo Januari 5, 2021, kwenye kipindi cha SupaBreakfast cha East Africa Radio, hii ni baada ya East Africa Radio kupokea malalamiko ya wananchi wengi kuhusu tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara katika maeneo yao hapa nchini.
"Kinondoni tuna tatizo la Kunguru kuathiri sana miundombinu yetu, tunatumia nyaya zenye magamba ya 'silver' ambazo zinaathirika sana na katika kutatua hili tumeanza kubadilisha nyaya, tunazoziweka sasa hivi hazitakuwa zinaathirika kiurahisi na Kunguru, ni tatizo linalotokea mara kwa mara na si sehemu ya tatizo kubwa ambalo tunaweza kusema watu wa Kinondoni wanashindwa kufanya kazi zao", amesema Johari
Aidha Johari ameongeza pia, "Uwepo wa Kunguru wengi wanaonyanyua nyaya kwenye madampo ya taka na kwenye viwanda vya nyaya vilivyoko maeneo mengi ya Kinondoni ikiwepo machinjio, inafanya Kunguru kutua kwenye nyaya za umeme wa msongo mkubwa (33KV na 11KV) na kusababisha milipuko kati ya waya na waya, pia wakitutua kwenye 'Transformer' husababisha milipuko na hizo nyaya wanazobeba kwa ajili ya kutengeneza viota vyao".
Akizungumzia kuhusu suala la gharama ya kuwekewa nguzo, Johari amesema kuwa, mwananchi hatakiwi kulipa gharama ya nguzo yoyote ya umeme, huku akiwasisitiza Watanzania kuacha kufanya shughuli za kibinadamu karibu na miundombinu ya umeme ili kutoiathiri.