TANESCO na TTCL: Pamoja na kupata ruzuku kubwa ya Serikali lakini ufanisi ni mdogo sana

blessings

JF-Expert Member
Jul 9, 2012
6,983
6,235
Haya makampuni, TANESCO & TTCL pamoja na kupata ruzuku kubwa ya serikali lakini ufanisi ni wa kusua sua, wanaishia kununua magari ya kifahari na kuyapiga rangi za ajabu ajabu (TTCL - Njano-Crazy Colour). La kusikitisha zaidi ni kuwa wana wakuu vijana lakini wana mawazo ya kizee mno (kama aliyekuwa Meya Ilala).

Iweje Kampuni kama HALOTEL waje juzi na wameweza kupenya kwenye telecom market ya Tanzania, halafu TTCL na ruzuku, miundo mbinu na wateja wa kuletewa na si kutafuta (ofisi za serikali zote wanatumia landline za TTCL) bado tu hawafanyi vizuri?

Tatizo ni nini?
 
Haya makampuni, TANESCO & TTCL pamoja na kupata ruzuku kubwa ya serikali lakini ufanisi ni wa kusua sua, wanaishia kununua magari ya kifahari na kuyapiga rangi za ajabu ajabu (TTCL - Njano-Crazy Colour). La kusikitisha zaidi ni kuwa wana wakuu vijana lakini wana mawazo ya kizee mno (kama aliyekuwa Meya Ilala).

Iweje Kampuni kama HALOTEL waje juzi na wameweza kupenya kwenye telecom market ya Tanzania, halafu TTCL na ruzuku, miundo mbinu na wateja wa kuletewa na si kutafuta (ofisi za serikali zote wanatumia landline za TTCL) bado tu hawafanyi vizuri?

Tatizo ni nini?
kazi kuongeza marupurupu ya mameneja na wakurugenzi wa bodi huku wamezigeuza kampuni mali zao bila kuwekeza kitu kwa kupiga dili. tingatinga sio kusafisha tu hawa watu inatakiwa kuwafilisi na kuwatupa lupango.
 
Haya makampuni, TANESCO & TTCL pamoja na kupata ruzuku kubwa ya serikali lakini ufanisi ni wa kusua sua, wanaishia kununua magari ya kifahari na kuyapiga rangi za ajabu ajabu (TTCL - Njano-Crazy Colour). La kusikitisha zaidi ni kuwa wana wakuu vijana lakini wana mawazo ya kizee mno (kama aliyekuwa Meya Ilala).

Iweje Kampuni kama HALOTEL waje juzi na wameweza kupenya kwenye telecom market ya Tanzania, halafu TTCL na ruzuku, miundo mbinu na wateja wa kuletewa na si kutafuta (ofisi za serikali zote wanatumia landline za TTCL) bado tu hawafanyi vizuri?

Tatizo ni nini?


Kwa mujibu wa mitandao mbalimbali ambayo imeandika habari za TTCL, nafikiri mwandishi wa taarifa ya hapo juu utakuwa huna taarifa tu kuhusu kinachoendelea kampuni hii ya umma. Labda uvivu katika kufanya tafiti ya kutosha kuhusu kampuni hii, binafsi mimi ni mteja wa kampuni hii, natumia moja ya huduma zao za data, simu ya mezani. Hawa jamaa nimewafatilia sana nikagundua kuna kitu kinafanyika ndani ya kampuni, bado tu awajaanza kupiga kelele sana. bofya link hizo labda utapata mwanga ni kitu gani kinaendelea.

Nilimsikia mkurugenzi wao mkuu akisema kwa sasa wanatekeleza mkakati wa kuleta mabadiliko ya kibiashara, wameishaunga taasisi mbalimbali za serikali na binafsi kwenye mkongo wa taifa, mawasilino ya simu kwenye kata zaidi ya 450…… , juzi tu nimenunua Mi-Fi ya 4G na tumia 4G ya TTCL, wanategemea kuingia kwenye 3G/2G, nasikia wanaingia kwenye mobile Money. cha muhimu kujiuliza ni lini mambo haya yatakamilika


http://www.theeastafrican.co.ke/business/TTCL-to-enter-mobile-market-by-end-of-year/-/2560/2645400/-/fsry7pz/-/com.coremedia.mauritius.cae.contentbeans.MauArticleImpl$$[id=2645400]&title=TTCL%20to%20enter%20mobile%20market%20by%20end%20of%20year

http://dewjiblog.com/2015/12/23/ttcl-yazindua-teknolojia-ya-4g-lte/

TTCL Yakabidhi Mradi wa Huduma za Mawasiliano TBL | Magazeti ya leo| Tanzania News |Tanzania Today

TTCL Yakabidhi Mradi wa Kuunganisha Matawi ya MSD Tanzania

MPALULEBLOG:: MATAWI YA SHIRIKA LA BIMA (NIC) NCHINI KOTE YAUNGANISHWA NA MKONGO WA MAWASILIANO WA TAIFA

TTCL to raise $330 million in a five-year turnaround plan

TTCL PLANS TO LIST ON THE DAR ES SALAAM STOCK EXCHANGE - Corporate Digest
 
Kwa mujibu wa mitandao mbalimbali ambayo imeandika habari za TTCL, nafikiri mwandishi wa taarifa ya hapo juu utakuwa huna taarifa tu kuhusu kinachoendelea kampuni hii ya umma. Labda uvivu katika kufanya tafiti ya kutosha kuhusu kampuni hii, binafsi mimi ni mteja wa kampuni hii, natumia moja ya huduma zao za data, simu ya mezani. Hawa jamaa nimewafatilia sana nikagundua kuna kitu kinafanyika ndani ya kampuni, bado tu awajaanza kupiga kelele sana. bofya link hizo labda utapata mwanga ni kitu gani kinaendelea.

Nilimsikia mkurugenzi wao mkuu akisema kwa sasa wanatekeleza mkakati wa kuleta mabadiliko ya kibiashara, wameishaunga taasisi mbalimbali za serikali na binafsi kwenye mkongo wa taifa, mawasilino ya simu kwenye kata zaidi ya 450…… , juzi tu nimenunua Mi-Fi ya 4G na tumia 4G ya TTCL, wanategemea kuingia kwenye 3G/2G, nasikia wanaingia kwenye mobile Money. cha muhimu kujiuliza ni lini mambo haya yatakamilika


http://www.theeastafrican.co.ke/business/TTCL-to-enter-mobile-market-by-end-of-year/-/2560/2645400/-/fsry7pz/-/com.coremedia.mauritius.cae.contentbeans.MauArticleImpl$$[id=2645400]&title=TTCL%20to%20enter%20mobile%20market%20by%20end%20of%20year

http://dewjiblog.com/2015/12/23/ttcl-yazindua-teknolojia-ya-4g-lte/

TTCL Yakabidhi Mradi wa Huduma za Mawasiliano TBL | Magazeti ya leo| Tanzania News |Tanzania Today

TTCL Yakabidhi Mradi wa Kuunganisha Matawi ya MSD Tanzania

MPALULEBLOG:: MATAWI YA SHIRIKA LA BIMA (NIC) NCHINI KOTE YAUNGANISHWA NA MKONGO WA MAWASILIANO WA TAIFA

TTCL to raise $330 million in a five-year turnaround plan

TTCL PLANS TO LIST ON THE DAR ES SALAAM STOCK EXCHANGE - Corporate Digest

Umemjibu vizuri sana!!.Afahamu pia mpaka dakika hii TTCL ni mali ya AIRTEL ndio walioizuia isifanye miradi yoyote ya maendeleo.Kwa taarifa nimemsikia waziri wa mawasiliano akitamka kuwa mwisho wa mwezi huu airtel watakuwa wameondoka TTCL na TTCL inakuja kwa kasi mimi natumia 4Glte ina speed kali sana.
 
Ipo tofauti kati MALENGO/MATARAJIO vs UHALISIA hayo mnayosema ni mipango (Serikali kumiliki TTCL 100%) si mpaka mwisho wa mwezi huu? Kikampuni kama SMILE COMMUNICATIONS wamekuja juzi na wamepenya na 4G mika sasa wanawauzia data makampuni makubwa ya madini, Oil Exploration companies, Dangote n.k. TTCL ikiwa imezubaa tu. Pengine kelele hizi zitawastua toka usingizini
 
Ipo tofauti kati MALENGO/MATARAJIO vs UHALISIA hayo mnayosema ni mipango (Serikali kumiliki TTCL 100%) si mpaka mwisho wa mwezi huu? Kikampuni kama SMILE COMMUNICATIONS wamekuja juzi na wamepenya na 4G mika sasa wanawauzia data makampuni makubwa ya madini, Oil Exploration companies, Dangote n.k. TTCL ikiwa imezubaa tu. Pengine kelele hizi zitawastua toka usingizini

Hii nimenukuu tu kutoka kwa kiongozi wao ...........Afisa Mkuu Masoko na Mauzo alisema kwa sasa TTCL inatoa huduma hizo kwa makampuni ya simu, taasisi mbalimbali za umma na binafsi, mabenki, hospitali kadhaa, vyombo vya habari, wateja binafsi pamoja na mataifa kama Rwanda, Burundi, Uganda, Kenya, Zambia na nchi ya Malawi. Unaweza click link hii

TTCL Yakabidhi Mradi wa Kuunganisha Matawi ya MSD Tanzania
 
Tatizo ni wafanyakazi ajira zao sio za kulenga ufanisi ila ni ukipata nafasi umetoka..,kwa soko la sahv technolojia inabadilika haraka haraka sana hivyo kama hufanyi kazi kwa ufanisi unajikuta nyuma siku zote
 
Haya makampuni, TANESCO & TTCL pamoja na kupata ruzuku kubwa ya serikali lakini ufanisi ni wa kusua sua, wanaishia kununua magari ya kifahari na kuyapiga rangi za ajabu ajabu (TTCL - Njano-Crazy Colour). La kusikitisha zaidi ni kuwa wana wakuu vijana lakini wana mawazo ya kizee mno (kama aliyekuwa Meya Ilala).

Iweje Kampuni kama HALOTEL waje juzi na wameweza kupenya kwenye telecom market ya Tanzania, halafu TTCL na ruzuku, miundo mbinu na wateja wa kuletewa na si kutafuta (ofisi za serikali zote wanatumia landline za TTCL) bado tu hawafanyi vizuri?

Tatizo ni nini?
TTCL haipokei ruzuku kutoka serikalini ndugu
 
Haya makampuni, TANESCO & TTCL pamoja na kupata ruzuku kubwa ya serikali lakini ufanisi ni wa kusua sua, wanaishia kununua magari ya kifahari na kuyapiga rangi za ajabu ajabu (TTCL - Njano-Crazy Colour). La kusikitisha zaidi ni kuwa wana wakuu vijana lakini wana mawazo ya kizee mno (kama aliyekuwa Meya Ilala).

Iweje Kampuni kama HALOTEL waje juzi na wameweza kupenya kwenye telecom market ya Tanzania, halafu TTCL na ruzuku, miundo mbinu na wateja wa kuletewa na si kutafuta (ofisi za serikali zote wanatumia landline za TTCL) bado tu hawafanyi vizuri?

Tatizo ni nini?
Ubunifu hakuna. Wabunifu tupo wachache sana hii inchi. Our education should foster creativity bila hivyo hatufiki mbali. Its time to think beyond formal education
 
Tatizo ni wafanyakazi ajira zao sio za kulenga ufanisi ila ni ukipata nafasi umetoka..,kwa soko la sahv technolojia inabadilika haraka haraka sana hivyo kama hufanyi kazi kwa ufanisi unajikuta nyuma siku zote
Hii comment nimeipenda. Kwenye mashirika kama haya wanatakiwa watu eenye ufanisi wa hali ya juu. Kuna watu naturally wanaweza kufanya mambo yaende. Tukiangalia sana vyeti hatutofika malengo .
 
Haya makampuni, TANESCO & TTCL pamoja na kupata ruzuku kubwa ya serikali lakini ufanisi ni wa kusua sua, wanaishia kununua magari ya kifahari na kuyapiga rangi za ajabu ajabu (TTCL - Njano-Crazy Colour). La kusikitisha zaidi ni kuwa wana wakuu vijana lakini wana mawazo ya kizee mno (kama aliyekuwa Meya Ilala).

Iweje Kampuni kama HALOTEL waje juzi na wameweza kupenya kwenye telecom market ya Tanzania, halafu TTCL na ruzuku, miundo mbinu na wateja wa kuletewa na si kutafuta (ofisi za serikali zote wanatumia landline za TTCL) bado tu hawafanyi vizuri?

Tatizo ni nini?
ukiritimba mwimgi sana sana......
 
But recently naona TTCL kuna move inatokea pale. Kwanza wamebadili logo, na pia wako very active kwenye social media facebook kujibu malalamiko ya wanzania. Thats good
 
Haya makampuni, TANESCO & TTCL pamoja na kupata ruzuku kubwa ya serikali lakini ufanisi ni wa kusua sua, wanaishia kununua magari ya kifahari na kuyapiga rangi za ajabu ajabu (TTCL - Njano-Crazy Colour). La kusikitisha zaidi ni kuwa wana wakuu vijana lakini wana mawazo ya kizee mno (kama aliyekuwa Meya Ilala).

Iweje Kampuni kama HALOTEL waje juzi na wameweza kupenya kwenye telecom market ya Tanzania, halafu TTCL na ruzuku, miundo mbinu na wateja wa kuletewa na si kutafuta (ofisi za serikali zote wanatumia landline za TTCL) bado tu hawafanyi vizuri?

Tatizo ni nini?
tatizo kubwa ni serikali waliingia UBIA na kampuni mbovu sasa wamechukua TTCL hope watakuja na mbinu mpya..ukiuliza kwa nn kampuni kama TTCL iliuzwa wakati ufanisi wake ulikuwa bora sana NO ONE KNOWS...Tanesco ina matatizo mengi sana mikataba mibovu sana sana ndio inachoangusha kampuni...management mbovu,wanasiasa wanaingilia sana haya makampuni
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mfano mzuri ni hawa TANESCO, inakuwaje Mtu Mara baada ya kulipia gharama za kufungiwa umeme, unalazimishwa kusubiria ndani ya Siku30. Na Wakati mwingine hizo siku30 kwa wengine huwa zinapitiliza hadi uwakumbushe.

Kuna nn cha muhimu hasa kwa Mteja ambaye keshalipia huduma ili aje afungiwe umeme, kisha anaambiwa atapigiwa simu baada ya siku30!?

Naomba kama kuna Mtu wa Tanesco alitolee ufafanuzi please.
 
Wakitaka mashirika yetu ya uma yafanye vizuri hawana budi kuajiri wakurugenzi na baadhi ya mameneja wazungu . maana waswahili wakiongoza makampuni mwisho wake ni kufirisika sababu ya wizi na uvivu.
 
Haya makampuni, TANESCO & TTCL pamoja na kupata ruzuku kubwa ya serikali lakini ufanisi ni wa kusua sua, wanaishia kununua magari ya kifahari na kuyapiga rangi za ajabu ajabu (TTCL - Njano-Crazy Colour). La kusikitisha zaidi ni kuwa wana wakuu vijana lakini wana mawazo ya kizee mno (kama aliyekuwa Meya Ilala).

Iweje Kampuni kama HALOTEL waje juzi na wameweza kupenya kwenye telecom market ya Tanzania, halafu TTCL na ruzuku, miundo mbinu na wateja wa kuletewa na si kutafuta (ofisi za serikali zote wanatumia landline za TTCL) bado tu hawafanyi vizuri?

Tatizo ni nini?


TANESCO YAFANYA MAKUBWA KUBORESHA SEKTA YA UMEME NCHINI

1.Kuongeza Uzalishaji Umeme

Kwa kuzingatia ukuaji wa sekta ndogo ya umeme hapa nchini na mahitaji makubwa ya umeme yanayoongezeka kwa kasi, Serikali iliweka mikakati mahsusi kuongeza uzalishaji wa umeme hadi kufikia MW 2,780 Mwaka 2015/16. Katika kipindi cha 2005 – 2015, Serikali ya Awamu ya Nne ilifanikiwa kuongeza uwezo wa mitambo ya kuzalisha umeme katika Gridi ya Taifa kutoka MW 891 zilizokuwepo mwaka 2005 hadi kufikia MW 1,501.24 mwaka 2014 sawa na ongezeko la asilimia 68.5. Mpaka kufikia Julai, 2015 uwezo wa mitambo ya kuzalisha umeme katika Grid ya Taifa ulipungua na kufikia MW 1,246.24 kutokana na kukoma kwa baadhi ya mikataba ya wazalishaji binafsi ambao wamekuwa mzigo kwa Shirika kutokana na gharama kubwa. Kuongezeka kwa uwezo wa mitambo ya kuzalisha umeme katika Gridi ya Taifa kwa kipindi cha Awamu ya Nne kutokana na utekelezaji wa mipango na miradi mbalimbali ya kuzalisha umeme. Juhudi zilizochangia mafanikio hayo ni pamoja na:

(i)Kukamilika kwa Mtambo wa kuzalisha umeme MW 100 – Ubungo I: Mtambo huo upo katika eneo la TANESCO-Ubungo Dar es Salaam. Mtambo huu una uwezo wa kufua umeme wa MW 100 kwa kutumia gesi asilia na ulifunguliwa rasmi na Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwezi Novemba, 2008.

(ii)Kukamilika kwa Ujenzi wa Mtambo wa Kufua Umeme, MW 45 – Tegeta: Ujenzi wa mtambo huo unaotumia gesi asilia una uwezo wa kufua umeme wa MW 45 ulikamilika na kuanza kufua umeme Mwezi Desemba, 2009.

(iii)Kukamilika kwa Ujenzi wa Mtambo wa Kufua Umeme, MW 105 – Ubungo II: Mtambo huu unatumia gesi asilia kufua umeme wa MW 105, upo katika eneo la TANESCO – Ubungo Jijini Dar es Salaam na ulizinduliwa rasmi na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Mh. Prof. Sospeter M. Muhongo Mwezi June, 2012.

(iv)Kukamilika kwa Mtambo wa kuzalisha umeme MW 60 – Mwanza: Ujenzi wa mtambo huo umekamilika na ulizinduliwa rasmi na Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 06 Septemba, 2013. Mtambo huu umesaidia kuboresha upatikanaji wa umeme na kuimarisha gridi ya Taifa katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.

(v)Kukamilika kwa Mradi wa Umeme wa Somanga Fungu, MW 7.5: Mitambo ya kufua umeme wa MW 7.5 kwa kutumia gesi asilia iliyopo Somanga Fungu mkoani Lindi ilizinduliwa na Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mwezi Agosti, 2010. Mitambo hiyo inafua umeme unaosambazwa katika miji ya Bungu, Kibiti, Kilwa Kivinje, Kilwa Masoko, Kindwitwi, Muhoro, Nangurukuru, Somanga, Tingi, Utete, Nyamwange, maeneo ya Njia Nne na Hospitali ya Mchukwi.

(vi)Mchango wa Wazalishaji Wadogo wa Umeme katika Gridi ya Taifa: Katika kipindi cha 2005 hadi 2015, wazalishaji wadogo wa umeme waliingia mikataba ya kuuziana umeme na TANESCO ambapo umeme wa MW 8 ununuliwa. Wazalishaji hao ni ni TANWAT – MW 1; TPC – MW 3; na Mwenga Mini Hydro – MW 4.

(vii)Kuboresha Huduma ya Umeme Katika Maeneo yaliyopo Nje ya Gridi ya Taifa: Katika kipindi cha 2005 hadi 2015, utekelezaji wa mipango mbalimbali ya ukarabati na ufungaji wa mitambo mipya ya kufua umeme kwa kutumia mafuta katika maeneo ambayo bado hayajaunganishwa katika gridi ya Taifa imefanyika. Ukarabati wa mitambo ya kufua umeme kwa kutumia mafuta ulifanyika kwenye vituo vya Mpanda, Kigoma, Masasi, Mafia, Songea, Tunduru, Ngara na Biharamulo. Aidha, Serikali kupitia TANESCO ilinunua mitambo mipya 19 ya kufua umeme kwa kutumia dizeli iliyofungwa katika vituo vya Kasulu (1.25 x 2), Kibondo (1.25 x 2), Kigoma (1.25 x 5), Loliondo (1.25 x 4), Namtumbo (0.32 x 1), Songea (1.9 x 1) na Sumbawanga (1.25 x 4). Mitambo hiyo mipya iligharimu EURO milioni 35.94 sawa na Shilingi bilioni 57.5. Pia kuna wazalishaji binafsi waliowekeza katika maeneo yaliyopo nje ya gridi ambao ni Ngombeni – MW 1.4 na Andoya Hydro MW 0.5.

(viii)Kukamilika kwa Mradi wa Mawengi wenye Uwezo wa Kuzalisha kW 300 kwa Kutumia Maporomoko Madogo ya Maji: Mradi huo uliopo Wilayani Ludewa ulizinduliwa na Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwezi Novemba, 2011, ambapo hadi kufikia Mwezi Octoba, 2014 zaidi ya kaya 1,153 zilikuwa zimeunganishiwa umeme.

Kukamilika kwa miradi hiyo kumewezesha upatikanaji wa umeme wa uhakika nchini na kufanikisha kuondoa mgawo wa umeme hususan kuanzia Mwaka 2012 na hivyo kuboresha ufanisi wa utekelezaji wa shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii.
Pamoja na kukamilika kwa miradi hiyo, pia kumekuwepo na mikakati mbalimbali ya kuongeza uzalishazi wa umeme kwenye Gridi ya Taifa na je ya Gridi ya Taifa kama ifuatavyo;
(i)Utekelezaji wa Mradi wa Kinyerezi I – MW 150 kwa Kutumia Gesi Asilia: Serikali imefanya juhudi kupunguza utegemezi wa mitambo ya kufua umeme kwa kutumia mafuta ambayo ni ghali. Hatua zilizochukuliwa ni pamoja na kuamua kwa dhati na kwa kutumia fedha za Watanzania kutekeleza mradi wa Kinyerezi - I (MW 150). Mradi huo unaojumuisha ujenzi wa njia za umeme za msongo wa kV 220 (Kinyerezi - Kimara) na kV 132 (Kinyerezi - Gongolamboto) utatumia gesi asilia na utagharimu Dola za Marekani milioni 183.30, sawa na Shilingi bilioni 293.28. Utekelezaji wa Mradi huo ulianza Mwezi Januari, 2013 na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Mwezi Agosti, 2015.

(ii)Mradi wa kupeleka umeme miji ya Mpanda, Ngara na Biharamulo (ORIO): Mradi huu unajumuisha ufungaji wa jenereta mbili (2) zenye uwezo wa MW 1.25 katika kila mji, ukarabati wa njia za umeme zilizoharibika na ujenzi w njia mpya za umeme. Awamu ya kwanza ya mradi (development) ilianza September, 2010; na wamu ya pili ya mradi ambayo ni Utelelezaji, Uendeshaji na Matengenezo (Implementation and Operation & Maintenance Phase) ilianza Septemba, 2012. Hadi sasa mchakato mzima wa tenda kwa ajili ya kuwapata wakandarasi kwa ajili ya utelezaji wa mradi huu umekamilika na kazi ya utekelezaji ilianza mwezi Oktoba, 2013. Pia kumekuwa na mafunzo kwa ajili ya wajasiriamali wadogo na wa kati pamoja na mafunzo ya uongozi wa miradi.
(iii)Mradi wa Kufua Umeme Rusumo na Njia ya Kusafirisha Umeme: Mradi huu unahusisha ujenzi wa kituo cha kufua umeme wa MW 80 kwa kutumia maji. Mpaka sasa uchambuzi yakinifu umekamirika, Ripoti ya mazingira kwa upande wa usambazaji kutoka BENACO mpaka mpakani Rusumo tayari imekamirika na kibari cha kuendeleza mradi kinasubiriwa kutoka NEMC. Mchakato wa kupata njia ardhi kwa ajili ya njia ya usafirishia umeme toka Rusumo mpaka Nyakanazi ya kV 220 tayari umeanza.

(iv)Mradi wa Kufua Umeme Kakono Hydro MW 87: Mradi huu unahusisha ujenzi wa kituo cha kufua umeme wa MW 87 kwa kutumia maji. Mpaka sasa uchambuzi yakinifu umekamilika, Ripoti ya mazingira ya kituo cha kuzalisha umeme na njia ya kusafirisha umeme toka Kakono hadi Kyaka ipo tayari na imewasilishwa NEMC Mwezi Mei, 2015 kwa ajili ya kupata kibali ya kuendeleza mradi. Gharama ya mradi inakadiriwa kuwa Dola za Kimarekani Milioni 379.4 na unatarajiwa kukamilika 2019.

1Kujenga na Kuimarisha Njia za Usafirishaji na Usambazaji Umeme

Katika kipindi cha kuanzia 2005 – 2015, juhudi kubwa zimefanyika kuimarisha njia za usafirishaji na usambazaji wa umeme ili kuwezesha nishati hiyo kuwafikia watumiaji kwa ubora na kwa wakati wote na kuweza kukidhi ongezeko la mahitaji ya umeme nchini. TANESCO imefanya ukarabati na kujenga miundombinu ya usafirishaji na usambazaji umeme. Ukarabati huu umefanyika na unaendelea kufanyika katika mikoa mbalimbali inayopata umeme kupitia Gridi ya Taifa. Kazi hii inafanyika kwa fedha za ndani na kwa ufadhili kutoka wahisani mbalimbali wakiwemo Benki ya Dunia, Benki ya Maendeleo ya Afrika, Shirika la Marekani linalotoaÂÂÂ misaada kwaÂÂÂ nchi maskini (MCC), Korea Kusini na JICA. Miradi hiyo ni pamoja na ifuatayo;

(i)Kukamilika kwa Mradi wa Kuboresha Kituo cha Taifa cha Kusimamia Mfumo wa Umeme wa Gridi (National Grid Control Cetre): Mradi huu ulianza mwaka 2009 na kukamilika mwaka 2012. Mradi huu ulihusisha ubadilishaji wa mfumo wa zamani SCADA na ufungwaji wa mfumo mpya wa SCADA/EMS. Mradi pia ulihusisha ununuzi, ufungwaji na majaribio ya ‘National Grid Control Center (GCC) – Ubungo, DSM na ufungwaji wa vifaa vingine viambatanavyo na mfumo huo katika nchi nzima. Gharama za Mradi huo ni Euro milioni 3.04 na Dola za Marekani 622,394 sawa na jumla ya Shilingi bilioni 7.4.
(ii)Mradi wa kuboresha mifumo na upatikanaji wa umeme katika Jiji la Dar es Salaam (TEDAP na Finish Project): Mradi wa TEDAP unahusisha ujenzi wa njiaÂÂÂ msongo wa 132kV ya kilomita 7 kutoka Ubungo – Makumbusho na kituo cha kupoozea umeme cha Makumbusho cha 132/33kV chenye uwezo wa 2 X 45MVA. Mradi huu umekamilika na kuondoa tatizo la umeme mdogo “Low Voltage” na kukatika katika katika maeneo ya Wilaya ya Kinondoni. Pia ulihusisha ujenzi wa vituo vipya vya kupoozea umeme maeneo ya katikati ya jiji, Kipawa, Mburahati, Mikocheni na Oysterbay, ukarabati wa vituo vya kupoozea umeme maeneo ya Chang’ombe, Kariakoo, Kurasini, Mbagala, Ubungo na ujenzi wa njia za umeme za kilomita 51.7 za msongo wa kilovolti 132 na kilomita 83 za msongo wa 0.4kV unaotegemewa kukamika ifikapo Mwezi Disemba, 2015.

Mradi wa Finish umehusisha kujenga njia ya usafirishaji umeme chini ya ardhi ya 132kV kutoka Ilala hadi City Centre Kujenga kituo cha kupoozea umeme cha 132/33/11kV chenye uwezo wa 2x45MVA, ujenzi wa njia ya umeme chini ya ardhi kwa ajili ya kuunga kituo cha Kariakoo – Railway – Sokoine na kituo cha zamani cha City Centre, kuanzisha kituo cha kuongozea mifumo ya usambazaji umeme katika msongo wa kV 33 na kV 11 (distribution SCADA). Mradi huu ulishaanza na unategemewa kukamilika ifikapo Mwezi Septemba, 2015.

(iii)Ujenzi wa Njia Mpya ya Kupeleka Umeme Zanzibar ya Msongo wa kV 132 na Kupeleka Umeme Pemba kutoka Tanga ya msongo wa kV 33: Mradi wa kupeleka umeme Zanzibar ulizinduliwa rasmi tarehe 10 Aprili 2013 na umeboresha usafirishaji umeme wa uhakika katika visiwa vya Zanzibar. Mradi ulihusisha ujenzi wa waya wa majini (Submarine cable) wa njia ya kilomita 39 ambao ulimalizika mwanzoni mwa mwezi Machi 2013. Pia waya wa juu (Overhead line) wa njia ya kilomita 37 ambao ulimalizika mwishoni mwa mwezi February 2013.ÂÂÂ Pia kukamilikaÂÂÂ mradi wa kupeleka umeme Pemba ambaoÂÂÂ ulizinduliwa rasmi tarehe 9 Mei, 2013 na umeboresha upatikanaji umeme wa uhakika katika kisiwa cha Pemba. Kazi hiiÂÂÂ ilihusisha kutandaza waya wa majini (submarine cable) yenye urefu wa kilomita 90.

(iv)Kuimarisha mfumo wa njia za usafirishaji na usambazaji katika Mikoa ya Arusha na Kilimanjaro (TEDAP): Mradi huu ulihusisha ufungwaji wa Transformer mpya katika vituo vya kupoozea umeme vya Boma Mbuzi, Mt. Meru, Kiltex, Njiro B, Sakina, Themi, Trade School na Unga Ltd. Pia ujenzi wa njia za usambazaji wa umeme katika miji ya Arusha kilomita 143 na Kilimanjaro kilomita 25, ukarabatiÂÂÂ wa kituo cha kupoozea umeme cha Kiyungi na ujenzi wa njia ya usafirishaji ya umeme ya kilomita 70 ya msongo wa kilovolti 132 kutoka Kiyungi – Njiro, Ujenzi wa kituo kipya cha kupoozea umeme cha KIA cha 132/33kV na ujenzi wa njia ya usafirishaji ya msongo wa 66kV Kiyungi (TPC) Moshi hadi Makuyuni Himo. Mradi huu tayari umekamilika.

(v)Mradi wa Makambako - Songea kV 220: Mradi huo unahusisha ujenzi wa njia yenye urefu wa kilomita 250 na kujenga vituo vya kupoozea umeme 220/132/33kV vya Makambako, Madaba na Songea. Mchakato wa kutafuta wakandarasi wa mradi wa ujenzi wa njia kuu pamoja na vituo vya kupoozea umeme umekamilika na taarifa ya tathmini imewakilishwa kwenye bodi ya zabuni kwa ajili ya kupata kibali hatimaye ipelekwe SIDA; na kujenga kilomita 900 za njia za usambazaji katika miji ya Makambako, Njombe, Ludewa, Songea, Namtumbo, Mbinga, Mbamba Bay, na vijiji vilivyopo karibu na njia ya kusafirishia umeme. Mchakato wa kutafuta wakandarasi wa mradi wa ujenzi wa njia za kusambaza umeme mijini na vijijini umekamilika na umepata kibali kutoka bodi ya dhabuni. Umepelekwa SIDA kwa ajili ya kupata kibali cha kuingia mkataba na mkadarasi aliyeshinda. Wakandarasi wa mradi huu tayari wameanza kazi za awali katika eneo la mradi na kazi inaendelea. Mradi huu unagharamiwa na Serikali ya Sweden kupitia Shirika la Maendeleo la Sweden (Sida) kwa kiasi cha Swedish Kroner milioni 500, sawa na Shilingi bilioni 112. Kwa upande wa usambazaji, mradi umekamilika kwa zaidi ya asilimia 5 na mradi kwa ujumla unatarajia kukamilika mwaka 2017.

(vi)Mradi wa Iringa - Shinyanga kV 400 (Backbone): Mradi huu ni wa kuimarisha Gridi ya Taifa ambapo kukamilika kwake kutapunguza upotevu wa umeme na kuongeza uwezo wa kusafirisha umeme wa kutosheleza mahitaji ya Kanda ya Kaskazini Magharibi. Taratibu za kumpata mtaalamu mshauri wa masuala ya ufundi, sheria na fedha alishapatikana na ameanza kazi; taratibu za manunuzi ya vifaa vya usambazaji umeme (cables na waya) zimekamilika na vifaa vimeanza kuwasili naÂÂÂ mtaalamu wa usimamizi wa mradi ameanza kazi. Vilevile, Serikali kupitia TANESCO imeanza kulipa fidia katika maeneo ya mradi. Aidha, Mshauri wa mradi, Kampuni ya Fitchner ya Ujerumani anaendelea na kazi ya kusanifu njia ya usafirishaji umeme na vituo vya kupozea umeme. Gharama za mradi zinakadiriwa kuwa Dola za Marekani milioni 650, sawa na Shilingi bilioni 1,040. Mradi unatarajiwa kukamilika Mwaka 2016.

(vii)Mradi wa Dar es Salaam – Chalinze – Tanga – Arusha kV 400: Serikali kupitia TANESCO imedurusu usanifu wa mradi (redesigning) ili uanzie Dar es Salaam kupitia Chalinze hadi Arusha badala ya kuanzia Morogoro. Mwezi Juni, 2012 TANESCO na mkandarasi Kampuni ya TBEA ya China walisaini mkataba wa marekebisho (EPC addendum), kwa lengo la kuongeza uwezo wa kusafirisha umeme kutoka Dar es Salaam. Mradi huu utatekelezwa kwa mkopo wa takribani Dola za Marekani milioni 770, sawa na Shilingi bilioni 1,232 kutoka Benki ya Exim ya China na unatarajiwa kukamilika mwaka 2017.

(viii)Mradi wa ujenzi wa njia ya umeme ya kV 220 ya Bulyanhulu – Geita – Nyakanazi: Mwezi Januari, 2011 Serikali ilisaini mkataba wa mkopo na Taasisi ya fedha ya BADEA ya Misri na OFID ya Saudi Arabia. Lengo ni kutekeleza mradi wa ujenzi wa njia ya umeme kV 220 kutoka Bulyanhulu hadi Nyakanazi kupitia Geita. Kazi ya kuandaa zabuni za kandarasi za ujenzi ilikamilika mwezi Juni, 2012. Maeneo kwa ajili ya kujenga vituo vya kupoozea umeme tayari yamepatikana na hatua za kuanza kuwalipa wananchi walioathirika na mradi zipo katika hatua za mwisho. Mradi utagharimu Dola za Marekani milioni 53, sawa na Shilingi bilioni 84.8 na unatarajiwa Mwaka, 2017.

(ix)Mradi North – West Grid kV 400: Serikali imeamua kubadilisha msongo wa njia hiyo ya kusafirisha umeme kutoka kV 220 hadi kV 400 kwa lengo la kuimarishaÂÂÂ mfumo na upatikanaji wa umeme katika Mikoa ya Geita, Kagera, Katavi, Kigoma, Mbeya, Rukwa na Shinyanga ili kukidhi matarajio ya shughuli mbalimbali za kiuchumi katika maeneo hayo. Maombi ya mkopo yamewasilishwa katika Benki ya Exim ya China kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo. Gharama za mradi zinakadiriwa kuwa Dola za Marekani milioni 259.2 na unatarajiwa kukamilika Mwaka, 2018

(x)Mradi wa electricity – V: Mradi huu ulitekelezwa kwa mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na ulihusisha usambazaji wa umeme katika vijiji, miji midogo na Makao Makuu ya Wilaya katika Mikoa ya Geita (Bukombe), Mwanza (Magu na Kwimba) na Simiyu (Bariadi) na kukarabati vituo vikubwa vya kupozea umeme kwenye mikoa ya Dar es Salaam na Arusha.ÂÂÂ Gharama za mradi ni Dola za Marekani milioni 31, sawa na Shilingi bilioni 49.6. Mradi umehusisha ujenzi wa km 480 wa njia za kilovolti 33, km 251 wa njia za volti ndogo (0.4kV) na ufungaji wa transifoma 109 za kilovolti 33/0.4 na uwezo wa kVA 50 hadi 315 juu ya nguzo; ufungaji wa taa za barabarani na kuunganisha wateja wapatao 8,600 katika mikoa ya Mwanza, Simiyu, Shinyanga na Geita;ÂÂÂ ukarabati wa vituo vya kupozea umeme. Kuongeza Transfoma ya mbili yenye uwezo wa 33/11kV, 15MVA; kubadilisha Switchgear zote za nje za 33kV na 11kV na kuweka za ndani pamoja na kuongeza njia za kusambaza umeme kwa wateja; kuimarisha mfumo wote wa umeme ndani ya kituo; kubadilisha Transifoma ya 33/11kV, 15MVA iliyoungua pamoja na kubadilisha kizima umeme (CB); kuongeza Transifoma 2 za 132/33kV, 50MVA; kurefusha switchgear ya 132kV na njia nyingine ya kupeleka umeme wa 132kV katika kituo cha Kiyungi; Kujenga switchgear mpya ya 33kV yenye njia zaidi ya kusambaza umeme na kuweka mfumo mpya wa kidigitali wa kuendesha kituo na kusimamia uzimaji na uwashaji. Mradi huu unategemea kukamilika ifikapo Mwezi Septemba, 2015.


(xi)Mradi wa Kujenga Njia za kusambaza Umeme:
Mradi huu unahusu ujenzi wa njia za msongo wa kV 33, kV 11 na kV 0.4 kwa ajili ya kusambaza umeme katika Mikoa ya Dodoma, Iringa, Manyara, Mbeya, Morogoro, Mwanza, Njombe na Tanga. Jumla ya kilomita 1,068 kati ya kilomita 1,335 zimekamilika za njia ya kV 33, kV 11, na kilomita 1,094.4 kati ya
C:\Users\Henly\AppData\Local\Temp\msohtmlclip1\01\clip_image002.gif
kilomita 1,368 zimekamilika kwa njia za kV 0.4. Sehemu ya miradi iliyokamilika kwa Mkoa wa Dodoma ilihusisha jumla ya vijiji 46 katika Kijiji cha Mkoka, Wilayani Kongwa.

(xii)Mradi wa Kujenga Njia ya Pili ya Umeme kutoka Dar es Salaam kwenda Unguja: Mradi huu ulihusika na ujenzi wa njia ya umeme ya kV 132 kutoka Ubungo hadi Ras-Kilomoni na utandazaji wa nyaya za umeme chini ya bahari kutoka Ras-Kilomoni hadi Mtoni – Unguja.. Gharama za mradi huo ni Dola za Marekani milioni 50, sawa na Shilingi bilioni 80 na tayari umekamilika.

(xiii)Mradi wa Kuunganisha Gridi ya Taifa na Gridi za nchi nyingine: Upembuzi yakinifu wa mradi wa kuunganisha Gridi ya Taifa na gridi za nchi za Zambia na Kenya (ZTK project) ulikamilika kwa upande wa Tanzania kwa ufadhili wa Serikali ya Norway. Aidha, Benki ya Dunia, Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na JICA zimekubali kufadhili utekelezaji wa mradi huo katika kipande cha Singida hadi Namanga. Fedha zinaendelea kutafutwa kwa ajili ya utekelezaji wa sehemu ya mradi kutoka Kabwe hadi Mbeya.ÂÂÂ Kukamilika kwa mradi huu kutawezesha biashara ya umeme kati ya Tanzania na nchi za Afrika Mashariki na Afrika ya Kusini. Gharama za mradi huu ni Dola za Marekani milioni 642. Mradi huu unatarajiwa kukamilika 2018.
 
Wakitaka mashirika yetu ya uma yafanye vizuri hawana budi kuajiri wakurugenzi na baadhi ya mameneja wazungu . maana waswahili wakiongoza makampuni mwisho wake ni kufirisika sababu ya wizi na uvivu.

Acha kukalili kila kinacho fanikiwa lazima kiwe cha mzungu huo ulionao ni utumwa wa mawazo na wa kimtazamo.

Watanzania wanaweza, na wameweza hata hali ya umeme hivi sasa inaimarika licha ya changamoto zinazojitokeza lakini hali ya Umeme nchini yazidi kuimarika.

Hali ya Umeme nchini imeimarika sana kwa sasa kutokana na ujao wa gesi, na bado kuna mitambo inaendelea kuwashwa.
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom