TANESCO mradi wa umeme Buyuni Block 17, 18, 19 na 20, Mkandarasi anajenga jinsi anavyotaka yeye

Lambert Mende

JF-Expert Member
Mar 16, 2015
210
43
Miezi kama mitatu (04) iliyopita TANESCO wameanza kuweka umeme kwenye block tajwa hapo juu, na taarifa zilizopo ni kwamba mzabuni ameshapewa pesa za kumaliza mradi huu, kinachoshangaza mradi huu unajengwa kwa jinsi ambavyo mkandarasi anavyotaka yeye.

Maeneo ya block 19 yamewekewa waya za kuunganisha umeme tayari, maeneo ya block 18 na 20 hayajukikani lini yatapata huo umeme, Mh Muhongo, hizi nguzo mmeziweka na umeme hatupati, halafu mnasema manataka wakazi wa DSM wakae maeneo yaliyopimwa, malizeni miradi hii basi, isiwe ni adhabu kukaa kwenye maeneo yaliyopimwa, ni ajabu kubwa watu wamejenga nyumba kwenye makazi salama kama haya na umeme hamuweki, kwanni? Au mpaka Mh Magufuli aseme ndio mtafanya kazi?
 
Lambert Mende una undugu na yule PR officer wa Mh Kabila?
Anyway poleni sana na mapori ya buyuni, yaani kinachokwamisha huo mradi huko ni huduma za kijamii hasa umeme na barabara,vipi yale madimbwi ya maji (mabwawa) wakati wa masika bado yapo?au mnapeta kipindi cha jua?nilikuja kuangalia site yangu huko mwezi wa tatu nilikata tamaa kabisa.Ila Mh Prof Mhongo na Mh Makonda wanapita sana online humu labda watasikia kilio chenu.

e579c0e471564d9ce4c27b76d2c20034.jpg


Msimu wa mvua mwezi March nilipiga picha Yale mabwawa yenu,hali ilikuwa kama hivi,na mvua za vuli ndio zinakuja muda si mrefu, mtaogelea soon!
 
Hilo tatizo lipo block 6-9 pia tangu waseme Umeme utawekwa may hadi Leo hakuna dalili.....!!!
 
Hilo tatizo lipo block 6-9 pia tangu waseme Umeme utawekwa may hadi Leo hakuna dalili.....!!!
kabanga
Unajua huyu mkandarasi aliepewa hii kazi anaifanya kwa jinsi anavyojisikia mwenyewe, nguzo zimesimishwa mwezi wa tatu huu,usambazaji hakuna,mpaka unashangaa,wameweka za nini?wanapomaliza mradi mapema ndio Tanesco wanapata pesa mapema,nchi hii kila sehemu ni jipu tu,kila sehemu mpaka.watumbuliwe, hembu wajiongeze,mpaka watu wachongeane? Tunawaomba jamani,njoooni mmalizie huu mradi wenu angalau na wengine watakuwa na hamu ya kuja kumalizia nyumba zao huku porini.
 
kabanga
Unajua huyu mkandarasi aliepewa hii kazi anaifanya kwa jinsi anavyojisikia mwenyewe, nguzo zimesimishwa mwezi wa tatu huu,usambazaji hakuna,mpaka unashangaa,wameweka za nini?wanapomaliza mradi mapema ndio Tanesco wanapata pesa mapema,nchi hii kila sehemu ni jipu tu,kila sehemu mpaka.watumbuliwe, hembu wajiongeze,mpaka watu wachongeane? Tunawaomba jamani,njoooni mmalizie huu mradi wenu angalau na wengine watakuwa na hamu ya kuja kumalizia nyumba zao huku porini.
Sisi upande wetu huo, alidai hana sehemu ya kuhifadhi vifaa, mheshima mmoja akajitolea hadi sasa hakuna nguzo wala vifaa....!! Inakera sana
 
Lambert Mende una undugu na yule PR officer wa Mh Kabila?
Anyway poleni sana na mapori ya buyuni, yaani kinachokwamisha huo mradi huko ni huduma za kijamii hasa umeme na barabara,vipi yale madimbwi ya maji (mabwawa) wakati wa masika bado yapo?au mnapeta kipindi cha jua?nilikuja kuangalia site yangu huko mwezi wa tatu nilikata tamaa kabisa.Ila Mh Prof Mhongo na Mh Makonda wanapita sana online humu labda watasikia kilio chenu.

e579c0e471564d9ce4c27b76d2c20034.jpg


Msimu wa mvua mwezi March nilipiga picha Yale mabwawa yenu,hali ilikuwa kama hivi,na mvua za vuli ndio zinakuja muda si mrefu, mtaogelea soon!
Nimeongea na injinia wa PSPF amenihakikishia wana mawasiliano ya karibu na manispaa watalekebisha soon.

By the way kama unafika kigenzi kuna shortcut ya kuingilia tuta la kwanza kwa zoo badala ya kuingilia Italian unazunguka sana.

Niko block 14 ni muruwa kabisa na dry all seasons,
 
Sisi upande wetu huo, alidai hana sehemu ya kuhifadhi vifaa, mheshima mmoja akajitolea hadi sasa hakuna nguzo wala vifaa....!! Inakera sana
Hii nchi ni kama ina laana,watu wakijenga kwenye maeneo ambayo hayapimwa wanabomolewa,ukijenga maeneo ya yaliyopimwa hupati huduma za kijamii,ni tatizo kubwa sana,hivi kila sehemu mpaka magufuli aje aongeee au atoe tamko?wenyewe hatuwezi kujiendesha?
 
Business as usual,wanajisahau kama wako utawala ule kumbe ni Hapa kasi tu soon watatumbuliwa.
 
Nimeongea na injinia wa Pspf amenihakikishia wana mawasiliano ya karibu na manispaa watalekebisha soon.

By the way kama unafika kigenzi kuna shortcut ya kuingilia tuta la kwanza kwa zoo badala ya kuingilia Italian unazunguka sana.

Niko block 14 ni muruwa kabisa na dry all seasons,
Wataleta kitu gani?umeme,umeshaona ratiba ya greda kuja kuchimba hyo barabara ya kutoka Taliani hadi mwisho wa mradi wa nyumba za PSPF?
Ratiba yao walisema wangejenga barabara kwa siku mbili,ssa jiulize barabara ya km 4 unaitengeneza kwa siku mbili?
Huo mradi wa umeme ni kama kudhalilishana tu,
 
Business as usual,wanajisahau kama wako utawala ule kumbe ni Hapa kasi tu soon watatumbuliwa.
Sijui tuna laaana gani tu,Yale maeneo yamepangwa vizuri kabisa,ila mapori yake mpaka balaa,ndio mwanzo wa kuhifadhi alshabaab kwenye Yale mapori,sijui mlioko huko mnaishi vipi hasa giza linapoingia.
 
Sijui tuna laaana gani tu,Yale maeneo yamepangwa vizuri kabisa,ila mapori yake mpaka balaa,ndio mwanzo wa kuhifadhi alshabaab kwenye Yale mapori,sijui mlioko huko mnaishi vipi hasa giza linapoingia.
Kwani wazee wako huko kijijini kusiko hata na umeme wanaishi vipi?
Nakumbuka kuna jamaa yangu by that time yeye alikuwa ana ajira nzuri na uchumi mzuri nilimpeleka Kinyerezi mwisho mtaa wa nyuma ya Safari pub alikataa shamba kubwa tu kwa milioni 5 tu.

Hana tofauti na akili ulizonazo wewe, nenda kaulize bei ya kiwanja leo Kinyerezi na siyo shamba maana hakuna mashamba tena.
 
Nimeongea na injinia wa Pspf amenihakikishia wana mawasiliano ya karibu na manispaa watalekebisha soon.

By the way kama unafika kigenzi kuna shortcut ya kuingilia tuta la kwanza kwa zoo badala ya kuingilia Italian unazunguka sana.

Niko block 14 ni muruwa kabisa na dry all seasons,
Matola
Kwa wanaokaa block 18 na 19 hata wapite wapi msimu wa mvua lazima madimbwi ya maji wayaoge tu,
Mmi namuomba Mh Makonda atembeleee huku siku moja aone jinsi watu wanavyoteseka na giza,wao wakiwa huko uzunguni ya kwetu hawayajui,
 
Kwani wazee wako huko kijijini kusiko hata na umeme wanaishi vipi? Wewe ni ********.

Nakumbuka kuna jamaa yangu by that time yeye alikuwa ana ajira nzuri na uchumi mzuri nilimpeleka Kinyerezi mwisho mtaa wa nyuma ya Safari pub alikataa shamba kubwa tu kwa milioni 5 tu.

Hana tofauti na akili ulizonazo wewe, nenda kaulize bei ya kiwanja leo Kinyerezi na siyo shamba maana hakuna mashamba tena.
Matola
Ssa matusi ya nn tena?sio.kwamba watu wanafurahia,ni kushagaaa kwa nn kuna mapori na miradi ya umeme haitekelezwi,au kwa vile wwe umeshaupata ndio unafikia mpaka stage ya kutukana wenzako?
Sio.sawa kabisa!
 
Matola
Kwa wanaokaa block 18 na 19 hata wapite wapi msimu wa mvua lazima madimbwi ya maji wayaoge tu,
Mmi namuomba Mh Makonda atembeleee huku siku moja aone jinsi watu wanavyoteseka na giza,wao wakiwa huko uzunguni ya kwetu hawayajui,
Waziri wa ardhi Lukuvi awanyang'anye viwanja walioacha mapori hiyo ndio dawa, hii ni tamaa ya watumishi wa wizara ya ardhi kujimegea viwanja na wanashindwa kuviendeleza. Hii ni roho mbaya ya kiswahili tu, wapo watu wengi wanahitaji vile viwanja lakini vyote vina watu na hawaviendelezi wala hawavisafishi.
 
Waziri wa ardhi Lukuvi awanyang'anye viwanja walioacha mapori hiyo ndio dawa, hii ni tamaa ya watumishi wa wizara ya ardhi kujimegea viwanja na wanashindwa kuviendeleza. Hii ni roho mbaya ya kiswahili tu, wapo watu wengi wanahitaji vile viwanja lakini vyote vina watu na hawaviendelezi wala hawavisafishi.
Pamoja na hilo,hata huduma za jamii hazijakaa sawa sana,angalia ile picha ya mkuu @chechemtungi una ki paso chako unapita vipi msimu wa mvua?
Halafu kwa nni mpaka Leo hiii hakuna umeme?
Na mbaya zaidi kuna mbunge wa ukawa ambae ni ki la za hamna mfano, hata akiulizwa kuhusu maendeleo ya mambo ya kule hajui chochote,naamini wana ukonga watajilaumu sana kuchagua yule ki la za
 
Pamoja na hilo,hata huduma za jamii hazijakaa sawa sana,angalia ile picha ya mkuu @chechemtungi una ki paso chako unapita vipi msimu wa mvua?
Halafu kwa nni mpaka Leo hiii hakuna umeme?
Na mbaya zaidi kuna mbunge wa ukawa ambae ni ki la za hamna mfano, hata akiulizwa kuhusu maendeleo ya mambo ya kule hajui chochote,naamini wana ukonga watajilaumu sana kuchagua yule ki la za
Ukichanganya siasa na mambo ya Buyuni mimi nitakuona ni zoba tu na hujui unasimamia nini.

Mimi nipo block 14 na huduma ya umeme wa TANESCO napata kama kawaida.

Changamoto za Buyuni haziwezi kutatuliwa kwa midadi ya kisiasa, kama issue ni umeme jiulize kwa nini Chanika umeme upo hadi Zingiziwa umeme umefika, why part of buyuni haina umeme? Hili siyo swala la kisiasa unaleri.
 
4cc32dc4928cdec9c94dcffa7dbec7f3.jpg


@lambertmende labda Matola ana V8 maana buyuni nako kuna wanene si haba,ssa wwe na kipaso chako ndio balaa,na hata huo.umeme umewekwa kwa mafungu,wenye nafasi walishachangamka na wakapata,si unaona hata maeneo ya bafanabafana na yule jamaa wa mbele kule,nafikiri ni block no 17,walivuta mapema tu,ssa walala hoi ndio.mpaka neema ya mungu ishuke,na kwa kuwa masalia ya ufisadi bado yapo mtakesha sana na giza la huko.
 
Sijui tuna laaana gani tu,Yale maeneo yamepangwa vizuri kabisa,ila mapori yake mpaka balaa,ndio mwanzo wa kuhifadhi alshabaab kwenye Yale mapori,sijui mlioko huko mnaishi vipi hasa giza linapoingia.
Acha tu kiongozi,juzi nilimsikiliza Hapi Ally DC kiukweli ametoa mtazamo mzuri sana ule wa kuvunja Tandale na manzese yote watafute muwekezaji aweke mall pale ili waondoe slams kiukweli ni good idea sana,na nikimuomba makonda sehemu zote zilizopimwa hivi karibuni kwa dar waweke miundombinu kule,viwanja vinapimwa lakini barabara hakuna,umeme hakuna kama hawapeleki miundombinu kulikuwa na haja gani ya kuwaondoa watu na kuwalipa fidia? Yaani serikali wana Magreda,Wana mainjinia wa kila aina,wana madereva na wakandarasi wa kutosha lakini kuleta kijiko/greda kuchonga barabara nao ni ngumu,umeme/majiyapo kilometer moja tu kufika kwenye viwanja vya maradi lakini inachukua miaka hadi mitatu kufika,kweli chizi karogwa tena.
 
mtu mwenye interest na buyuni ani PM nauza 1700 sqm bei Poa kabisa umeme, maji tapo nice neighbourhood.... mita 800 from tarmac road..
 
Ukichanganya siasa na mambo ya Buyuni mimi nitakuona ni zoba tu na hujui unasimamia nini.

Mimi nipo block 14 na huduma ya umeme wa Tanesco napata kama kawaida.

Changamoto za Buyuni haziwezi kutatuliwa kwa midadi ya kisiasa, kama issue ni umeme jiulize kwa nini Chanika umeme upo hadi Zingiziwa umeme umefika, why part of buyuni haina umeme? Hili siyo swala la kisiasa unaferi.
Hata kama Siasa hazipo lakini.zina nafasi yake,nafasi ya mbunge kwenye eneo lake iko wapi?mradi wa umeme sio tsh 10 ambao unaweza ukatolewa na mtu mmoja au watatu,halafu unaposema kuna midadi ya kisiasa unakosea,ushawahi kusikia au kumuona mbunge wa ukonga hata akitembelea tu maeneo ya huko?yaani yeye na wale wa Ccm hawana tofauti kabsa,tena bora wangechagua wa CCM angalau wangeweza hata kumuomba JPM na angesikia.
 
Back
Top Bottom