Something is wrong. Niko kisiwani Goziba ambako TANESCO wameanzisha mradi wa umeme wa REA kwa kutumia SOLAR PANEL (umeme wa jua). Katika hali ya kushangaza na kutia simanzi na kusikitisha sana, umeme wa huku unit moja ni Tshs 3,500/=, sijakosea ni Tsh 3,500/=
Hoja waliyonayo TANESCO ni kuwa wanataka kurudisha gharama zao mapema.
Mwanzoni kulikuwa na umeme wa jenereta zile za diesel ambazo zilikuwa zinatupatia umeme kwa gharama ya Tshs 10000 kwa mwezi kwa wale wa taa mbili mpaka tatu, na wale wenye maduka na bar gharama ilikuwa Tsh 30000 mpaka 50000 kwa mwezi kulingana na wingi wa vitu vyako, lakini serikali wamewapiga marufuku watu hao kwa kisingizio cha uchafuzi wa mazingira.
Meneja wa TANESCO Mkoa wa Kagera tunaomba ushughulikie suala hili kwa undani ili Wananchi walioko Goziba wafaidi kodi zao na wagawane keki ya taifa sawa na Watanzania waliko Namtumbo maana wananchi wa huku wanajiona siyo Watanzania.
Naomba kuwasilishaa
Hoja waliyonayo TANESCO ni kuwa wanataka kurudisha gharama zao mapema.
Mwanzoni kulikuwa na umeme wa jenereta zile za diesel ambazo zilikuwa zinatupatia umeme kwa gharama ya Tshs 10000 kwa mwezi kwa wale wa taa mbili mpaka tatu, na wale wenye maduka na bar gharama ilikuwa Tsh 30000 mpaka 50000 kwa mwezi kulingana na wingi wa vitu vyako, lakini serikali wamewapiga marufuku watu hao kwa kisingizio cha uchafuzi wa mazingira.
Meneja wa TANESCO Mkoa wa Kagera tunaomba ushughulikie suala hili kwa undani ili Wananchi walioko Goziba wafaidi kodi zao na wagawane keki ya taifa sawa na Watanzania waliko Namtumbo maana wananchi wa huku wanajiona siyo Watanzania.
Naomba kuwasilishaa