TANESCO mkoa wa Mara hususani wilaya ya Bunda Mashariki na Serengeti vijijni limekuwa ni kero

Bangila

Member
Mar 20, 2014
99
111
Kwanza hongera na pole kupewa wizara nyeti na ngumu. Nirudi kwenye malalamiko yangu hili shirika la umeme TANESCO mkoa wa Mara hususani wilaya ya Bunda Mashariki na Serengeti vijijni limekuwa ni kero kwa sisi watumiaji. Umeme unakatika hovyo na hawajali. Ninavyongea hakuna umeme toka juzi usiku baada ya kunyesha mvua. Walirudisha mchana kwa saa moja baadae wakakata tena na haujarudi. Kila siku za wikiendi umeme haupo kutwa mzima.

Upepo au mvua kidogo ikinyesha basi mnalala giza. Nafahamu kulikuwa na uafadhali kidogo mwanzoni mwa mwaka 2016 lakini kuanzia mwaka 2019 mpaka Sasa shida. Naamini wanakuchukulia poa lakini Sasa hivi wananchi wanahusisha na uwepo wa Mama Samia madarakani. Usicheke na nyani utavuna mabua. Tunahitaji msaada wako.
 
Kwanza hongera na pole kupewa wizara nyeti na ngumu. Nirudi kwenye malalamiko yangu hili shirika la umeme TANESCO mkoa wa Mara hususani wilaya ya Bunda Mashariki na Serengeti vijijni limekuwa ni kero kwa sisi watumiaji. Umeme unakatika hovyo na hawajali. Ninavyongea hakuna umeme toka juzi usiku baada ya kunyesha mvua. Walirudisha mchana kwa saa moja baadae wakakata tena na haujarudi. Kila siku za wikiendi umeme haupo kutwa mzima.

Upepo au mvua kidogo ikinyesha basi mnalala giza. Nafahamu kulikuwa na uafadhali kidogo mwanzoni mwa mwaka 2016 lakini kuanzia mwaka 2019 mpaka Sasa shida. Naamini wanakuchukulia poa lakini Sasa hivi wananchi wanahusisha na uwepo wa Mama Samia madarakani. Usicheke na nyani utavuna mabua. Tunahitaji msaada wako.
Ndugu mpendwa Mteja wetu

Tunafurahia kukuhudumia kupitia kurasa zetu za mitandao ya kijamii, tafadhali onesha taarifa kamili kwa huduma bora.

Jina

Eneo

Wilaya

Namba ya simu

Tatizo

Toka lini

Namba ya taarifa

Ahsante sana

TANESCO Huduma kwa Wateja
 
Back
Top Bottom