Bangila
Member
- Mar 20, 2014
- 99
- 111
Kwanza hongera na pole kupewa wizara nyeti na ngumu. Nirudi kwenye malalamiko yangu hili shirika la umeme TANESCO mkoa wa Mara hususani wilaya ya Bunda Mashariki na Serengeti vijijni limekuwa ni kero kwa sisi watumiaji. Umeme unakatika hovyo na hawajali. Ninavyongea hakuna umeme toka juzi usiku baada ya kunyesha mvua. Walirudisha mchana kwa saa moja baadae wakakata tena na haujarudi. Kila siku za wikiendi umeme haupo kutwa mzima.
Upepo au mvua kidogo ikinyesha basi mnalala giza. Nafahamu kulikuwa na uafadhali kidogo mwanzoni mwa mwaka 2016 lakini kuanzia mwaka 2019 mpaka Sasa shida. Naamini wanakuchukulia poa lakini Sasa hivi wananchi wanahusisha na uwepo wa Mama Samia madarakani. Usicheke na nyani utavuna mabua. Tunahitaji msaada wako.
Upepo au mvua kidogo ikinyesha basi mnalala giza. Nafahamu kulikuwa na uafadhali kidogo mwanzoni mwa mwaka 2016 lakini kuanzia mwaka 2019 mpaka Sasa shida. Naamini wanakuchukulia poa lakini Sasa hivi wananchi wanahusisha na uwepo wa Mama Samia madarakani. Usicheke na nyani utavuna mabua. Tunahitaji msaada wako.