Black Mirror
JF-Expert Member
- Oct 17, 2019
- 833
- 1,041
Salaam mabibi na mabwana, Salaam Mh Kalemani, salaam Dada Subira Mgalu, Rea na Tanesco
Miaka nenda miaka rudi Tanesco mmejificha kwenye kivuli cha kuwa hamna nguzo ndiyo maana umeme wa REA na Tanesco hausambazwi vitongojini au vijijni km inavyotakuwa. Wateja wa Tanesco pia huambiwa na kucheleweshewa huduma ya kufungiwa umeme kwani mnadai hamna nguzo, si rahisi kusema hamna nyaya wala material nyingine bali mnasema hamna nguzo. Naomba kuelimishwa juu ya hili mana misitu yenye miti ni mingi sana hapa Tanzania lakini mnasema hamna nguzo. Mwanzoni niliamini kuna miti maalumu kwa kazi hiyo ndiyo maana mnasema hamna nguzo, nilistaajabu baada ya kuona nguzo ni miongoni mwa miti ya Karatusi ambayo imetapakaa kila kona ya nchi hii kuliko karibia mti wowote hapa Tanzania. Je, inakuwaje mnaseama hamna nguzo? Je,hizo nguzo mnazosema ninyi zina sifa zipi ambazo huwa vigumu kuzipata kwa wakati?
Ningeomba shirikia hili lije na majibu juu ya kero hii, serikali ilikuja na jambo jema sana la umeme wa REA lakini mpaka sekunde hii kati ya takribani vijiji 12,380 vya nchi hii vingi havina umeme japo inakadriwa ni karibia vijiji elfu 8 vina umeme tayari lakini huu ni umeme wa kwenye makaratasi! Na hii ningetamani Mawaziri, Makatibu na Viongozi wengine wajue hadi ikiwezekana na Mh Rais ajue kuwa umeme unasimikwa tu kwenye maeneo ya shule,zahanati nk sehemu muhimu kwenye kijiji lakini maeneo mengi yanabaki bila umeme. Unakuta kwenye kijiji ni kama 2% tu wanaopata umeme ila 98% wanabaki bila umeme. Ni vijiji vichache sana ambavyo hupata umeme kwa 100% na ukiona hivyo jua kuna msukumo flani nyuma yake. Ningeomba sote kwa pamoja tutafakari haya
1) Kwanini ukosefu wa nguzo umekuwa ni kigezo kikuu cha kusababisha watu wasipewe huduma hii muhimu?
2) Je, ni miti aina gani hutakiwa kwa ajili ya kupata hizo nguzo?
3) Hapa Tanzania hakuna uwezekano wa kupata nguzo hizo kwa urahisi?
4) Wakandarasi huelekezwa kusambaza umeme kwenye maeneo muhimu tu?
5) Kama nguzo za miti imekuwa changamoto hatuwezi kupata mbadala wa nguzo?
6)Kwanini kila mtanzania anayehitaji umeme asifungiwe umeme hata kwa mkopo alafu mkawa na mkataba wa jinsi ya kulipia taratibu?
7)Mbona huwa hatuambiwi hakuna nyaya, au materials nyingine tofauti na nguzo?
8) Mnajua umeme ulivyo nguzo muhimu sana katika kuinua maisha ya kila Mtanzania kuliko karibia kitu chochote?
9)Kama Tanesco inaelemewa kwanini wasitafute wasaidizi wengine?
Mh Kalemani na Mh Mgalu hii kazi ni ngumu kweli lakini jaribuni walau kuwa wazi kwa raia kuliko kuwa mnawapa matumaini hewa juu ya kila raia kupata huduma ya REA.
Miaka nenda miaka rudi Tanesco mmejificha kwenye kivuli cha kuwa hamna nguzo ndiyo maana umeme wa REA na Tanesco hausambazwi vitongojini au vijijni km inavyotakuwa. Wateja wa Tanesco pia huambiwa na kucheleweshewa huduma ya kufungiwa umeme kwani mnadai hamna nguzo, si rahisi kusema hamna nyaya wala material nyingine bali mnasema hamna nguzo. Naomba kuelimishwa juu ya hili mana misitu yenye miti ni mingi sana hapa Tanzania lakini mnasema hamna nguzo. Mwanzoni niliamini kuna miti maalumu kwa kazi hiyo ndiyo maana mnasema hamna nguzo, nilistaajabu baada ya kuona nguzo ni miongoni mwa miti ya Karatusi ambayo imetapakaa kila kona ya nchi hii kuliko karibia mti wowote hapa Tanzania. Je, inakuwaje mnaseama hamna nguzo? Je,hizo nguzo mnazosema ninyi zina sifa zipi ambazo huwa vigumu kuzipata kwa wakati?
Ningeomba shirikia hili lije na majibu juu ya kero hii, serikali ilikuja na jambo jema sana la umeme wa REA lakini mpaka sekunde hii kati ya takribani vijiji 12,380 vya nchi hii vingi havina umeme japo inakadriwa ni karibia vijiji elfu 8 vina umeme tayari lakini huu ni umeme wa kwenye makaratasi! Na hii ningetamani Mawaziri, Makatibu na Viongozi wengine wajue hadi ikiwezekana na Mh Rais ajue kuwa umeme unasimikwa tu kwenye maeneo ya shule,zahanati nk sehemu muhimu kwenye kijiji lakini maeneo mengi yanabaki bila umeme. Unakuta kwenye kijiji ni kama 2% tu wanaopata umeme ila 98% wanabaki bila umeme. Ni vijiji vichache sana ambavyo hupata umeme kwa 100% na ukiona hivyo jua kuna msukumo flani nyuma yake. Ningeomba sote kwa pamoja tutafakari haya
1) Kwanini ukosefu wa nguzo umekuwa ni kigezo kikuu cha kusababisha watu wasipewe huduma hii muhimu?
2) Je, ni miti aina gani hutakiwa kwa ajili ya kupata hizo nguzo?
3) Hapa Tanzania hakuna uwezekano wa kupata nguzo hizo kwa urahisi?
4) Wakandarasi huelekezwa kusambaza umeme kwenye maeneo muhimu tu?
5) Kama nguzo za miti imekuwa changamoto hatuwezi kupata mbadala wa nguzo?
6)Kwanini kila mtanzania anayehitaji umeme asifungiwe umeme hata kwa mkopo alafu mkawa na mkataba wa jinsi ya kulipia taratibu?
7)Mbona huwa hatuambiwi hakuna nyaya, au materials nyingine tofauti na nguzo?
8) Mnajua umeme ulivyo nguzo muhimu sana katika kuinua maisha ya kila Mtanzania kuliko karibia kitu chochote?
9)Kama Tanesco inaelemewa kwanini wasitafute wasaidizi wengine?
Mh Kalemani na Mh Mgalu hii kazi ni ngumu kweli lakini jaribuni walau kuwa wazi kwa raia kuliko kuwa mnawapa matumaini hewa juu ya kila raia kupata huduma ya REA.