ukikaidi utapigwa2
JF-Expert Member
- Feb 24, 2015
- 13,833
- 27,252
Tanescrow again
Dogo anajali muonekano kuliko vitendoTuna huyu Waziri yeye ni show off tu za kuvaa mashati meupe ya mikono mirefu na kuyakunja hadi usawa wa viwiko kama Barack Obama, hakuna kitu.
Tunahitaji Mawaziri ambao wako down to earth na wanaleta mabadiliko hapo hapo ya upatikani wa nishati, kila kitu tunacho tatizo nini? Kuzurura zurura kwenye nchi za watu na kuomba omba haiwezi kutusaidia.
Kilimanjaro kila siku wanakata umeme tena kutwaaa , tumeanza kuzoea kwa kweli hata kama hawatoi taarifaMikoa 11 ya Tanzania itakosa umeme kwa saa 12 Novemba 15 mwaka huu kutokana na matengenezo yanayofanywa na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) katika njia ya kusafirisha umeme wa kilovolti 220 kutoka Kidatu hadi Iringa.
Umeme utakatika kuanzia saa 12 alfajiri hadi saa 12 jioni ili kupisha matengenezo yanayolenga kuboresha hali ya upatikanaji wa umeme katika gridi ya Taifa.
Kutokana na matengenezo hayo kutakuwa na upungufu wa umeme kwa baadhi ya maeneo ya mikoa ya Mbeya, Njombe, Ruvuma, Singida, Shinyanga, Mwanza, Mara, Tabora, Arusha Kilimanjaro na Tanga.
TANESCO imewaomba radhi wateja wake kwa usumbufu utakaojitokeza.
===
MATENGENEZO NJIA YA USAFIRISHAJI UMEME KIDATU-IRINGA
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawafahamisha wateja wake kuwa, Jumatatu Novemba 15, 2021 kutakuwa na matengenezo ya njia ya kusafirisha umeme wa kilovolti 220 kutoka Kidatu hadi Iringa kuanzia saa 12:00 asubuhi hadi saa 12:00 jioni.
SABABU: Kuboresha hali ya upatikanaji wa umeme katika gridi ya Taifa. Kutokana na matengenezo hayo kutakuwa na upungufu wa umeme kwa baadhi ya maeneo ya mikoa ya Mbeya, Njombe, Ruvuma, Singida, Shinyanga, Mwanza, Mara, Tabora, Arusha, Kilimanjaro na Tanga. Tunawaomba radhi watejawetu kwa usumbufu utakaojitokeza.
Tafadhali usishike wala kukanyaga waya uliokatika, toa taarifa dawati la dharura la wilaya kwa msaada zaidi au Kituo cha Miito ya Simu Makao Makuu:+255 222 194 400 na +255 768 985 100
Source:
Ingekuwa enzi za Magu, ungesikia Magu ana chuki na watu wa kaskazini...Kilimanjaro kila siku wanakata umeme tena kutwaaa , tumeanza kuzoea kwa kweli hata kama hawatoi taarifa
Mkuu mimi tayari nimesha vuta kamtambo kangu ka Sun king solar... Deposit elfu 40 wanakufungia taa zako 5, charger ya simu na karedio ka kupata news...Ondoeni na nyaya kabisa tutanunua solar
Ni kweli kabisa tunaendelea kukumbuka zile 1.3 Trilioni zilizoyeyuka mbele ya macho ya Prof Assad.... Namshukuru Nape kwa kutaka uchunguzi wa mikopo yootee aliyochukua ufanyike haraka sanaa...
Ni kweli kabisa tunaendelea kukumbuka zile 1.3 Trilioni zilizoyeyuka mbele ya macho ya Prof Assad.... Namshukuru Nape kwa kutaka uchunguzi wa mikopo yootee aliyochukua ufanyike haraka sanaa...
It will be a shamemakamba kuwa rais si alheri kuingia msituni
Apotee mara ngapi mkuuSisi Leo tumeshinda bila ya umeme toka asubuhi mpaka Sasa TANESCO
Mheshimiwa Makamba chukua hatua. Utapotea kisiasa mapema. Na Tanesco ndio kaburi lako.
Mabigwa wa kufeli hahaaYani serikali yetu hakuna jambo ambalo unaweza sema imefanikiwa kwa 90% yani si elimu, si maji, si afya, si umeme
Ufisadi wamepita 100%Yani serikali yetu hakuna jambo ambalo unaweza sema imefanikiwa kwa 90% yani si elimu, si maji, si afya, si umeme
Nakumbuka palikua na mgao wakati magu akiwepo sema alikua hatoi taarifa kwa wananchi.
Unaweza ni nionyesha hiyo t 1.3 kwenye ripoti CAG au highlight hiyo paragraph iliyosema t 1.3 ilipigwa.Ni kweli kabisa tunaendelea kukumbuka zile 1.3 Trilioni zilizoyeyuka mbele ya macho ya Prof Assad.... Namshukuru Nape kwa kutaka uchunguzi wa mikopo yootee aliyochukua ufanyike haraka sanaa...
Katafute mwenyewe hizo kimbukumbu.mtu kakwambia ni kumbukumbu wewe unakazana akuonyeshe.Au kwavile mlificha taarifa ndo maana unashupaza shingo hapa.Unaweza ni nionyesha hiyo t 1.3 kwenye ripoti CAG au highlight hiyo paragraph iliyosema t 1.3 ilipigwa.