Wadau nimesikia Tanesco wako mipangoni kuongeza bei ya umeme. Kinachonisikitisha sio bei tu bali hata ratiba ya ukataji umeme haieleweki.Pili hi serikali imekua kama shule ya chekeckea mheshimiwa waziri nishati alisema makali ya mgao yatapungua kumbe ni uongo mtupu wanakata mpaka wanapitiliza sikuhizi. Tuliokua mkutanoni mlimani city ya 50yrs construction (engineers, architect, qs na wadau) mkuu wa nchi alitoa direct order ratiba ya mgao wa umeme iwekwe wazi na idara husika kwa wananchi pia nalo halijatekelezwa. Sasa mi nimekua na maswali mengi kuliko majibu hebu nifafanulieni kwa hoja.