TANESCO hili sio sawa

julaibibi

JF-Expert Member
Jun 16, 2020
2,606
3,399
Shirika letu ndio lilipaswa kuwa la kwanza kuwa walinzi wa mazingira. Hili suala limekuwa na ukakasi mkubwa ukataji miti bila kujali manufaa yake eti kisa waya upo juu uangaliwe upya

Miti ya mjini ni muhimu sana kupendezesha mandhari na kivuli. kama waya upo juu bajeti hio hio ya kuifyeka mngei prune kwa juu vizuuri sio kuifyeka kabisa nchi itakuwa jangwa. Kitengo cha mazingira kaeni tena muweke mikakati ya kuinusuru miti ya mjini.yaani idara ya mazingira imekosa kabisa mbinu?

Inusuruni miti ya mjini, miti ina faida sana kijamii,kiroho na kdhalika mimi kama bwana miti inaniuma sana hili jambo.

Nimepita mahali wamefyeka miti mikubwa mikubwa mjin kati si mngeikata juu huko
 
Miti mingine ni ya zamani line ndio imezikuta.sasa wangepunguza juu.dar es salaam mkoloni kuanzia mjeruman aliunda designated parks akaapanda miti mfano shaban Robert street jaalia wakate ile miti?? patakuwaje?
 
miti mingine ni ya zamani line ndio imezikuta.sasa wangepunguza juu.dar es salaam mkoloni kuanzia mjeruman aliunda designated parks akaapanda miti mfano shaban Robert street jaalia wakate ile miti? patakuwaje?
Hapo kosa ni la tanesco Kama waliikuta ilibidi waikate kipindi Cha ujenzi wa line maana kupunguza kwa juu nigarama inayo jirudia Kila mwaka.
 
Misitu ya hifadhi inageuzwa makazi na mapori tengefu yanageuzwa mashamba wewe unakuja kulia lia Miti kukatwa Mjini ni aibu. Wazungu wanajenga viwanda vikubwa vinavyochafua hali ya hewa kwa kiasi kikubwa sisi tukijenga stragglers gorge tunaambiwa tutaharibu uoto wa asili .....foolish mindset
 
Back
Top Bottom