Tanesco: hatujui mgawo utaisha lini

YeshuaHaMelech

JF-Expert Member
Oct 12, 2010
2,597
37
Elizabeth Ernest na Mwanaidi Abasi
SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco), limesema haijulikani ni mgawo wa nishati hiyo ambayo mkoani Dar es Salaam, imekuwa ikipatikana kwa njia hiyo, utamalizika lini.

Kauli hiyo inakuja huku mgano huo ulioathiri shughuli mbalimbali zikiwezo za uchumi ambazo uendeshaji wake umekuwa ukitegemea umeme, ukiwa umeingia katika wiki ya pili.

Mgawo huo ulioanza takribani wiki mbili zilizopita unadaiwa kuwa umesababishwa na ubovu wa mitambo katika gridi ya taifa.

Meneja Uhusiano wa Tanesco, Badra Masoud aliiambia Mwananchi juzi kuwa mgawo huo utamalizika wakati wowote bila kutaja muda halisi.

"Mgawo utamalizika muda wowote kuanzia leo (juzi) kwa sababu sijui ni lini mitambo iliyoharibika itakuwa imekamilika,"alisema.

Alisema mgawo huo umetokana na ubovu wa mitambo ya umeme iliyoko Tegeta, jijini Dar es Salaam na kwamba mafundi wanaendelea na jitihada za kuifanyia matengenezo ya mitambo hiyo.

"Kwa sababu bado mitambo inaendelea kutengenezwa, sijui mafundi watakamilisha lini matengenezo hayo na ni vigumu kwa mafundi kusema kama matengenezo hayo yatamalizika lini,"alisema.

Masoud alisema sababu kubwa ya kufanyika kwa mgawo huo ni ubovu wa mitambo ambayo kwa sasa iko katika matengenezo na kwamba itakapokamilika ndipo watakapo sitisha mgawo huo.

Hivi karibuni shirika hilo lilitoa taarifa kuwa mgawo wa umeme, umetokana na kuharibika kwa baadhi ya mitambo ya Songas iliyopo Ubungo, jjini Dar es Salaam.

Pia taarifa hizo zilisema kupungua kwa kina cha maji katika mabwawa ya Pangani na Kihansi na kuisha kwa mafuta katika mtambo wa IPTL, kumechangia kuongezeka kwa tatizo hilo.
Source:
 
Elizabeth Ernest na Mwanaidi Abasi
SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco), limesema haijulikani ni mgawo wa nishati hiyo ambayo mkoani Dar es Salaam, imekuwa ikipatikana kwa njia hiyo, utamalizika lini.

Kauli hiyo inakuja huku mgano huo ulioathiri shughuli mbalimbali zikiwezo za uchumi ambazo uendeshaji wake umekuwa ukitegemea umeme, ukiwa umeingia katika wiki ya pili.

Mgawo huo ulioanza takribani wiki mbili zilizopita unadaiwa kuwa umesababishwa na ubovu wa mitambo katika gridi ya taifa.

Meneja Uhusiano wa Tanesco, Badra Masoud aliiambia Mwananchi juzi kuwa mgawo huo utamalizika wakati wowote bila kutaja muda halisi.

"Mgawo utamalizika muda wowote kuanzia leo (juzi) kwa sababu sijui ni lini mitambo iliyoharibika itakuwa imekamilika,"alisema.

Alisema mgawo huo umetokana na ubovu wa mitambo ya umeme iliyoko Tegeta, jijini Dar es Salaam na kwamba mafundi wanaendelea na jitihada za kuifanyia matengenezo ya mitambo hiyo.

"Kwa sababu bado mitambo inaendelea kutengenezwa, sijui mafundi watakamilisha lini matengenezo hayo na ni vigumu kwa mafundi kusema kama matengenezo hayo yatamalizika lini,"alisema.

Masoud alisema sababu kubwa ya kufanyika kwa mgawo huo ni ubovu wa mitambo ambayo kwa sasa iko katika matengenezo na kwamba itakapokamilika ndipo watakapo sitisha mgawo huo.

Hivi karibuni shirika hilo lilitoa taarifa kuwa mgawo wa umeme, umetokana na kuharibika kwa baadhi ya mitambo ya Songas iliyopo Ubungo, jjini Dar es Salaam.

Pia taarifa hizo zilisema kupungua kwa kina cha maji katika mabwawa ya Pangani na Kihansi na kuisha kwa mafuta katika mtambo wa IPTL, kumechangia kuongezeka kwa tatizo hilo.
Source:

I dont buy this crap kwani mjini hapa hakuna mafuta kiasi cha kuifanya mitambo IPTL ishindwe ku-operate au waseme tu wameshindwa kuwalipa hela za mafuta
 
kazi kweli...na bado tuna miaka mitano.
Mungu atusaidie kuvumilia haya maumivu wakati tukitafuta jinsi ya kuondokana na umaskini ktk nchi tajiri kama hii.
One day...the day is coming!
 
Hii inaonyesha jinsi gani watu wanavyofanya kazi kwa kubahatisha;kwasababu kitaalamu hawa mafundi wanatakiwa waitathmini kazi kujua mahitaji na kujua itachukua muda gani kutekeleza kazi hiyo.Sasa hii habari ya kuwaambia wananchi hatujui muda gani tatizo litakuwa limeisha si kauli nzuri hata kidogo.
Na kama ni hivyo ina maana Tanesco hawajui tatizo ni nini na wanatakiwa kufanya nini!!Labda ili kuwepo na ufanisi ni bora shirika libinafsishwe na kuruhusiwe wawekezaji kataika sekta ya umeme kama yalivyo makampuni ya simu dhidi ya TTCL;hapa nafikiri akili zitarudi katika mstari.
 
Hii inaonyesha jinsi gani watu wanavyofanya kazi kwa kubahatisha;kwasababu kitaalamu hawa mafundi wanatakiwa waitathmini kazi kujua mahitaji na kujua itachukua muda gani kutekeleza kazi hiyo.Sasa hii habari ya kuwaambia wananchi hatujui muda gani tatizo litakuwa limeisha si kauli nzuri hata kidogo.
Na kama ni hivyo ina maana Tanesco hawajui tatizo ni nini na wanatakiwa kufanya nini!!Labda ili kuwepo na ufanisi ni bora shirika libinafsishwe na kuruhusiwe wawekezaji kataika sekta ya umeme kama yalivyo makampuni ya simu dhidi ya TTCL;hapa nafikiri akili zitarudi katika mstari.

Ndugu yangu TANESCO iliacha kuendeshwa na wataalamu toka alipokufa yule SALVATORY MOSHA miaka ile ya kale....Baada ya hapo wanasiasa waakichukua Rasmi wakiongozwa na JK huyuhuyu mnae mlilia hapa
 
Back
Top Bottom