Mzee wa Kale
Member
- Feb 7, 2009
- 44
- 0
Wakuu heshima kwenu,
Nilifika Tandale Sokoni majira ya saa 11, jioni nikiwa na ndugu zangu niliotoka nao Zanzibar, ambapo kesho yake alfajiri walitakiwa kuondoka kwenda nje ya nchi, sasa tulikwenda huko kwa ajili ya kununua angalau vijizawadi kidogo, tulifika pale tukiwa na Tax driver ambaye tulimchukua kutoka maeneyo ya Kwa Mtogole, baada ya kukamilisha kununua nafaka na kupakia kwenye Tax, na kuanza safari ya kurudi hotelini mambo yakaanza, alikuja jamaa mmoja akavamila gari kwa ghafla akadai gari yetu imemkanyagia embe zake, hatukuona embe zilizokanyangwa, akamvamia driver wetu akampora simu, baada ya muda kidogo kundi kubwa la vijana likaja kuzunguka gari ambapo sisi tukiwa ndani wakitaka tutoke ili kumsaidia driver wetu, mimi nikawauliza kama ni msaada kwa nini nyinyi ambao ndio mko wengi msimsaidie, nikawaambia ndugu zangu fungeni vioo wekeni lock inawezekana sisi ndio wametulenga huyo driver ni mchezo tu a kuigiza, kwa kweli hapo tukapona na tukaondoka salama.
Natafakari sipati jibu maisha ya vijana wetu utu kwao haupo, wakimwona mtu na vijisenti wako tayari kumtoa roho ili mradi siku ipite, Wana JF tunawezaje kuwasaidia vijana hawa ili kupunguza tatizo linaloikabili nchi yetu kwa wakati wa sasa na ujao?
Nilifika Tandale Sokoni majira ya saa 11, jioni nikiwa na ndugu zangu niliotoka nao Zanzibar, ambapo kesho yake alfajiri walitakiwa kuondoka kwenda nje ya nchi, sasa tulikwenda huko kwa ajili ya kununua angalau vijizawadi kidogo, tulifika pale tukiwa na Tax driver ambaye tulimchukua kutoka maeneyo ya Kwa Mtogole, baada ya kukamilisha kununua nafaka na kupakia kwenye Tax, na kuanza safari ya kurudi hotelini mambo yakaanza, alikuja jamaa mmoja akavamila gari kwa ghafla akadai gari yetu imemkanyagia embe zake, hatukuona embe zilizokanyangwa, akamvamia driver wetu akampora simu, baada ya muda kidogo kundi kubwa la vijana likaja kuzunguka gari ambapo sisi tukiwa ndani wakitaka tutoke ili kumsaidia driver wetu, mimi nikawauliza kama ni msaada kwa nini nyinyi ambao ndio mko wengi msimsaidie, nikawaambia ndugu zangu fungeni vioo wekeni lock inawezekana sisi ndio wametulenga huyo driver ni mchezo tu a kuigiza, kwa kweli hapo tukapona na tukaondoka salama.
Natafakari sipati jibu maisha ya vijana wetu utu kwao haupo, wakimwona mtu na vijisenti wako tayari kumtoa roho ili mradi siku ipite, Wana JF tunawezaje kuwasaidia vijana hawa ili kupunguza tatizo linaloikabili nchi yetu kwa wakati wa sasa na ujao?