winnie9999
Member
- Nov 27, 2021
- 65
- 102
- Thread starter
- #21
TAMTHILIA: CHALLENGE MADE.
MUANDISHI: WINIFRIDA FRANCIS THOBIAS.
SEHEMU: 9 $ 10
WhatsApp no : 0746115688.
Mr.kivuli alishangazwa sana na kitendo cha jasmini kumshika mkono lakini jasmini alipoona Mr.kivuli anaonekana kuwa na hasira japo anajitahidi kufichaficha jasmini aliangua kicheko na kumwambia Mr.kivuli samahani ila ni kwausalama wa mtoto lazima unawe kabla ya kumshika hiyo itasaidia akue bila maambukizi ya aina yeyote. Mr.kivuli alicheka sana na kila mtu aliyekuwa pale pia alicheka na hapohapo Mr.kivuli hasira zilimpotea na kuchukulia kama tabia ya jasmini inatokana na upendo wake kwa mtoto wake, hivyo aliachana na mtoto wa grace nakuwaomba wakinamama wote wapumzike tu, kwani yeye anamizunguko yake ndani ya hospitali . Basi wakinamama walibakia wote hodini lakini grace wakati walinzi wakihangaika na msafara wa Mr.kivuli yeye alitoroka na pikipiki ya kununulia mahitaji muhimu akaelekea kwenye kampuni yake ya usafirishaji ya Graja kwani alipigwa simu na kujulishwa kuna proposal mpya ya kibiashara kutoka katika kampuni ya Culture.
upande wa pili Mr.kivuli alitembea na james hospitali nzima na kisha james alichagua chumba kitakacho mtoshea yeye kufanya mambo yake na baada ya hapo Mr.kivuli alielekea ofisini akiwa yeye, Jackbosi pamoja na james lakini baada ya wote kukaa Mr.kivuli alimuomba Jackbosi akaendelee nashughuli zake za kila siku kwani alikuwa na mazungumzo ya kibinafsi na james. Jackbosi aliondoka lakini kumbe alikuwa ametegesha kamera kwani safari hii hakutaka kuonekana mjinga tena hivyo wakati kikao kinaendelea na yeye aliingia katika chumba ambacho kilikuwa hakina mtu nakuanza kuangalia na kusikiliza kila kilicho kuwa kinaongelewa na Mr.kivuli pamoja na james lakini ghafla wakati Jackbosi anasikiliza maongezi ya Mr.kivuli na james aliweka simu yake mfukoni nakukimbia moja kwa moja katika chumba cha wakina mama bila kugonga hodi aliusukuma mlango na kuwauliza grace yupo wapi, Ade akamwambia kuna kazi muhimu ameenda kuifanya kwenye kampuni , Jackbosi akawaambia hakikisheni wote mnaandaa vitu vyenu vya umuhimu leo usiku mnatoka hapa na hakuna yeyote anapaswa kukataa juu ya jambo hili kisha akamchukua Ade pamoja na mwenzie mmoja nakuwapa kazi ya kufungua tank za pikipiki zote na kuchukua mafuta kisha kuyaweka kwenye makopo aliyo wapa kwani yata wasaidia wakati wa kutoka hapo. baada ya Jackbosi kuwapa maelezo hayo alitoka na kwenda kukaa katika ofisi ya madaktari na muda haukupita mlinzi alimfuata na kumtaarifu kuwa baba yake alikuwa anamuita hivyo Jackbosi alielekea baba yake alipo na baba yake alimtaarifu kuwa kuanzia kesho James atakuja kuanza kazi yake hapa pamoja na wafanyakazi wake. Jackbosi alimwambia baba yake sawa lakini moyoni mwake aliweka kiapo kwamba ikifika kesho hospitali itakuwa imekwisha sahaulika. lakini kwa upande wa james alimwambia kinafki Jackbosi amsamehe kwakumkosea siku ya part kwani kuanzia sasa watakuwa wakionana mara nyingi. Jackbosi alicheka sana na kumwambia usijali tupo pamoja ni jambo dogo sana lililotokea Siku ile mbona mimi nilikusamehe hofu kwako tu. Mr.kuvuli yeye aliona kawaida kwa vijana kuongea maneno kama hayo hivyo alimwambia tu binti yake kafanya jambo zuri kumsamehe mapema james ukizingatia wao James ni mshirika mwenzao kwasasa. baada ya Mr.kivuli kuongea maneno hayo alimwambia James waondoke wakaendelee na majukumu mengine lakini pia akamwambia binti yake chukua likizo kuanzia kesho mama yako amekukumbuka sana . Jackbosi alionekana mwenye furaha sana nakumshukuru baba yake kwa kumpa likizo, lakini Baada tu ya Mr.kivuli kuondoka Jackbosi alijalibu kuwasiliana sana na grace lakini hakukuwa na majibu yeyote kwani grace alikuwa hapokei simu . Lakini kumbe grace nae alisahau kifaachake anachotumia kuwasiliana na watu kwenye droo yake ya mafaili ofisini kwake alipo kuwa akijiandaa kuelekea kwenye kikao kilichokuwa kinafanyika ili kutoa maamuzi kama kampuni yao itashirikiana na Culture company au haitakuwa tayari.
Maamuzi ya grace alikubaliana na kusaini makubaliano hayo lakini kama Mr.kivuli mwenyewe ataonyesha kujali na kuja mwenyewe kusaini makubaliano hayo ofisini kwake lakini kama hatakuwa tayari makubaliano hayata fanyika.
wawakilishi wa kampuni ya Culture waliona kama vile grace anadharau sana lakini grace hakuwa tayari kubadili sharti hilo na aliwapa masaa mawili wawe wamesha wasiliana na bosi wao nakutoa jibu kama bosi wao yuko tayari au la. kisha yeye akarudi ofisini kwake na kuendelea kupitia kazi mbalimbali hasahasa ambazo hazikupitia mikononi mwake .
Wawakilishi wa kampuni ya Culture walikuwa wakimpigia sana mwenyekiti wa kampuni ya Culture ambaye ni Mr.kivuli lakini kwabahati mbaya Mr.kivuli alikuwa ameacha simu yake ndani ya gari hivyo ilikuwa ngumu sana kuwasiliana nae kwa njia ya simu hivyo walikubaliana muwamkilishi mmoja aende kwenye kampuni kwani walikubaliana na Mr.kivuli baada ya makubaliano hayo watakutana nae kwenye ukumbi wa mikutano wa kampuni ya Culture .
Upande wa pili Jackbosi aliendelea na mipango yake ya kuhakikisha ana watorosha wakina mama wote usiku.
Baada ya lisaa limoja grace alirudi katika chumba cha mkutano wa makubaliano na kuwauliza kama wawakilishi wa kampuni ya Culture wamesha wasiliana na bosi wao lakini kwa bahati mbaya hawakuwa na jibu hivyo grace alisimama nakuwaambia makubaliano hayatakuwepo tena muda umeisha , lakini kabla
grace hajatoka nnje ya chumba cha makubaliano simu ya muwakilishi kutoka kampuni ya Culture iliita na muwakilishi huyo aliweka loud speaker kwani bosi wao Mr.kivuli alipiga na moja kwa moja Mr.kivuli alimwambia grace kesho ntakuja mimi mwenyewe kusaini mkataba , grace bila hata ya kuogopa alimwambia Mr.kivuli saa 3:00 asubuhi na usisahau naenda na muda. Mr.kivuli alikubaliana nae japo alipatwa na hasira sana kwani kwenye maisha yake hakuwahi kukutana na mtu wakumdharau , Siku zote watu wamekuwa wakimuheshimu lakini grace hakujali. Baada ya mkutano grace alielekea nyumbani kwao ili kuweza kuangalia hali ya baba yake pamoja na wakinamama wote walio kuwa wanaishi katika nyumba yao , wakati huo Jackbosi nae aliendelea kumtafuta grace mara kwa mara lakini grace hakuwa na kifaa cha mawasiliano.Jackbosi alifanya maamuzi ya kuendelea kupanga mipango yake ya kuwatoa wa kinamama wote hospitalini .
Mida ya saa mbili usiku Jackbosi alimuita mlinzi wake na kumwambia kaangalie wakinamama kama wapo. mlinzi alienda na aliporudi alimpa jibu kuwa wakinamama wote wapo, grace akamwambia chukua kufuli hili kawafungie muda huu utawafungulia asubuhi kisha Jackbosi akampa mlinzi ufunguo moja na yeye akachukua mmoja, mlinzi akaenda kuwafungia wakinamama kisha Jackbosi akamruhusu aende tu nnje kuendelea na shughuli nyingine . Mlinzi alipo tòka tu Jackbosi alielekea kwa wakinamama na kuwatoa wote kisha akaufunga mlango kama alivyo ufunga mlinzi wake na baada ya hapo akawatoa wakinamama wote nnje kupitia njia ya siri na kuwaingiza kwenye gari iliyo kuwa ikiwangojea upande huo. kisha akamchukua ade na mmama mmoja wakasaidiana kumwaga mafuta hospitali nzima na baada ya hapo akawaambia wakimbie na wala wasijali kuhusu yeye kwani atakuwa salama . Baada tu ya wakinamama kuondoka na gari iliyowabeba kutoka maeneo ya hospitalini Jackbosi alitupa njiti ya kibiriti ndani ya hospitali na kisha moto ukaanza Kuwaka walinzi na madaktari wote walikimbia kwani moto ulianza kwa kasi sana lakini Jackbosi yeye alitoka nnje ya geti la hospitalini na kunywa vidonge vilivyo mfanya azimie . Moja kati ya walinzi alimpigia Mr.kivuli na kumpa taarifa juu ya kilicho tokea lakini Mr.kivuli alimuuliza mlinzi huyo kuhusu Jackbosi na hapo ndipo mlinzi alipo mpa taarifa Mr.kivuli ya kuwa sikumuona wakati moto ulivyo anza lakini nakumbuka alikuwepo ndani ya hospitali , anaweza kuwa karibu ya hospitalini tu , kwani sisi tuliondoka kabisa eneo lile tupo njiani kuelekea kwenye kampuni kama ulivyotuambiaga .
mke wa Mr.kivuli aliposikia hayo alishindwa kuendelea kusubiri mipango ya mumewe alichukua gari nakuanza safari ya kuelekea hospitalini kumfuata binti yake wakati alipokuwa akiendelea kutafuta alipofika eneo la hospitalini alimuona Jackbosi akiwa amezimia na haraka alimchukua mwanae na kumkimbiza hospitalini kwani hakuwa amesaidika ukizingatia hospitali ilikuwa nnje kabisa ya Mji hakukuwa na watu wakuwasaidia baada ya janga hilo kuwakuta .
walipofika hospitalini Daktari alimwambia Mrs.kivuli binti yako yuko sawa japo anahitaji muda wa kupumzika kwani anaonekana amevuta hewa chafu ya kutosha atakuwa sawa anahitaji kupumzika tu.
wakati grace alipokuwa anataka kurudi hospitalini ghafla aliona kosta ikisimama nnje ya nyumba yake na alipofika nnje ili ajue nini kinaendelea alishangaa kuona ni wakinamama wote wamerudi, grace aliogopa sana na alipo jalibu kushika kifaa chake cha mawasiliano masikioni ili awasiliane na Jackbosi aligundua kifaa hicho hakipo na hapo ndo ilimbidi awe mpole na kuwasaidia wakinamama wengine kushuka kwenye gari hasahasa wale waliozaa kwa upasuaji.
kisha wote grace akawapa vyumba na baada ya hapo akamchukua mtoto wake pamoja na jasmini akawaingiza kwenye chumba chake kisha akawaambia wakinamama wote wapumzike tu watapewa kila wanacho kihitaji na asubuhi wataongea mambo mengi zaidi .
grace aliingia kwa jasmini akamuuliza ' imekuwaje' ?. lakini jasmini alimwambia ghafla Jackbosi alikuja akikutafuta mno naalipo ona hupatikani alituambia tujiandae anatutoa pale hospitalini leo na hospitali nayo mwisho wake ni leo tulihisi kama utani lakini kweli ilipofika saambili Jackbosi alikuja na kututoa wote kisha akawasha jengo la hospitali moto na nahisi mpaka sasa jengo la hospitali litakuwa limesha teketea kabisa.
grace hakuamini anachoambiwa hivyo alichukua pikipiki nakwenda kuhakikisha alichoambiwa ni kweli au kuna uongo ndani yake, lakini alipo fika eneo la hospitalini alikutana na majivu tu, grace alichukia sana na kuchukulia maamuzi ya Jackbosi ni ya kipumbavu sana na kuanzia hapo hakutaka kuwasiliana nae na akaamua kupanga mipango yake ya kumteketeza Mr.kivuli kwa muda wa mwezi .
wiki moja baadae Jackbosi alienda kumtembelea grace kwani alikuwa hampati kwenye simu lakini alipoingia ndani grace na Wakinamama wote walionekana kumchukia sana kwani waliisi yeye amewatoa pale ili wasimmalize baba yake hivyo kila alivyojalibu kuwaonyesha upendo wao walirejesha maneno ya chuki. Jackbosi alipoona amna mwenye furaha na yeye aliamua kuondoka lakini aliacha CD akawaambia kama wakipenda wanaweza kuangalia ni nzuri.
Baada tu ya Jackbosi kuondoka Ade alichukua CD na kuweka katika deki, lakini kabla haijaanza kuplay wakinamama wengine wote pamoja na grace walisimama ili kuondoka eneo lile. lakini Ade alikaa pale pale na kabla grace na wakina mama kuondoka kabisa eneolile Cd ilianza kuonyesha, Jackbosi alikuwa amefuatilia kila biashara za baba yake chafu ambazo walikuwa hawazijui na wanazo zijua kisha akachukua video kila mahali ambapo makontena ya baba yake yapo na ulinzi uliokuwepo lakini mwishoni aliweka kipande cha mkutano wa baba yake na james ambao huo ndo ulisababisha yeye kuwatorosha wakinamama na kuchoma hospitali, na walipo angalia waligundua mpango wa james na Mr.kivuli ulikuwa baada ya kikao kile siku inayafuata james aamie pale, kisha usiku wa siku hiyo saa tisa wakati wakinamama wote wamelala yeye atafanya majalibio ya madawa yake kwenye miili yao ili aweze kuona kama madawa hayo yanauwezo wa kumfanya mtu asiache madawa tena maishani anapo dungwa siku ya kwanza tu, na kama yataleta matokeo mazuri watoto wote wata chukulia nakulelewa palepale kwani wakinamama wote hawatajali tena watoto wao zaidi ya madawa na kisha watoto wasingepelekwa tena nchi za nnje bali wangefundishwa kuwa watumiaji na wasambazaji wazuri ambao hawajawahi kutokea nchini. Lakini pia mama zao wangeishia kuwa wajalibishwaji wa madawa hayo maisha yao yote kwani madawa hayo yana nguvu sana unapoanza kutumia huwezi kuacha mpaka unakufa .
lakini pia mpango mwingine ulikuwa kumtoa Jackbosi katika hospitali ile ili asiingilie chochote na ndio maana baba yake alimwambia achukue likizo mama yake amemkumbuka sana.
mwishoni kabisa Jackbosi alionekana akicheka sana na kuwaambia nakuja kuwa grace hivi karibuni, kwasasa grace karibu kuwa Jackbosi mipango ianze ndani ya wiki nnaimani hakutakuwa na Mr.kivuli tena kwani taarifa zake muhimu ndo izooo na peke yako huwezi, peke yangu siwezi ila pamoja tunaweza. byeeeee.
USIKOSE SEHEMU YA 11 $ 12.
MUANDISHI: WINIFRIDA FRANCIS THOBIAS.
SEHEMU: 9 $ 10
WhatsApp no : 0746115688.
Mr.kivuli alishangazwa sana na kitendo cha jasmini kumshika mkono lakini jasmini alipoona Mr.kivuli anaonekana kuwa na hasira japo anajitahidi kufichaficha jasmini aliangua kicheko na kumwambia Mr.kivuli samahani ila ni kwausalama wa mtoto lazima unawe kabla ya kumshika hiyo itasaidia akue bila maambukizi ya aina yeyote. Mr.kivuli alicheka sana na kila mtu aliyekuwa pale pia alicheka na hapohapo Mr.kivuli hasira zilimpotea na kuchukulia kama tabia ya jasmini inatokana na upendo wake kwa mtoto wake, hivyo aliachana na mtoto wa grace nakuwaomba wakinamama wote wapumzike tu, kwani yeye anamizunguko yake ndani ya hospitali . Basi wakinamama walibakia wote hodini lakini grace wakati walinzi wakihangaika na msafara wa Mr.kivuli yeye alitoroka na pikipiki ya kununulia mahitaji muhimu akaelekea kwenye kampuni yake ya usafirishaji ya Graja kwani alipigwa simu na kujulishwa kuna proposal mpya ya kibiashara kutoka katika kampuni ya Culture.
upande wa pili Mr.kivuli alitembea na james hospitali nzima na kisha james alichagua chumba kitakacho mtoshea yeye kufanya mambo yake na baada ya hapo Mr.kivuli alielekea ofisini akiwa yeye, Jackbosi pamoja na james lakini baada ya wote kukaa Mr.kivuli alimuomba Jackbosi akaendelee nashughuli zake za kila siku kwani alikuwa na mazungumzo ya kibinafsi na james. Jackbosi aliondoka lakini kumbe alikuwa ametegesha kamera kwani safari hii hakutaka kuonekana mjinga tena hivyo wakati kikao kinaendelea na yeye aliingia katika chumba ambacho kilikuwa hakina mtu nakuanza kuangalia na kusikiliza kila kilicho kuwa kinaongelewa na Mr.kivuli pamoja na james lakini ghafla wakati Jackbosi anasikiliza maongezi ya Mr.kivuli na james aliweka simu yake mfukoni nakukimbia moja kwa moja katika chumba cha wakina mama bila kugonga hodi aliusukuma mlango na kuwauliza grace yupo wapi, Ade akamwambia kuna kazi muhimu ameenda kuifanya kwenye kampuni , Jackbosi akawaambia hakikisheni wote mnaandaa vitu vyenu vya umuhimu leo usiku mnatoka hapa na hakuna yeyote anapaswa kukataa juu ya jambo hili kisha akamchukua Ade pamoja na mwenzie mmoja nakuwapa kazi ya kufungua tank za pikipiki zote na kuchukua mafuta kisha kuyaweka kwenye makopo aliyo wapa kwani yata wasaidia wakati wa kutoka hapo. baada ya Jackbosi kuwapa maelezo hayo alitoka na kwenda kukaa katika ofisi ya madaktari na muda haukupita mlinzi alimfuata na kumtaarifu kuwa baba yake alikuwa anamuita hivyo Jackbosi alielekea baba yake alipo na baba yake alimtaarifu kuwa kuanzia kesho James atakuja kuanza kazi yake hapa pamoja na wafanyakazi wake. Jackbosi alimwambia baba yake sawa lakini moyoni mwake aliweka kiapo kwamba ikifika kesho hospitali itakuwa imekwisha sahaulika. lakini kwa upande wa james alimwambia kinafki Jackbosi amsamehe kwakumkosea siku ya part kwani kuanzia sasa watakuwa wakionana mara nyingi. Jackbosi alicheka sana na kumwambia usijali tupo pamoja ni jambo dogo sana lililotokea Siku ile mbona mimi nilikusamehe hofu kwako tu. Mr.kuvuli yeye aliona kawaida kwa vijana kuongea maneno kama hayo hivyo alimwambia tu binti yake kafanya jambo zuri kumsamehe mapema james ukizingatia wao James ni mshirika mwenzao kwasasa. baada ya Mr.kivuli kuongea maneno hayo alimwambia James waondoke wakaendelee na majukumu mengine lakini pia akamwambia binti yake chukua likizo kuanzia kesho mama yako amekukumbuka sana . Jackbosi alionekana mwenye furaha sana nakumshukuru baba yake kwa kumpa likizo, lakini Baada tu ya Mr.kivuli kuondoka Jackbosi alijalibu kuwasiliana sana na grace lakini hakukuwa na majibu yeyote kwani grace alikuwa hapokei simu . Lakini kumbe grace nae alisahau kifaachake anachotumia kuwasiliana na watu kwenye droo yake ya mafaili ofisini kwake alipo kuwa akijiandaa kuelekea kwenye kikao kilichokuwa kinafanyika ili kutoa maamuzi kama kampuni yao itashirikiana na Culture company au haitakuwa tayari.
Maamuzi ya grace alikubaliana na kusaini makubaliano hayo lakini kama Mr.kivuli mwenyewe ataonyesha kujali na kuja mwenyewe kusaini makubaliano hayo ofisini kwake lakini kama hatakuwa tayari makubaliano hayata fanyika.
wawakilishi wa kampuni ya Culture waliona kama vile grace anadharau sana lakini grace hakuwa tayari kubadili sharti hilo na aliwapa masaa mawili wawe wamesha wasiliana na bosi wao nakutoa jibu kama bosi wao yuko tayari au la. kisha yeye akarudi ofisini kwake na kuendelea kupitia kazi mbalimbali hasahasa ambazo hazikupitia mikononi mwake .
Wawakilishi wa kampuni ya Culture walikuwa wakimpigia sana mwenyekiti wa kampuni ya Culture ambaye ni Mr.kivuli lakini kwabahati mbaya Mr.kivuli alikuwa ameacha simu yake ndani ya gari hivyo ilikuwa ngumu sana kuwasiliana nae kwa njia ya simu hivyo walikubaliana muwamkilishi mmoja aende kwenye kampuni kwani walikubaliana na Mr.kivuli baada ya makubaliano hayo watakutana nae kwenye ukumbi wa mikutano wa kampuni ya Culture .
Upande wa pili Jackbosi aliendelea na mipango yake ya kuhakikisha ana watorosha wakina mama wote usiku.
Baada ya lisaa limoja grace alirudi katika chumba cha mkutano wa makubaliano na kuwauliza kama wawakilishi wa kampuni ya Culture wamesha wasiliana na bosi wao lakini kwa bahati mbaya hawakuwa na jibu hivyo grace alisimama nakuwaambia makubaliano hayatakuwepo tena muda umeisha , lakini kabla
grace hajatoka nnje ya chumba cha makubaliano simu ya muwakilishi kutoka kampuni ya Culture iliita na muwakilishi huyo aliweka loud speaker kwani bosi wao Mr.kivuli alipiga na moja kwa moja Mr.kivuli alimwambia grace kesho ntakuja mimi mwenyewe kusaini mkataba , grace bila hata ya kuogopa alimwambia Mr.kivuli saa 3:00 asubuhi na usisahau naenda na muda. Mr.kivuli alikubaliana nae japo alipatwa na hasira sana kwani kwenye maisha yake hakuwahi kukutana na mtu wakumdharau , Siku zote watu wamekuwa wakimuheshimu lakini grace hakujali. Baada ya mkutano grace alielekea nyumbani kwao ili kuweza kuangalia hali ya baba yake pamoja na wakinamama wote walio kuwa wanaishi katika nyumba yao , wakati huo Jackbosi nae aliendelea kumtafuta grace mara kwa mara lakini grace hakuwa na kifaa cha mawasiliano.Jackbosi alifanya maamuzi ya kuendelea kupanga mipango yake ya kuwatoa wa kinamama wote hospitalini .
Mida ya saa mbili usiku Jackbosi alimuita mlinzi wake na kumwambia kaangalie wakinamama kama wapo. mlinzi alienda na aliporudi alimpa jibu kuwa wakinamama wote wapo, grace akamwambia chukua kufuli hili kawafungie muda huu utawafungulia asubuhi kisha Jackbosi akampa mlinzi ufunguo moja na yeye akachukua mmoja, mlinzi akaenda kuwafungia wakinamama kisha Jackbosi akamruhusu aende tu nnje kuendelea na shughuli nyingine . Mlinzi alipo tòka tu Jackbosi alielekea kwa wakinamama na kuwatoa wote kisha akaufunga mlango kama alivyo ufunga mlinzi wake na baada ya hapo akawatoa wakinamama wote nnje kupitia njia ya siri na kuwaingiza kwenye gari iliyo kuwa ikiwangojea upande huo. kisha akamchukua ade na mmama mmoja wakasaidiana kumwaga mafuta hospitali nzima na baada ya hapo akawaambia wakimbie na wala wasijali kuhusu yeye kwani atakuwa salama . Baada tu ya wakinamama kuondoka na gari iliyowabeba kutoka maeneo ya hospitalini Jackbosi alitupa njiti ya kibiriti ndani ya hospitali na kisha moto ukaanza Kuwaka walinzi na madaktari wote walikimbia kwani moto ulianza kwa kasi sana lakini Jackbosi yeye alitoka nnje ya geti la hospitalini na kunywa vidonge vilivyo mfanya azimie . Moja kati ya walinzi alimpigia Mr.kivuli na kumpa taarifa juu ya kilicho tokea lakini Mr.kivuli alimuuliza mlinzi huyo kuhusu Jackbosi na hapo ndipo mlinzi alipo mpa taarifa Mr.kivuli ya kuwa sikumuona wakati moto ulivyo anza lakini nakumbuka alikuwepo ndani ya hospitali , anaweza kuwa karibu ya hospitalini tu , kwani sisi tuliondoka kabisa eneo lile tupo njiani kuelekea kwenye kampuni kama ulivyotuambiaga .
mke wa Mr.kivuli aliposikia hayo alishindwa kuendelea kusubiri mipango ya mumewe alichukua gari nakuanza safari ya kuelekea hospitalini kumfuata binti yake wakati alipokuwa akiendelea kutafuta alipofika eneo la hospitalini alimuona Jackbosi akiwa amezimia na haraka alimchukua mwanae na kumkimbiza hospitalini kwani hakuwa amesaidika ukizingatia hospitali ilikuwa nnje kabisa ya Mji hakukuwa na watu wakuwasaidia baada ya janga hilo kuwakuta .
walipofika hospitalini Daktari alimwambia Mrs.kivuli binti yako yuko sawa japo anahitaji muda wa kupumzika kwani anaonekana amevuta hewa chafu ya kutosha atakuwa sawa anahitaji kupumzika tu.
wakati grace alipokuwa anataka kurudi hospitalini ghafla aliona kosta ikisimama nnje ya nyumba yake na alipofika nnje ili ajue nini kinaendelea alishangaa kuona ni wakinamama wote wamerudi, grace aliogopa sana na alipo jalibu kushika kifaa chake cha mawasiliano masikioni ili awasiliane na Jackbosi aligundua kifaa hicho hakipo na hapo ndo ilimbidi awe mpole na kuwasaidia wakinamama wengine kushuka kwenye gari hasahasa wale waliozaa kwa upasuaji.
kisha wote grace akawapa vyumba na baada ya hapo akamchukua mtoto wake pamoja na jasmini akawaingiza kwenye chumba chake kisha akawaambia wakinamama wote wapumzike tu watapewa kila wanacho kihitaji na asubuhi wataongea mambo mengi zaidi .
grace aliingia kwa jasmini akamuuliza ' imekuwaje' ?. lakini jasmini alimwambia ghafla Jackbosi alikuja akikutafuta mno naalipo ona hupatikani alituambia tujiandae anatutoa pale hospitalini leo na hospitali nayo mwisho wake ni leo tulihisi kama utani lakini kweli ilipofika saambili Jackbosi alikuja na kututoa wote kisha akawasha jengo la hospitali moto na nahisi mpaka sasa jengo la hospitali litakuwa limesha teketea kabisa.
grace hakuamini anachoambiwa hivyo alichukua pikipiki nakwenda kuhakikisha alichoambiwa ni kweli au kuna uongo ndani yake, lakini alipo fika eneo la hospitalini alikutana na majivu tu, grace alichukia sana na kuchukulia maamuzi ya Jackbosi ni ya kipumbavu sana na kuanzia hapo hakutaka kuwasiliana nae na akaamua kupanga mipango yake ya kumteketeza Mr.kivuli kwa muda wa mwezi .
wiki moja baadae Jackbosi alienda kumtembelea grace kwani alikuwa hampati kwenye simu lakini alipoingia ndani grace na Wakinamama wote walionekana kumchukia sana kwani waliisi yeye amewatoa pale ili wasimmalize baba yake hivyo kila alivyojalibu kuwaonyesha upendo wao walirejesha maneno ya chuki. Jackbosi alipoona amna mwenye furaha na yeye aliamua kuondoka lakini aliacha CD akawaambia kama wakipenda wanaweza kuangalia ni nzuri.
Baada tu ya Jackbosi kuondoka Ade alichukua CD na kuweka katika deki, lakini kabla haijaanza kuplay wakinamama wengine wote pamoja na grace walisimama ili kuondoka eneo lile. lakini Ade alikaa pale pale na kabla grace na wakina mama kuondoka kabisa eneolile Cd ilianza kuonyesha, Jackbosi alikuwa amefuatilia kila biashara za baba yake chafu ambazo walikuwa hawazijui na wanazo zijua kisha akachukua video kila mahali ambapo makontena ya baba yake yapo na ulinzi uliokuwepo lakini mwishoni aliweka kipande cha mkutano wa baba yake na james ambao huo ndo ulisababisha yeye kuwatorosha wakinamama na kuchoma hospitali, na walipo angalia waligundua mpango wa james na Mr.kivuli ulikuwa baada ya kikao kile siku inayafuata james aamie pale, kisha usiku wa siku hiyo saa tisa wakati wakinamama wote wamelala yeye atafanya majalibio ya madawa yake kwenye miili yao ili aweze kuona kama madawa hayo yanauwezo wa kumfanya mtu asiache madawa tena maishani anapo dungwa siku ya kwanza tu, na kama yataleta matokeo mazuri watoto wote wata chukulia nakulelewa palepale kwani wakinamama wote hawatajali tena watoto wao zaidi ya madawa na kisha watoto wasingepelekwa tena nchi za nnje bali wangefundishwa kuwa watumiaji na wasambazaji wazuri ambao hawajawahi kutokea nchini. Lakini pia mama zao wangeishia kuwa wajalibishwaji wa madawa hayo maisha yao yote kwani madawa hayo yana nguvu sana unapoanza kutumia huwezi kuacha mpaka unakufa .
lakini pia mpango mwingine ulikuwa kumtoa Jackbosi katika hospitali ile ili asiingilie chochote na ndio maana baba yake alimwambia achukue likizo mama yake amemkumbuka sana.
mwishoni kabisa Jackbosi alionekana akicheka sana na kuwaambia nakuja kuwa grace hivi karibuni, kwasasa grace karibu kuwa Jackbosi mipango ianze ndani ya wiki nnaimani hakutakuwa na Mr.kivuli tena kwani taarifa zake muhimu ndo izooo na peke yako huwezi, peke yangu siwezi ila pamoja tunaweza. byeeeee.
USIKOSE SEHEMU YA 11 $ 12.