Elections 2010 Tamko rasmi la Dr. Slaa kuhusu CCM kustisha midahalo TBC

Kaka tuna-tatizo la kimfumo... lakini kwa bahati mbaya sana tunadhani tunaweza kutibu ukimwi,,, kwa kutibu magonjwa nyemelezi... Mdahalo ni mzuri sana kwa jamii inayoelewa mdahalo ni nini? Sio hii ya kwetu mkuu... well!! Ni muhimu sana uelewi simtetei Kikwete kwenye hili la mdahalo maana anatakiwa asimame mwenyewe kwa kuwa urais anataka yeye... najua anakwepa kwa sababu ni mdhaifu upande huo... tena sana, maana hata pale anapoongea mwenyewe unaona kabisa si mjuzi wa kupangilia hoja zake....
Lakini ukweli unabaki pale pale... mdahalo mzuri but not the only choosing criteria.

Mimi Mtanzania Huru Bwana... na Huenda nisiwe mwanachama wa chama chochote Daima... kwa mfano... chama kinachoamini cheo cha makamu wa Rais ambacho kimetajwa kwenye katiba ni cheo cha mchezo siwezi kuchukua kadi yao of course. CCM pia sijadhirika nayo ndio maana sina hata chembe ya documents zao ... only msomaji mzuri wa ilani za vyama.

Interestingly nchi haiendeshwi kwa matakwa ya mtu binafsi, nchi inaendeshwa kwa kufuata sheria. Therefore sioni kitakachomshinda mtu mwenye akili timamu kuiongoza nchi.

Kasheshe kwa bahati mbaya hatutafuata standards zako katika hili tunaongozwa na the letter of the constitution.

Hebu niambie ni kipi ambacho Dr. Shein alikuwa anakifanya katika position ya umakamu wa rais ambacho mtu kama mgombea mwenza wa CHADEMA hawezi kukifanya.
 
Kwani Ndoa inahusianaje..je na nuke mkiulizwa main unaanguka anguka jukwaani utajibu Ccm ban a yaani mawazo yenu ya kizamani sana
Siku hizi hawa jamaa hata JF members wametekwa na mawazo ya Makamba regardless ya hoja iliyoletwa say ya mdahalo au barabara wao wataingiza ndoa ya Slaa, it means is the only left weapon waliyoitegemea labda itawasaidia lakini mwisho hata wenyewe wanaona inawaboa sasa.
 
Hapo kwenye red ni kwa ccm tu au na chadema,
kama ni uoga, basi uoga alikuwa nao mbowe akatumia ubabe kumzuia zito asigombee uenyekiti chadema
Watu kama wewe ndio ambao hawawezi kushiriki midahalo. Mada inazungumzia jambo hili wewe unajadili jambo lile, Wenye kusikiliza watakutambua tuu kuwa ukoje
 
Mtu wa pwani, it is simple... assume ww ni mgombea wa CCM, ambaye hata sio mbunge wa kipindi kilichopita (Incumbent MP); kawaida kwenye mdahalo you need to be in the same level... thus huwezi kuambiwa hujaleta maji wakati haukuwa mbunge... hope you get it... Leo hii tunamhukumu Kikwete kwenye kura za Urais kwa kuwa alikuwepo 5 years ago... and he needs to defend kwa nini alishindwa x, y, z... the other thing is ... Mdahalo needs not to zomea au etc... angalia kipindi cha Adam Simbeye... TBC1 hoja tupu hakuna makofi au kuzomea etc...

Hoja kama hizi zinanikumbusha upuuzi mmoja unaitwa tume huru... na definition ya kwamba tume huru ni ile yenye composition ya representation ya vyama... to me tume huru ni ile yenye wataalamu tupu and we don't need to know unatoka chama gani.

So I could have been happy TBC1 waandae vipindi vyao,,, maswali yaulizwe but hakuna haja ya kuwa kama vile kuna representation ya vyama kwa wale walioko benchi.. i think they don't even needs to put on their party uniforms.

Acha hizo ni upuuzi tu.. kwani kwenye midahalo ile CCM wanakuwa wamefungwa kamba? wamezuiwa kuleta watu wao, wamezuiwa kuzomea?? kwani ni CCM tu wanaozomewa.... kuzomewa\ kwa mtu ni kutokana na kuchemka kwake..... hamna cha kuongea ndo maana mnakimbia....na bado....
 
Kama ingelikuwa uwezo wa kukariri ngonjera na kutapika mbele za watu kwa staili ya mdahalo ndio kigezo cha kuwa kiongozi wa watu basi kiongozi wa kwanza angekuwa Shehe Mtopea, Rev. Mtikila n.k Ila Uongozi una vigezo vingi kama vile uadilifu, ukweli, elimu, kukubalika na watu , mapenzi yako kwa watu. JEE TUKIANDAA MDAHALO SUALA LAKO LA NDOA LIKIULIZWA UTALIJIBU!!!!! . Tusubiri Oktoba 31 ndio siku ya mdahalo mzuri.
Hahahahahaaaaaa, majibu yote atakuwanayo tena ya mojakwamoja, Je' wakimuuliza huyo bwana wa kijani watoto wake wa ziada mama zao wako wapi ataweza kujibu? Mafisadi ataweza kuwaelezea, Kiwira, EPA ..................... ataweza????
 
analysis inaonyesha wagombea wa upinzani wanafanya vizuri hasa wa Chadema kwene midahalo huku wale wa CCM wakifunikwa ile mbaya.
 
dsbanner.jpg


Mgombea wa urais wa chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Dr. Wilibrod Slaa amesema; Uamuzi wa CCM kukataza wagombea wake kushiriki midahalo ya kisiasa ni aibu kwa mwelekeo wa demokrasia nchini. Kiongozi anayetaka nafasi ya kisiasa anayekwepa nafasi ya kuzungumza na wananchi anaotaka kuwaongoza na anataka kuwahubiria tu ni mwoga na hafai kuwa kiongozi wao. Chadema tuko tayari wakati wowote na mahali popote kujadiliana na mtu yeyote wa chama chochote.

My take: Kwanini uogope kukutana na wananchi unaowaomba kura?

Dr. Wilbrod Slaa 2010
...kwa kukataa mdahalo ambao vyombo vya habari vinaona ni fursa nzr kwa wagombea kuwasiliana na wapiga kura wakiwa pamoja, napendekeza vyombo vya habari makini wasusie kufanya coverage za ccm zinazohusu uchaguzi!!!!
 
Kama ingelikuwa uwezo wa kukariri ngonjera na kutapika mbele za watu kwa staili ya mdahalo ndio kigezo cha kuwa kiongozi wa watu basi kiongozi wa kwanza angekuwa Shehe Mtopea, Rev. Mtikila n.k Ila Uongozi una vigezo vingi kama vile uadilifu, ukweli, elimu, kukubalika na watu , mapenzi yako kwa watu. JEE TUKIANDAA MDAHALO SUALA LAKO LA NDOA LIKIULIZWA UTALIJIBU!!!!! . Tusubiri Oktoba 31 ndio siku ya mdahalo mzuri.

Hizi ndizo stupid comments ambazo hatutaki kwenye forum hii....hivi wewe unaona mambo ya nyumbani kwa mtu ni muhimu kuliko mustakabali wa nchi yetu? Kweli wewe umefilisika kimawazo....nashangaa unaweza hata kufungua tuvoti hii....elimu yako ni mpaka darasa la ngapi?....because you have no comment worth reading....bankrupt brain with bankrupt ideas..
 
...Ukiona mtu anajaribu kuficha wasihi wake basi ujue liko kjambo.. na ukiona mtu ajiamini na uelewa wake ujue kuna jambo nyeti na zito liliojificha ndani ya nafsi yake au nafsini mwao na si lingine zaidi ya UKIHIYO an kufoji vyeti ... Tunao wengi sana hao watu hasa kwa upande wa hao wanaopenda vya kuchomoa vyao Mapema...Always wanaishia kwenye kupewa digrii ambazo hazina jasho tangu lini ukasimsikia Baraka Obama akitwa Mheshimiwa Docta Baraka Obama???? ila ukiwa na elimu ya kuungishwa utasikia yote hayo. Hata siku moja mtu aliyekesha na kuweka miguu ndani ya ndoo ya maji au kupambazua (Kusoma usiku Kucha) akakwepa mdahalo....???.Mtui kama huyo anakuwa fit muda wote ana anajiamni si kasoma na nyanga zipo kichwani bwana kwa sababu alijiamni tangu anasoma . na bado sana watakimbia mpaka majukwaanim wa pale wanacnhio waliochoshwa na maovu yao watakaploawafuata huko huko na maswali ya kina siju watawajibu nin i hawa waliozoelwaka kuitwa wadanyaika lakini sasa wamevumbuka macho....
 
Kasheshe,
Mkuu wangu umenisikitisha sana ku undermine Mdahalo kiasi kwamba unasema ati - Mdahalo mzuri but not the only choosing criteria. Hakika sidhani kama unayo critea yoyote ile unayoweza kutupa ktk kumchagua mbunge..Kifupi nitarudia tena kutokuwepo na mjadala ni sawa na kumwajiri mtu pasipo interview ukitumia hizo criteria za CV za kutundika Ukutani ambazo ndizo zimetufikisha hapa tulipo.

Kwa mfano:- Wakazi wengi wa Kinondoni walimchagua Zungu wasijue kabisa Zungu ni nani,wengine hata hawajawahi kumtia machoni zaidi ya kuona mabango ya picha yake. Pia wapo wengi wanaomjiua Zungu kwa uchafu wake kiasi kwamba ingekuwa nafasi yao kumuuliza maswali magumu kuhusu yeye binafsi na pia ahadi alowapa miaka mitano ilopita. wakinyimwa nafasi hii, matokeo yake wataendelea kumchagua kwa sura na umaarufu wake.

Hili sio swala la CCM, Chadema wala CUF ni swala la haki ya wananchi kupewa uwezo wa kuwachagua viongozi wao kwa kupitia taratibu zenye kuwawezesha kuchagua viongozi bora. Na wala mimi sijali kabisa kama CCM wanakwepa JK asiweze kusimama na Dr.Slaa isipokuwa maamuzi ya chama kimoja yanaondoa kabisa utaratibu utakao wawezesha kumchagua kiongozi bora.

Kama Chadema wamemsimamisha huyo Mgombea darasa la saba kuwa makamu wa Rais ni vizuri sana tukipewa nafasi na kumhoji mtu huyu. Fare kwake na kwetu sote, kwani kasoro moja au mbili haziwezi kuondoa sifa nyingi na kubwa ambazo mgombea anaweza kuwa amezibeba na ndio maana amewakilishwa kwetu. Mimi na wewe hatuzifahamu na wala hatutaweza kuzifahamu kama sipopata nafasi ya kuuliza iomekuwaje mtu huyu wa darasa la sababa asimame kkama mgombea mwenza wa kiti cha rais...kwa sifa gani....

Hata huyo Bilal anazo kasoro nyingi sana kiasi kwamba unaweza sema afadhali kuongozwa na zezeta, lakini yote haya hatuwezi fikia maamuzi ya uwezo wa Bilal na kasoro zake kama hatutaweza kumpa nafasi ya kujiuza kwetu na pia wananchi wenyewe kumpima kwa yale wanayoyataka wao na sii kutumia hizo sifa za chama CCM.

Nitakwambia tena mkuu wangu hakuna njia bora ya kuchagua Wabunge zaidi ya kuwepo na midahalo kwa sababu mara nyingi sana hotuba za vyama huhudhuliwa na wanachama wake na watoto wa shule kuliko wananchi wote wapiga kura..Sii rahisi kwa mfanyakazi na mwanachama wa Chadema kwenda mkutano wa CCM wakati wa kazi ama aache biashara zake..Lakini ni rahisi kwa Watanzania wapiga kura wengi kukaa majumbani mwao kutazama mdahalo wa wagombea wao ambao utatayarishwa na wahusika baada ya kukusanya hoja muhimu za wanajimbo. Ni makosa makubwa kumwajiri mtu pasipo kumfaniyia Interview ambayo mara zote ni mwajiri anayepanga maswali kutokana na sifa au ujuzi unaotakiwa toka kwa mwajiriwa.
 
Of course nilikuwa shocked sana kusikia katika redio kwamba Makamba kawazuia wagombea wa sisiemu kushiiki mijadala na midahalo katika TV baada ya DC Ng'humbi kuchemsha katika kujibu maswali ya 'wenye nchi'. Kama sisiemu wanajua haana majibu kwa maswali ya wananchi, ni nani ana majibu basi? Makamba aache hizo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom