Tamko la Vijana 'WASOMI' wa vyuo vikuu Mkoa wa Dodoma Dhidi ya wabunge wa CHADEMA

Nina mdogo wangu hapo chuoni na amesema mbona hawajashirikishwa kuandaa msimamo wa chuo? Hivi huu ni msimamo wa nani?...........lakini la msingi kama hawa kweli ni wasomi hapo chuoni wamekwenda kufanya nini?.............................nijuavyo wasomi wapo makazini wanatatua matatizo ya jamii ...............aliyeko chuoni anautafuta usomi kwa hiyo hana ubavu wa kujiita msomi................hususani pale hata wale anaodai kuwawakilisha hata hataki kuwashirikisha kwenye maamuzi nyeti kama haya..................

Youre Right, wasomi wako makazini na mitaani siku hizi, hao ni watoto wa form Six wanatafuta vyeti. Nenda mtaani utawakuya graduates kibao, watu wenye master ndio usisema wasomi
 
wamekusanyikwa wachache then wanasema tamko la vijana wa elimu ya juu..................

si hwa nd walinyimwa haki ya kupiga kura?

leo wanakuja na tamko?!!1


they cant think beyond the next meal!!
 
Leo ndiyo nimeamini kuwa humu JF kuna vilaza na mbumbumbu wakubwa. Hiyo taarifa ya vijana inajieleza na iko wazi kabisa. Oneni aibu na muwashauri wabunge wa Chadema. Soon or later they will go out of sight mirror completely


Hongera kwa kuwafumbua macho vilaza wanojiita wasomi humu JF kwa kutokujadili na kutoa shutuma bila tafakuri za kina juu ya tamko hilo.

MSOMI ni mtu mwenye kuvutiwa na fikra na mwenye mbinu za kizisarifu na kuzitumia vilivyo(fikra hizo) baadhi au zote. Profesa Ali Mazurui.
 
Hao ni wasomi wa wapi kikundi fulani cha mafisadi, tutatoana roho wasiwatanie watanzania.

Msomi gani unaunga mkono sheria inavunjwa, Usomi si kuunga mkono ufisadi.

Hao ni wale watoto wa mafisadi kama kweli wanauchungu na nchi hii, embu waorodheshe majina yao tuwafahamu, maana isijekuwa wale Mkada wanaonunuliwa na CCM kwa 5000 na kupewa kadi halafu unasema usomi.

Mbona hawakutoa tamko wakati ule NEC imewazuia kupiga kura, hao ni kikundi cha wezi tu, wale ambao wanajiita UVCCM.

Hata mtoe tamko maana aliitoa Shimbo bado watu wakawa na msimamo ndio hiyo inayotoleawa na wapumbavu.

WaTZ na Wana Chadema tusonge mbele najua CCM na mafisadi wanakereka na mambo mnayofanya lakini sisi wananchi tunaiamini sana Chadema na viongozi wake.


PEOPLES POWER
 
.....kamwe mtoto hawezi kudai kuwa hamtabui Baba yake kisha anaendelea kumwita Baba na kutumia kila kitu kinachotolewa na Baba huyo huyo.............

Typical SISIEMU..........! Masikini watoto hawa, hata hawajuia abcs za haya wanayoyasema........!
 
Hawa wamesoma shule za CCM za kata. Wasomi halisi wangedai Katiba mpya na Tume huru ya Uchaguzi. Waulize akina Samwel sitta waliosoma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam enzi hizo walivyokuwa Revolutionary kwenye kiwanja cha Revolutionary Square! Wanaojiita wasomi hawana ubavu wakuhoji rushwa na ufisadi ndani ya serikali.
 
Leo ndiyo nimeamini kuwa humu JF kuna vilaza na mbumbumbu wakubwa. Hiyo taarifa ya vijana inajieleza na iko wazi kabisa. Oneni aibu na muwashauri wabunge wa Chadema. Soon or later they will go out of sight mirror completely


Hongera kwa kuwafumbua macho vilaza wanojiita wasomi humu JF kwa kutokujadili na kutoa shutuma bila tafakuri za kina juu ya tamko hilo.

MSOMI ni mtu mwenye kuvutiwa na fikra na mwenye mbinu za kizisarifu na kuzitumia vilivyo(fikra hizo) baadhi au zote. Profesa Ali Mazurui.

wapuuzi wakubwa ninyi!!

mnazan jf ni kijiweni? mtaburuzwa hadi dk ya mwisho.....chambeni mkalale wehu wakubwa ninyi
 
Hao ni wasomi CCM na wanawakilisha CCM, ngoja tusubiri tamko la wasomi Chadema

Naomba niwasahihishe, hawa sio wanafunzi wa vyuo vikuu Dom, bali ni kijikundi cha wahuni wa CCM waliopewa vijihela vya kumalizia siku wanakuja kuchafua hali ya hewa tu

Kwanza kwa CHADEMA kujibu waraka mwepesi wa watoto kama hawa hakuna maana yeyote. Ukilumbana n amjinga we ndo utaonekana mjinga. Hawa saizi yetu wala sio saizi ya uongozi wetu CHADEMA. Msipoteze Muda Dr. Kujadili hayo, tuachieni tuyafundishe adabu haya matoto

Tena nangoja keshokutwa yalilie kucheleweshewa au kutopewa mikopo!!!!
 
Waraka huu umesomwa muda si mrefu mbele ya vyombo vya habari zaidi ya 15 huko Dodoma.

TAMKO LA VIJANA WASOMI WA VYUO VIKUU WA MKOA WA DODOMA, KUHUSU KITENDO CHA BAADHI YA WABUNGE WA CHADEMA KUTOKA NJE YA UKUMBI WA BUNGE.

NDUGU WAANDISHI WA HABARI,
NDUGU WANANCHI,.


Awali ya yote nawashukuru sana kuhitikia wito wetu wa gfafla kuja kujumika pamoja nasi leo hii, akhsanteni sana.

Sisi vijana wasomi wa vyuo vikuu mbalimbali vilivyoko mkoa wa Dodoma kwa pamoja tunapenda kuweka wazi maoni yetu juu ya kitendo kilichofanywa na Wabunge wa CHADEMA jana 18.11.2010 wakati Mhe. Rais alihutubia Bunge.


Kwanza tumeshtushwa na kitendo hicho na kuweka wazi masikitiko yetu kwa kuwa kilichofanyika ni kinyume na matarajio ya wapiga kura waliowachagua waheshimiwa wabunge hao kuwawakilisha ndani ya chombo hicho kikubwa na chenye heshima kubwa ndani na nje ya nchi.


Bunge ni sehemu ya kuwakilisha wananchi kwa hoja chini ya kanuni zilizopo bila kujali itikadi ya chama chochote cha siasa na kazi kubwa ya mbunge ni kuishauri na kuisimamia Serikali kwa niaba ya wananchi waliomchagua au kuwachagua.


Kwa mantiki hiyo basi kama Wabunge hawamtambui Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania maana yake hawana kazi ya kufanya ndani ya Bunge kwani kazi yao kubwa ni kuishauri na kuisimania Serikali sasa kama hawaitambui Serikali hiyo hawana sababu ya kuendelea kuwepo Bungeni.


Pili Baada ya uchaguzi wa Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda, wabunge hao pia walinukuliwa na vyombo vya habari na ushaidi tunao wakiweka wazi kumkubali kiongozi huyo, na kauli mbiu yake ya ‘Bunge moja’ je, kitendo walichofanya inaashiria utekelezaji wa kauli mbiu ya Bunge moja?


Tatu msimamo wa kutomtambua Rais ni wa CHADEMA kama chama na waliotoka nje ya Bunge ni wabunge sasa ni vema wabune hao watambue na kutafakari upya kama kweli wanawawakilisha Bungeni wananchi au cha na kutekeleza misimamo yao bila kujali maslahi ya waliowachagua na kumpa kura nyingi Rais Kikwete?.


Nne Kwa badhi ya wabunge wa CHADEMA kutomtambua Rais wakati akilihutubia bunge ni wazi kuwa hata sheria zitakzopitishwa na Bunge hawatahusika kwa kuwa mwenye mamlaka ya mwisho kukubali sheria iliyotungwa na Bunge itumike ni Rais ambaye wanadai hawamtutambui.


Ni dhahiri kuwa watashindwa kufanya kazi yao ya uwakilishi na usimamizi wa Serikali Bungeni .


Je wanawaonesha watanzania dalili gani kama si kutaka kuleta machafuko nchini na mgawanyiko ndani ya Bunge na kwa Jamii kwa ujumla?.


Wananchi waliowachagua wabunge hao wanapaswa kutafakari upya wawakilishi waliowachagua kama wana uelewa wa kutosha kuhusu bunge, sisi vijana wa vyuo vikuu tunajua na tunatambua kuwa Rais ni Sehemu ya Bunge na Bunge haliwezi kukamilika bila Rais na hii ndio maana kila sheria inayopitishwa na Bunge ni lazima yeye Rais aweke sahihi yake.


Katika mazungumo yake na waandishi wa habari wiki hii Mweneykiti wa CHADEMA MHE. Freeman Mbowe, alinukuliwa na vyombo vya habari akisema wabunge wake na madiwani wanaweza kuendelea kuwakilisha wananchi licha ya kutomtambua Rais.


Sisi tunasema hili si sahihi bali ni upotoshaji mkubwa, kamwe mtoto hawezi kudai kuwa hamtabui Baba yake kisha anaendelea kumwita Baba na kutumia kila kitu kinachotolewa na Baba huyo huyo. Huo ni utovu wa nidhamu au kukosa maadili.


Sisi vijana wa vyuo vikuu Mkoa wa Dodoma tunawaomba Watanzania wote wenye nia njema na Taifa letu kuwapuuza wabunge wa CHADEMA na kutambua kuwa lengo lao ni kutaka kutuhamisha kutoka kwenye ajenda ya msingi ya Maendeleo na kubaki kwenye malumbano ya kisiasa kama tulivyoshuhudia katika nchi jirani.


Kamwe tusikubali kudanganywa na watu wachache.


Mwisho tungependa kuwaomba Wabunge wa CHADEMA wawaombe radhi watanzania kwa kuvuruga tashwira safi ya Bunge letu lisilo na ubaguzi na itikadi za kisiasa vinginevyo wanawadharau watanzania waliowachagua wakidhani kwamba niwaadilifu wa Taifa na si cha chama chao.


Tutambue kuwa kazi kubwa ya CHADEMA na Wabunge wake kwa sasa ni kuwachanganya watanzania ili badala ya kuendelea na shughuli za ujenzi wa taifa wabaki na malumbano ya hapa na pale kwa manufaa yao binafsi.


Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Bunge letu na kutuepusha na ubaguzi kama huu uliofanywa na baadhi ya Wabunge wa CHADEMA.


Aksanteni sana.


IMESOMWA NA THOBIAS MWESIGA RICHARD

KWA NIABA YA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOMA

Time will tell
 
imewauma kwa kuwa bunge lipo karibu nao , waambiwe kuwa kukaa karibu na mahakama sio kujua sheria, imewauma kwa kuwa mtu wao wa karibu kahaibishwa mbele ya umma na umoja wa Mataifa, siku za usoni mnakumbuka kuwa walijitoa kuwa wanamsapoti kikwete wakiwa wamevaa mavazi ya kila aina ya CCM hivyo hatuwashangai kwa kuwa wote bado wanajifunza, cha maana wajifunze kudai haki kama chadema sio wao wanashindwa kudai haki yao ya msingi ya kudai Elimu bure kwa wote, wanasahau kuwa sera za chadema ndizo zinazokubalika hivyo CCM wanajiandaa kuitumia baada ya kubaini inafaa sana, walie tu hao wanoandikiwa madudu
 
nyinyi wana chadema jf branch mbona mnakosa ustaarabu wasomi si wametoa mtazamo wao!!!!
wapeni uhuru wa kuongea kama kuna wana chadema udom branch na wao si waseme ya kwao!
mnapenda kulazimisha kila kitu!!!

msomi akiwa chadema akiwa ccm si msomi...........! msomi aisifuye chadema aikosoaye si msomi.....! kama mchangia mada mmoja alivyosema... twasubiri wasomi wa chama cha migomo nao watoe tamko...!

Mnasikitisha mpaka mnatia kinyaa. Hivi ninyi ni magraduate wa hicho chuo cha Dodoma nini!! Tatizo wanafunzi wa Dodoma wapo pale kulipa fadhira kwa JK. Inaelekea bila yeye chuo wasingekiona na wengineo wangekuwa wanakunywa gongo vijijini!!
 
Hao ni wasomi wa wapi kikundi fulani cha mafisadi, tutatoana roho wasiwatanie watanzania.

Msomi gani unaunga mkono sheria inavunjwa, Usomi si kuunga mkono ufisadi.

Hao ni wale watoto wa mafisadi kama kweli wanauchungu na nchi hii, embu waorodheshe majina yao tuwafahamu, maana isijekuwa wale Mkada wanaonunuliwa na CCM kwa 5000 na kupewa kadi halafu unasema usomi.

Mbona hawakutoa tamko wakati ule NEC imewazuia kupiga kura, hao ni kikundi cha wezi tu, wale ambao wanajiita UVCCM.

Hata mtoe tamko maana aliitoa Shimbo bado watu wakawa na msimamo ndio hiyo inayotoleawa na wapumbavu.

WaTZ na Wana Chadema tusonge mbele najua CCM na mafisadi wanakereka na mambo mnayofanya lakini sisi wananchi tunaiamini sana Chadema na viongozi wake.


PEOPLES POWER

...Mkuu hapo kwenye highlight umegonga ikulu!

Hawa watoto wamepata wapi nguvu ya kutoa tamko wakati wao wenyewe walinyimwa haki yao ya msingi ya kupiga kura? Mimi nilitegemea kwamba wao kama kweli ni wazalendo wangetoa tamko la kutomtambua JK pia kwa sababu hawakupewa na nafasi stahili ya kumchagua........! Sasa nashangaa, leo kura wapige wengine, wao wamenyimwa haki, leo wanakuja kutoa kitamko juu ya rais ambaye hata wao hawakupata nafasi ya kumpa kura, kama wanampenda kweli......! shame!
 
:angry: Wana JF;

TAMKO lililotolewa hivi punde na wanaojiita "wasomi" wa vyuo mabalimbali pale Dodoma limenisikitisha sana. Ingawa naamini kwamba "wametumwa" na WACHAKACHUZI kupeleka ujumbe huo bado statement yao imedhihirisha kitu kimoja; SERIKALI YA CHAMA CHA MAPINDUZI IMEUA ELIMU NA MATOKEO YAKE HATA VYUO VIKUU VIMESHINDWA KUWA NA WANAFUNZI WENYE KUWEZA KUFANYA UPEMBUZI YAKINIFU WA MASUALA YANAYOIZUNGUKA JAMII!!

Miaka michache nyuma vyuo vikuu ilikuwa ni sehemu mojawapo ya kuikosoa serikali inapofanya madudu; leo hii tunaonda vijana walioshindwa kutoa tamko la kukemea maovi yaliyofanywa naserikali ya wakati wa uchaguzi (hata pale wenzao waliponyimwa haki ya kupiga kura ili CCM ipate ushindi katika majimbo kadhaa) bado leo wanaitisha mkutano na waandishi wa habar eti KUIKEMEA CHADEMA!!

Nimejaribu kujibu baadhi ya hoja zao, ningependa tuendeleze hoja hii kwa kuwaelimisha vijana wetu hawa wasioelewa wapi serikali ya CCM inatupeleka!

Naomba kuwakilisha kama ilivyotolewa mwanzoni (hoja zangu nimeziweka kwenye mabano, in blue colour/bold letters)
Awali ya yote nawashukuru sana kuhitikia wito wetu wa gfafla (ghafla ) kuja kujumika pamoja nasi leo hii, akhsanteni sana.

Sisi vijana wasomi wa vyuo vikuu mbalimbali vilivyoko mkoa wa Dodoma kwa pamoja tunapenda kuweka wazi maoni yetu juu ya kitendo kilichofanywa na Wabunge wa CHADEMA jana 18.11.2010 wakati Mhe. Rais alihutubia Bunge.

Kwanza tumeshtushwa na kitendo hicho na kuweka wazi masikitiko yetu kwa kuwa kilichofanyika ni kinyume na matarajio ya wapiga kura waliowachagua waheshimiwa wabunge hao kuwawakilisha ndani ya chombo hicho kikubwa na chenye heshima kubwa ndani na nje ya nchi.
(Kwani hawa watoto wao wametumwa na wapiga kura wa wabunge wa Chadema? Wametoka katika majimbo waliyotoka hawa wabunge hadi wazungumzie matarajio ya wapiga kura wao?)
Bunge ni sehemu ya kuwakilisha wananchi kwa hoja chini ya kanuni zilizopo bila kujali itikadi ya chama chochote cha siasa na kazi kubwa ya mbunge ni kuishauri na kuisimamia Serikali kwa niaba ya wananchi waliomchagua au kuwachagua.

Kwa mantiki hiyo basi kama Wabunge hawamtambui Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania maana yake hawana kazi ya kufanya ndani ya Bunge kwani kazi yao kubwa ni kuishauri na kuisimania Serikali sasa kama hawaitambui Serikali hiyo hawana sababu ya kuendelea kuwepo Bungeni 9Je ni kifungu kipi cha katiba au kanuni za kudumu za bunge kinazongumzia hili?
(Kama hawa watoto wanafahamu/wanajiita wasomi walipaswa kuchambua hoja with data; wangefanya utafiti kuipitia katiba na kanuni za kudumu za bunge maana hizo ndiyo zinatoa muongozo!! Hoja bila vielelezo inaonyesha mapungufu makubwa ya hawa "wasomi")
Pili Baada ya uchaguzi wa Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda, wabunge hao pia walinukuliwa na vyombo vya habari na ushaidi tunao
(kwa nini hawajauwasilisha kwa wanahabari?)
wakiweka wazi kumkubali kiongozi huyo, na kauli mbiu yake ya ‘Bunge moja' je, kitendo walichofanya inaashiria utekelezaji wa kauli mbiu ya Bunge moja?
(Hii kauli mbiuu si ya Chadema, ni ya CCM, hawa ni wabunge wa Chadema, mnapaswa kulitambua hilo)

Tatu msimamo wa kutomtambua Rais ni wa CHADEMA kama chama na waliotoka nje ya Bunge ni wabunge sasa ni vema wabune (wabunge?) hao watambue na kutafakari upya kama kweli wanawawakilisha Bungeni wananchi au cha na kutekeleza misimamo yao bila kujali maslahi ya waliowachagua na kumpa kura nyingi Rais Kikwete?.
(Wasomi feki kumbukeni kwamba hoja ya Chadema ni kwamba kura zilizompa ushindi rais wenu ZILICHAKACHULIWA!! Hiyo ndiyo sababu kuu ya kutomkubali, ukweli ni kwamba hakuchaguliwa kwa kura nyingi kama mnavyodai/mlivyotumwa kueleza)
Nne Kwa badhi (baadhi?) ya wabunge wa CHADEMA kutomtambua Rais wakati akilihutubia bunge ni wazi kuwa hata sheria zitakzopitishwa na Bunge hawatahusika kwa kuwa mwenye mamlaka ya mwisho kukubali sheria iliyotungwa na Bunge itumike ni Rais ambaye wanadai hawamtutambui.

Ni dhahiri kuwa watashindwa kufanya kazi yao ya uwakilishi na usimamizi wa Serikali Bungeni .
(Bunge halina kazi moja tu ya kupitisha sheria, wabunge wa Chadema bado wana kazi nyingi bungeni na nje ya bunge! Mbunge si mtu wa kuhudhuria vikao Dodoma tu na kupitisha sheria kama mnavyodhani)
Je wanawaonesha watanzania dalili gani kama si kutaka kuleta machafuko nchini na mgawanyiko ndani ya Bunge na kwa Jamii kwa ujumla?.
( Kususia hotuba ya Rais kuna uhusiano gain na machafuko? Je, wizi wa kura na KUCHAKACHUA MATOKEO mmeona hakuhusiani na machafuko? Mbonamlikaa kimya wakati CCM inachakachua matokeo? Au pale ilipotumia vyombo vya dola kuiba kura? Ina maana maoni ya wengi na malalamiko ya wananchi hamkuyasikia? Mbona hamkotoa tamko hapo?)

Wananchi waliowachagua wabunge hao wanapaswa kutafakari upya wawakilishi waliowachagua kama wana uelewa wa kutosha kuhusu bunge, sisi vijana wa vyuo vikuu tunajua na tunatambua kuwa Rais ni Sehemu ya Bunge na Bunge haliwezi kukamilika bila Rais na hii ndio maana kila sheria inayopitishwa na Bunge ni lazima yeye Rais aweke sahihi yake.
(Hapa mmepotoka; ina maana mnaanza kuwashawishi wapiga kura wawakatae Chadema? Who are you to do this? Waacheni wananchi wenyewe waliowachagua wabunge hawa kwa kura nyingi watoe maoni yao; unajuajje kama ndiyo walikuwa wanatekeleza mojawapo ya maelekezo ya wapiga kura wao?)

Katika mazungumo yake na waandishi wa habari wiki hii Mweneykiti wa CHADEMA MHE. Freeman Mbowe, alinukuliwa na vyombo vya habari akisema wabunge wake na madiwani wanaweza kuendelea kuwakilisha wananchi licha ya kutomtambua Rais.

Sisi tunasema hili si sahihi bali ni upotoshaji mkubwa, kamwe mtoto hawezi kudai kuwa hamtabui Baba yake kisha anaendelea kumwita Baba na kutumia kila kitu kinachotolewa na Baba huyo huyo. Huo ni utovu wa nidhamu au kukosa maadili.
(Nyie ndiyo mmekosa nidhamu! Mtu anaweza kuendelea kuwa baba lakini endapo hatiumizi wajibu wake; au hatendei haki wanawe wote basi mtoto ana hali ya kumwambia baba ‘sikuridhika na hili"!! Hiki ndicho kinafanywa na Chadema)

Sisi vijana wa vyuo vikuu Mkoa wa Dodoma tunawaomba Watanzania wote wenye nia njema na Taifa letu kuwapuuza wabunge wa CHADEMA na kutambua kuwa lengo lao ni kutaka kutuhamisha kutoka kwenye ajenda ya msingi ya Maendeleo na kubaki kwenye malumbano ya kisiasa kama tulivyoshuhudia katika nchi jirani
(Huo ndiyo mkakati wa CCM; kuleta agenda za nchi jirani kama kielelezo cha amani!! Angalia nini kimetokea Kenya, sasa wana Katiba mpya; agenda hizo zilikuwa zinaletwa na wapinzani, sasa kila kitu kiko OK!! Leo hii bado nyie manoojiita wasomi mnaona agenda za Chadema amabazo ndiyo zitatupeleka kwenye agenda ya Katiba mpya kuwa ni mwanzo wa machafuko!! What a shame? Mnanishangaza hadi leo hamjaweza kuelewa maana halisi ya mapinduzi ya kweli)

Kamwe tusikubali kudanganywa na watu wachache
(Acheni upuuzi, mbona mmedanganyika kwa CCM hadi kuitisha press conference?)
Mwisho tungependa kuwaomba Wabunge wa CHADEMA wawaombe radhi watanzania kwa kuvuruga tashwira safi ya Bunge letu lisilo na ubaguzi na itikadi za kisiasa vinginevyo wanawadharau watanzania waliowachagua wakidhani kwamba niwaadilifu wa Taifa na si cha chama chao.
(NYIE NDIYO MUWAOMBE WAO RADHI PAMOJA NA KUTUCHEFUA WANANCHI)

Tutambue kuwa kazi kubwa ya CHADEMA na Wabunge wake kwa sasa ni kuwachanganya watanzania ili badala ya kuendelea na shughuli za ujenzi wa taifa wabaki na malumbano ya hapa na pale kwa manufaa yao binafsi.
(WTF?? Na kazi yenu nyie ni nini? Mmekuwa tawi la WACHAKACHUAJI?)

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Bunge letu na kutuepusha na ubaguzi kama huu uliofanywa na baadhi ya Wabunge wa CHADEMA
(Vipi kuhusu ubaguzi unaofanywa na CCM miaka mingi tokea uhuru?)

Aksanteni sana.

IMESOMWA NA THOBIAS MWESIGA RICHARD
(who the hell are you?):angry:
 
Well: Hebu angalia mfano wanaotoa Wasomi:

Sisi tunasema hili si sahihi bali ni upotoshaji mkubwa, kamwe mtoto hawezi kudai kuwa hamtabui Baba yake kisha anaendelea kumwita Baba na kutumia kila kitu kinachotolewa na Baba huyo huyo. Huo ni utovu wa nidhamu au kukosa maadili.

Nimejaribu kufikiri uhusiano wa Wabunge wa CHADEMA kutoka nje ya Bunge wakati wa Hotuba ya Kikwete na mfano huo hapo juu sikupata mantiki. Ni kweli kwamba Kikwete ni "Baba" na Wabunge wa CHADEMA ni "Watoto" kwa ulinganifu? No, that is sheer ridiculous!
 
Vyuo vikuu?. kikiwemo UDOM au?. maana hawa hatakudai haki zao za msingi hawawezi.Hebu tafutena wa pale kileleni kwenye chuo KIKUU msikie komenti zao.Hawa wote na chuo chao ni sisiem.
 
KNOWLEDGE *IS NOT* POWER..........IT IS REALLY:
Knowledge becomes power only when it is put into action for the attainment of a definite objective.

Use your Knowledge to help your Parents by Changing the Old Constitution which does not cop with 21 century.
This is what CHADEMA are doing for now.
This CHADEMA move-OUT will help those who are not only CHADEMA Members but also all the political parties.
 
Back
Top Bottom