Tamko la TCRA kuhusu ujumbe wa simu unaomchafua Dr. Slaa

Ngoja nicrame hili jina... Kalonga Joseph... Kalonga Joseph.... Kalonga Joseph... Kalonga Joseph.... Kalonga Joseph... Kalonga Joseph... Limeshakaa, adui yangu namba moja kwa sasa...
 
Jana nimepokea ujumbe huu kutoka kijijini kwetu, kutoka kwa mwanakijiji ambaye naye alitumiwa na mtu asiyemjua:

"Tusimpe nafasi shetani ya kulimaliza Taifa lenye amani kwa udanganyifu wa sera zisizotekelezeka wanazotoa wapinzani. Pasipo Kikwete na CCM taifa hatarini"

Ujumbe huu unatumwa kwa wanakijiji!! Ambao hawasomi magazeti, na mara chache wanasikiliza habari kutoka redioni zilizochakachuliwa. Je matokeo yake ni nini???
 
Kalonga Joseph, aliyeko Guinea Bissau..... KAMA SIO LEO AU KESHO NI SIKU YOYOTE TU ATAADHIBIWA MANA AUAE KWA UPANGA NAE ATAKUFA KWA UPANGA
 
Mimi pia niliupata, siyo mara moja, hata ule unaoanzia na code +3......, Lakini mi nashindwa kujua, hawa wanaosajili simu, kwa nini wanaruhusu jumbe kama hizi tuzipate? Simu yangu inajaa jumbe za kijinga kila siku, nani kawambia ninazihitaji? Huu upumbavu, kama jamaa yao hauziki wasitusumbue kwa upumbavu wao. Aiseeeeeee, nina hasira na huu ujinga wa CCM wanaoufanya.
Na nyie watu wa mitandao, kwa nini mnaruhusu jumbe hizi?

Mnyonge, mnyongeni...................
 
Watanzania wengi tunawashangaa ccm na propaganda zao -sasa tunaiomba serikali kupitia TCRA wawakamate wanaotuma ujumbe wa simu kumzushia eti Dr.Slaa anaropoka kumwaga damu, nawahusisha ccm na watu hawa kwa sababu nimesoma magazetini na kuona wagombea wa ccm wanawaambia watanzania wasiwachague watu wanaohubiri kumwaga damu, kwahiyo kwa uhalisia wake ni kwamba wanaotuma ujumbe wa simu wametumwa na ccm kuwafikia wapigakura sasa tunaomba hatua kali zichukuliwe dhidi ya ccm. Lakini pia niwakumbushe vyama vyote kwamba watanzania kwa sasa wametoa tongotongo propaganda za kijima hazibadili kura bali zinaongeza. Wagombea wanatakiwa kuwaomba tume ya uchaguzi kutokiuka taratibu zote za uchaguzi kwakuwa kufanya hivyo ndio kutapelekea uvunjifu wa amani, niwaombe tume ya uchaguzi, na polisi kuondoa kabisa unafiki kwani wakiweka unafiki nguvu ya wa wananchi inatisha! ni balaaaaaaa, TCRA sasa mlisajiri simu zetu kuzitoa kwa wahalifu? kwanini msichukuliwe hatua?????
 
Mlimsikia yule ofisa wa TCRA the other day alipokuwa anajieleza ni kwa nini hawajazifunga hizo namba zinazotuma hujumbe wa kumchafua mgombe wa Urais kwa tiketi ya Chadema. Alisema hawawezi kuifunga mpaka wajue inatoka wapi!! Uende ikawa inatoka nje au ni hapa nchini. Maana yake ni kuwa iachwe tu hizo namba ziendelee kutuma ujumbe huo mpaka hapo zikapojulikana. Yaani kwa maneno mengine wacha zifanye kazi zake for now. Hainiingii akilini kabisa.

Wanajukwaa tatizo hapa ni kitu kinaitwa madaraka ya rais. Wakuu wa taasisi nyingi/muhimu sana kwa maendeleo ya taifa uteuliwa na kuwajibika kwa rais (Kama taasisi). Unategemea nini? Ni kuwa na kama huyo afisa wa TCRA alivyotoa majibu ambayo si-professional kwa sababu ya kutotaka kumkwaza mkuu wa taasisi.
 
Hao ni ccm tu wenye roho mbaya, hivi tuli sajiri line zetu ili watutumie upumbavu wao? Nahic wameishiwa.
 
Ni weekendi iliyopita, watanzania wengi sana walitumiwa jumbe za simu kuwa mgombea mmoja wa chama cha siasa atamwaga damu.
Mimi binafsi nilikuwa suijasikia kauli ya mwanasiasa huyo na hata kama tungesikia sisi siyo mambumbumbu kutochagua nani anatufaa.

Lakini cah kushangaza ni pale mamlaka husika zilipojifanya kutojua kabisa na hata kutofanya uchunguzi kidogo to eti code no +3.... ni yawapi wakati ni Finland. lakini pia walisema kuwa watawauliza makampuni ya simu wakati wakijua kabisa kuwa makampuni hayo hayana code hizo, na kwa ujumbe ule hakuna ambaye angekubali.

Lakiini sasa jana jioni CCM wametuma jumbe zenye kushabihiana na zile japo tofauti ni wamesema tusicahgue wapinzani.

Kwanza wana JF kuna watu wamepata hizi?
Na hatuna sababu ya kuamini kuwa waliotuma ni hao hao CCM kwa kutumia mtandao?? maana mbaya wa CHADEMA kwa sasa ni CCM peke yake na hakuna mwingine!!

Sasa kama umegombana na mtu, halafu ukadhurika, Je mtuhumiwa wa kwanza si mbaya wako!?

1. Kwanza CCM tunawashauri, kama wapiga kura wamechoka basi wasubirini tu maana kama ni amani walinzi ni wananchi na siyo chama ,
2. Chama hiki kinafahamika na mazuri yaliyofanyika yanajulikana, lakini na uchovu wake unaonekana!
3.Chama kiache kabisa kuwapotosha watu kwa hoja zisizokuwa na maana na za uwongo mkubwa.
4. Chama kiombe tu kura kwa watu kistaarabu bila ya kumhofia mtu na kumtafutia hoja ambazo hata yeye mwenyewe hajawahi kuziota.
5. CCM waachie wapiga kura waamue nani wa kuwatumikia siyo lazima wao tu.

kwa walio sikiliza BBC leo asubuhi. Mr Kinana alikiri kuwa zile msg za Kuisifia CCM wao ndio waliziandaa na Kutuma ila zile zinazochafua upinzani wao hawahusiki nazo. swali Je wamepata wapi namba zetu?
 
Mi namshukuru Mungu sijapata sms ya kisenge ila nimesikia tu watu wakilalama kuhusu hizo sms, TCRA wanajua zinatoka wapi ila kwa kuwa wanogopa ndio maana hukaa kimya au kujifanya hawajui.Hao ni CCM tu, ila mwaka huu watakiona cha mtema kuni.
 
Zaidi tusubiri uchunguzi kutoka kwa makachero wa kule Ufini ,nafikiri wengi wetu kama tutazituma akili zetu basi hatuhitajii Microscope kumuelewa ni nani, baadhi ya watu wanajiuliza hivi kwani bado yupo Ufini au tayari alikwisha rudi Tanzania? ("Stay Tuned")
 
Mbona anajulikana tayari? Anaitwa Kalonga Joseph.....................
 
kwa walio sikiliza BBC leo asubuhi. Mr Kinana alikiri kuwa zile msg za Kuisifia CCM wao ndio waliziandaa na Kutuma ila zile zinazochafua upinzani wao hawahusiki nazo. swali Je wamepata wapi namba zetu?

Kimsingi mimi roho yangu inanituma kuaminikuwa CCM ndio wanhusika na hizo zote,
IT wao wamemlipa zile pesa zetu afanye kila awezalo, na TCRA wakawapa chao wakatae na kutuzuga eti hawajui.

BILA CHADEMA MAENDELEO TZ NI NDOTO!!
 
Mi namshukuru Mungu sijapata sms ya kisenge ila nimesikia tu watu wakilalama kuhusu hizo sms, TCRA wanajua zinatoka wapi ila kwa kuwa wanogopa ndio maana hukaa kimya au kujifanya hawajui.Hao ni CCM tu, ila mwaka huu watakiona cha mtema kuni.

asante Tonge,

ni hao hao tu na hata kama siyo JK basi ni moja kati ya vibaraka wake maana ndo wanatapatapa
 
Hao ni ccm tu wenye roho mbaya, hivi tuli sajiri line zetu ili watutumie upumbavu wao? Nahic wameishiwa.

Usihisi tu ndugu, ndo ukweli wenyewe- WAMEPUKUTIKA LAKINI MDA WA KUJIREKEBISHA WANAO JAPO HAWATAKI
mihela ya TZ mitamu sana
 
kwa walio sikiliza BBC leo asubuhi. Mr Kinana alikiri kuwa zile msg za Kuisifia CCM wao ndio waliziandaa na Kutuma ila zile zinazochafua upinzani wao hawahusiki nazo. swali Je wamepata wapi namba zetu?
Sasa the same same number yao ndiyo inatuma those two kinds za smses. hivi inawezekanaje mtu atumie namba yako wakati weye unaitumia? inawezekana hiyo kweli?
Dawa ni kuwaonesha kwamba wanapoangukia wao sie tulishainuka loooong taima
 
Back
Top Bottom