Qwy
JF-Expert Member
- Nov 23, 2018
- 6,238
- 31,146
Let each side fight with the arsenals they possess, as one side uses the police so let the other side use the influence and the pressure of the international community. Fair enough.Tanzania ni nchi huru na inaongozwa na Utawala wa sheria (Rule of Law) Hakuna aliye juu ya sheria, watu wote wapo sawa mbele ya sheria, mtu yeyote akifanya kosa lolote la kijinai atachukuliwa hatua za kisheria bila kujali nafasi yake, rangi take au jinsia yake.
Mbowe anatuhumiwa kwa makosa ya Kigaidi yeye na genge lake, ni kinyume cha Utawala wa kisheria kuanza kumtetea Mtuhumiwa/watuhumiwa kabla hata hajafikishwa Mbele ya Mahakama.
Tanzania inaheshimu utawala wa sheria na lazima Mbowe atafikishwa mbele ya Mahakama kujibu tuhuma na bila shaka watapata nafasi ya kujitetea, kinacho fanywa hivi sasa na Viongozi wa chadema ni kujaribu ku "frustrate" mchakato wa kumshitaki Mbowe kwa tuhuma za ugaidi kwa kutumia vyombo vya habari vya kimataifa, wakiamini kuwa Vyombo vya ulinzi vya tz vitaogopa na kurudi nyuma, hilo ndio lengo la chadema hivi sasa. wanaitishia nyau serikali makini!!!
Naamini vyombo vyetu vya ulinzi na usalama havitoingia kwenye mtego wa chadema wanao fanya hivi sasa kamwe vyombo vyetu visitetereshwe wala wasiogope kufuata utawala wa sheria kwa kumhofia Mbowe au hata mtu mwengine.
Utawala wa sheria ni "Hakuna aliye juu ya sheria".
Mbowe hatuko juu ya sheria lazima ashitakiwe na kwa kufanya hivyo ndio kuheshimu na kufuata utawala wa sheria.