Tamko la Mkurugenzi wa TCAA Hamza Johari kuhusu waunda ndege wazawa ni la hovyo

YEHODAYA

JF-Expert Member
Aug 9, 2015
36,910
51,904
Mkurugenzi wa mamlaka ya anga TCAA Amesikika vyombo vya habari akisema kuwa ni marufuku watu kutengeneza ndege kienyeji linaua ubunifu wa watu na kwenda kinyume na sera ya viwanda Ya Magufuli.Yeye kama mkurugenzi wa Anga hakutakiwa kutoa Tamko koko kama lile alitakiwa awaalike watu ofisini kwake wote wanaotaka kuunda ndege awasaidie namna wanavyoweza kufanikisha azima yao au awatembelee ajue namna ya kuwasaidia.

Yupo pale kuwasaidia watu wafikie ndoto zao sio tu kusema ni marufuku.Anaua ubunifu na vipaji vyao.Yeye anatakiwa awabaini na atafute mbinu zipi za kuwasaidia hadi ikiwezekana wawe na viwanda vyao vya kuunda ndege au helikopta.Wakurugenzi mamangi meza kama hawa hawawezi isaidia nchi kufikia kuwa ya viwanda.

Kila mkurugenzi anatakiwa ajipange ajue atafanyaje kuiwezesha nchi kuwa ya viwanda katika eneo lake siyo ashinde anaota atafanyaje kuikwamisha nchi kufikia kuwa ya viwanda

Angalia huyu Mkenya alivyojitengenezea ndege kienyeji

 
Wewe endelea kushangilia na kuimba mapambio ya mtukufu,maraika mkuu na mtakatifu Pombe.Mambo ya ubunifu na ugunduzi sio saizi yako.

Wabunifu wengi nchi hii ni watu ambao wengine hata kusoma hawajasoma.Wasomi inabidi watafute namna gani ya kuwasaidia sio kutumia elimu zao kuwakatisha tamaa au kuwavunja moyo kwenye ugunduzi wao hata uwe mdogo na wa kiwango cha chini vipi wawatie moyo
 
1468995131330.jpg
 
Sheria za kimataifa haziruhusu ugunduzi wa kitu ambacho tayari kimekwishagunduliwa, kwanza wanatumia injini za magari
Huo ni uwongo uliokubuhu.Kinachozuiliwa ni kuiga kitu chenye hatimiliki (copyright) lakini waweza unda gari yako ukitaka hata leo mradi usiite TOYOTA iite hata HOYOTA hakuna atakaehangaika na wewe.

Kuhusu kutumia injini ya gari nao ni ubunifu.Mbona ziko ndege wamegundua zinatumia Mwanga wa jua (solar). Mara ya kwanza watu wa Anga walipinga kuwa ni hatari lakini wagunduzi wakakomaa tu wakawapuuza.
sasa hivi hiyo hapo inazurura duniani kwa majaribio.Unaweza gundua gari hata inayotumia pumba ni ugunduzi

 
Inashangaza sana, tutaendelea kutegemea wazungu siku zote. Badala ya kuwapongeza na kuwatembelea na kuwasaidia mahali wanapokwama, WANAZUIWA!!!! Waliounda ndege wale wa kwanza familia ya Wright hawakuzuiwa ndo maana tekinolojia imefika hapo
 
Inashangaza sana, tutaendelea kutegemea wazungu siku zote. Badala ya kuwapongeza na kuwatembelea na kuwasaidia mahali wanapokwama, WANAZUIWA!!!! Waliounda ndege wale wa kwanza familia ya Wright hawakuzuiwa ndo maana tekinolojia imefika hapo
Mie nadhan wangechukuliwa na kupelekwa hata veta kupata ujuzi zaidi na kuwezeshwa na serikali na si kuwazuia. Hakika tanzania kuendelea ni vigumu sana
 
Hata mimi wakuu nimesikitika sna kusikia tamko.Ingekuwa ni mweupe anayengeneza angekaa kimya.Watu kama hawa wangepelekwa sido na kupewa vifaa na siku moja wangeweka historia.
 
Hata mimi wakuu nimesikitika sna kusikia tamko.

Mkuu yaani mamlaka zetu za anga waafrika sijui kuna tatizo gani kwenye waongozaji.Kuna mamlaka ya Anga Swaziland imepitisha sheria ya kuwakataza wachawi wakiruka angani wasizidi mita 150 kutoka aridhini .Kama wakiruka angani zaidi ya mita hizo watakamatwa na mamlaka na kutozwa faini ya rand 500,000!!! Huo ndio ubunifu wa mamlaka ya anga ya swaziland!!! Habari yao hiyo hapo

Swaziland bans witches from 150m flying
 
Mkurugenzi wa mamlaka ya anga TCAA Amesikika vyombo vya habari akisema kuwa ni marufuku watu kutengeneza ndege kienyeji linaua ubunifu wa watu na kwenda kinyume na sera ya viwanda Ya Magufuli.Yeye kama mkurugenzi wa Anga hakutakiwa kutoa Tamko koko kama lile alitakiwa awaalike watu ofisini kwake wote wanaotaka kuunda ndege awasaidie namna wanavyoweza kufanikisha azima yao au awatembelee ajue namna ya kuwasaidia.

Yupo pale kuwasaidia watu wafikie ndoto zao sio tu kusema ni marufuku.Anaua ubunifu na vipaji vyao.Yeye anatakiwa awabaini na atafute mbinu zipi za kuwasaidia hadi ikiwezekana wawe na viwanda vyao vya kuunda ndege au helikopta.Wakurugenzi mamangi meza kama hawa hawawezi isaidia nchi kufikia kuwa ya viwanda.

Kila mkurugenzi anatakiwa ajipange ajue atafanyaje kuiwezesha nchi kuwa ya viwanda katika eneo lake siyo ashinde anaota atafanyaje kuikwamisha nchi kufikia kuwa ya viwanda

Angalia huyu Mkenya alivyojitengenezea ndege kienyeji


TCAA ni Regulatory Authority iliyopo kisheria, Agizo kwenye andiko la Mkurugenzi ni matakwa ya kisheria yenye lengo la kulinda usalama wa watu na mazingira ambapo hiyo ndege itaoperate, msilete ushabiki wenu wa siasa kwenye mambo ya kitalaamu. Gundua chochote lakini matakwa ya kisheria na kanuni yatimizwe.
 
Msiwe ****** nyie TCAA ni Regulatory Authority iliyopo kisheria, Agizo kwenye andiko la Mkurugenzi ni matakwa ya kisheria yenye lengo la kulinda usalama wa watu na mazingira ambapo hiyo ndege itaoperate, msilete ushabiki wenu wa siasa kwenye mambo ya kitalaamu. Gundua chochote lakini matakwa ya kisheria na kanuni yatimizwe.

Matakwa hayo ya kisheria yanamtaka azuie watu kwenye karakana zao iwe vyuoni,kwenye magereji au majumbani kuunda ndege? Zikiwa ziko chini aridhini kwenye maabara zinaundwa haziko hata kwenye majaribio ya kurushwa hazijapaa hata sentimeta moja hewani ni kazi yake kuzuia?
 
Kama ni mimi Rais ningemtumbua mkurugenzi TCAA
Badala ya kumsuport mtu kukuza kipaji mnampiga marufuku
Mpeni utaratibu wa kufanya na pa kufanyia kazi zake na mazoezi pia
 
Matakwa hayo ya kisheria yanamtaka azuie watu kwenye karakana zao iwe vyuoni,kwenye magereji au majumbani kuunda ndege? Zikiwa ziko chini aridhini kwenye maabara zinaundwa haziko hata kwenye majaribio ya kurushwa hazijapaa hata sentimeta moja hewani ni kazi yake kuzuia?
Ili ipae si inabidi iundwe?Regulation zinapaswa zifuate kuanzia kwenye wazo mpaka utekelezaji.
 
Mwalimu aliwaita baadhi wajinga huku akiwa makini kutumia neno 'wapumbavu', JPM kawaita baadhi Vi.laza, Mzee Mwinyi alisema wendawazimu, Mkapa akaita 'wapu.mbavu' na malofa, huyo JK namweka akiba.

Hoja yangu ni kuwa hawa ndio sisi na sisi ndio Watanzania na sina uhakika hawa viongozi walikuwa wakiongelea asilimia ngapi hasa ya Watanzania 50,000,000. kikubwa ni kuwa hata aliyetoa hii kauli anaangukia kwenye maneno haya ya watangulizi.

Nilivyoisikai hiyo kauli nikajiuliza na naendelea kutafuta katika historia kama kweli 'TCAA' za huko kwingine ziliwahi kutoa amri au tamko kuwa 'wananchi anzeni kutengeneza ndege' ili kulilinganisha na hili la "hamruhusiwi kutengeneza ndege".
 
Back
Top Bottom