Tamko la mbunge Ubungo kuhusu bomoa bomoa ya Magufuli

Sasa kwa nini huo wingi wa magari unaonekana kwenye makutano tu?

Halafu, ni kuwa impractical kutufananisha na France. Too utopian. Tanzania yetu hii mmejaa mafundi mchundo ambao hata kujenga kibarabara hamuwezi (asingekuwepo Mchina hapa, ushamuona Mchina anajenga barabara Paris? Kama umepita/umeishi hiyo miji ya Magharibi na Latin America, tuambie, ushaona Mchina kavaa helmet Copenhagen huko?), ndo tutaweza kujenga hiyo mipango miji ya La Defense na Brazil, please!

Ndo maana, kwa kuanzia, napendekeza kinachowezekana. Small-minded you may call it, but it is the practical model you can be afford technically and fiscally.

Mkuu, neno "peke yake" unalielewa lakini? Taa, makutano n.k. zote zinachangia kuleta foleni lakini si main cause. Sababu kubwa ni watu wengi kuelekea upande mmoja kwa wakati mmoja. Hii inasababishwa na watu wanakoishi na wanakoenda kujitafutia riziki, starehe, manunuzi ya kawaida n.k. Haya yote yanatokana na jinsi mji ulivyopangwa na si taa au sheli.

Kumbe tatizo lako ni mafundi mchundo? Kwa vile haujaona mswahili amevaa helmeti basi unataka kututosa wote? Hivi unadhani hizo unazoita overpass atajenga nani? Mbona siku hizi karibu kila kitu kinatengenezwa uchina, basi ina maana kuwa hao wa nchi za magharibi wamekuwa hamnacho? Hivi kama unataka kujipima afya, utajifananisha na mgonjwa? Mifano niliyokutolea inahusu mipango miji, na kinachotakiwa ni ubunifu tu ili kuhakikisha utatumia fedha kiduchu ulizokuwa nazo kwa ufanisi zaidi.

Unachopendekeza ni utopian, based kwenye picha za fly-over za nchi za magharibi bila kujua adha zake. Na ni kweli small minded kwa maana ni mfano wa jinsi tunavyopenda majibu mepesi kwa maswali magumu. Kama vile kumkata mtu mguu kwa vile ana kidonda bila kuchunguza chanzo cha kidonda.

Kwa vile inaelekea uko hapa kubishana na si kujadiliana basi naona heri nikuachie forum.

Nilikuwepo.

Amandla......
 
Mkuu, neno ...
Vitu vinavyotengenezwa China si vyote ni vya "Kichina". Kampuni za Ulaya na Marekani zinapo outsource labor fahamu kwamba ni wao wenyewe bado wanafanya designing and managing the production to their own specifications. Ukiona sneaker ya Nike inauzwa USA imeandikwa ''Made in China'' usidhani ni Nike ya Kichina! Sisi ndio tunaletewa vya Kichina vilivyo design-niwa na Wachina, kwa vile hatuna utaalam wala balls za kukataa kuwa dumping ground kwa sababu tumejawa na mafundi mchundo.

Huwezi kujifananisha na mgonjwa any more than huwezi kufananisha mtoto na mtu mzima hata kama wote si wagonjwa. Wewe nchi yako haina hata infrastructure ya kuhifadhi mabomu, watu wanaishi kwenye tembe za udongo na kulala na mbuzi, leo mjenge miji mipya ya La Defense na Copenhagen you sound funny and utopian.

"Sababu kubwa [ya foleni] ni watu wengi kuelekea upande mmoja wakati mmoja" hatujui hilo. Kwa nini foleni zipo kutwa nzima? Watu wote wanaenda "kujitafutia riziki, starehe, manunuzi ya kawaida" wakati huo huo, sehemu hizo hizo? Na kwa nini kwenye makutano yenye foleni nzito unakuta pande zote nne zimejaa msururu, wale wote wanaelekea kumoja? Hatujui kwamba "kuelekea upande mmoja" ndio sababu kubwa, hujafanya utafiti, huna haki ya kuongea mahitimisho hapa. Tuanze na tunachokimudu, overpass kwenye makutano ya barabara kubwa zinazosababisha msongamano.

Kwa vile inaelekea uko hapa kubishana na si kujadiliana basi naona heri nikuachie forum.
Fundi Mchundo, you can bow out of a debate civilly, no need for "uko hapa kubishana, nakuachia jamvi..." Crass!

Hata wewe unanibishia hoja yangu! Wote tuna approach tofauti, sasa kwa nini iwe ya kwangu ndio inabishia ya kwako? Na hata kama ningekuwa nimebisha, mtu "anapobisha" maana yake umeshindwa kum convince! Unataka usipingwe umekuwa Anna Makinda? Au Gaddafi? Watanzania tujifunze kuumiza vichwa bila kukimbilia kusema "anabishana." tuko hapa for diversion tu, don't take these things too seriously, you think Magufuli is gonna read these proposals for sure? Get a grip. Kuna ubaya gani ku debate the best ways to solve national crises such as road jams?
 
Back
Top Bottom