Fumadilu Kalimanzila
JF-Expert Member
- Dec 10, 2016
- 1,651
- 5,126
Ni hivi karibuni tu Paul Makonda akiwa amewaita viongozi mbalimbali wa dini pale Julius Nyerere Convection Center kuwafundisha na kuwahabarisha kuhusu " maajabu" aliyofanya Mheshimiwa Rais Dr.John Pombe Joseph Magufuli kwa kipindi cha miaka 4.
Mhashamu Baba Kadinali Pengo alisikika akisema Makonda ni mmoja wa viongozi majasiri wanaofaa kuwa warithi wa Magufuli hapo baadaye!
Mhashamu Baba Kadinali Pengo alitoa hiyo "reckless statement " bila kuzingatia mwenendo wa Makonda katika kipindi hiki cha Serikali ya Awamu ya 5 na hisia za jamii pana juu yake!
Leo mtu tuliyeambiwa na Mhashamu Baba Kadinali Pengo kuwa anafaa kuwa mrithi wa Magufuli ,Marekani wana m- Brand kama mtu asiyependa kuishi kwa watu wengine, yaani kwa maneno rahisi ni sawa na kusema ni "Muuaji" !
Mimi kama Mkatoliki napata wasiwasi isijekuwa baadhi ya Viongozi wetu wa Dini hapa Nchini hawana tofauti na Viongozi wa Dini pale Uganda waliomkumbusha Rais Yoweri Kaguta Museveni kuwa hakuzaliwa 1943 bali alikosea alizaliwa 1947 ili tu apate uhalali wa kugombea Urais comes 2021!
Mhashamu Baba Kadinali Pengo alisikika akisema Makonda ni mmoja wa viongozi majasiri wanaofaa kuwa warithi wa Magufuli hapo baadaye!
Mhashamu Baba Kadinali Pengo alitoa hiyo "reckless statement " bila kuzingatia mwenendo wa Makonda katika kipindi hiki cha Serikali ya Awamu ya 5 na hisia za jamii pana juu yake!
Leo mtu tuliyeambiwa na Mhashamu Baba Kadinali Pengo kuwa anafaa kuwa mrithi wa Magufuli ,Marekani wana m- Brand kama mtu asiyependa kuishi kwa watu wengine, yaani kwa maneno rahisi ni sawa na kusema ni "Muuaji" !
Mimi kama Mkatoliki napata wasiwasi isijekuwa baadhi ya Viongozi wetu wa Dini hapa Nchini hawana tofauti na Viongozi wa Dini pale Uganda waliomkumbusha Rais Yoweri Kaguta Museveni kuwa hakuzaliwa 1943 bali alikosea alizaliwa 1947 ili tu apate uhalali wa kugombea Urais comes 2021!