Mdau nakushukuru,nimekisoma hicho kipengele na kukielewa vema.Na kwangu nadhani hoja kubwa iko hapa,nanukuu"5. Kamati Kuu inaamini kuwa pamoja na Sheria ya Mabadiliko ya Katiba kupitishwa, bado kuna fursa za kisiasa na kijamii katika kujenga mwafaka wa kitaifa juu ya haja, nia, mchakato na misingi ya Katiba Mpya." mwisho wa kunukuu. Kimsingi sina tatizo na hoja hii. Lakini binafsi nilidhani kwamba ingekuwa jambo la busara zaidi kama Kamati kuu ya CDM ingekuja kwanza na azimio hilo la kutaka kukutana na JK kabla ya kuutangazia umma maazimio haya. Maana hii sentensi niliyoinukuu inajiielekeza huko.Baada ya kukutana na Rais Kikwete ndipo sasa,kamati kuu ya CDM ndipo ingekuja na maazimio yao.Hapo binafsi naamini ingekuwa imekaa vema.Maana sasa ninachokiona hapa ni kwamba maazimio ni mazito yakimlenga moja kwa moja Rais JK. Sasa unapotaka kukutana na mtu huyo huyo baada ya kuwa umeshamsema,mmm kidogo inaleta shida.Sina tatizo na wazo la CDM kukutana na Rais.Lakini approach ndio inanisumbua.
Ni tamko zuri sana, lakini tusiliangalie kisiasa na wala kishabiki. tuliangalie kwa maslahi ya taifa na nyuma ya pazia ya objective za CDM, CCM, Makumdi ya CCM na watu wanaofadhili makundi ya CCM na nyuma ya pazia ya objectives za CDM katika mustakabali wa taifa hili. Hili ni tamko jepesi sana kuliandika na kulishabikia kimaslahi, lakini ukiangalia kwa makini ni tamko gumu kwa vizazi vyetu vijavyo vya Tanzania kama taifa. Bwana Pascal ktk thread moja ambayo ipo na bado ni hot kuendelea kuchangiwa, amewakosoa CDM kuwa walichemka kutoka bungeni, na hakatai kuwa walikuwa na pointi za msingi. walichofanya CDM ni sawa na opponents wa Liberia. Kwa kifupi CDM wametangaza serikali yao nje ya mfumo rasmi, na kwa hili tusitegemee chochote chema kwa taifa letu zaidi ya vurugu za umwagaji damu. hii ni kwakuwa, iliyopitishwa naitakayosainiwa kwa mbwembwe na mtukufu raisi, ndiyo sheria, na inabaraka zaidi ya nusu nusu ya wabunge wa upinzani, forget about kambi rasmi ya upinzani(Hawajiamini hawa jamaa, na ndiyo maana wanajiita kambi rasmi). CDM ni wapotoshaji, na huitaji kuwa na PHd ya phychology kujua hawa jamaa ni wapotoshaji na waongo.
ccm inatoa tamko chadema inatoa tamko mnatuchosha tuchague lipi? tengenezeni utaifa katika mjadala huu
Ikiwa hilo ndiyo tamko la magwanda, ama kweli mna "wasomi" na si wasomi. Hivi kama chama cha upinzani mmekaa haswa mkachemsha vichwa vyenu mkaja na tamko kama hilo? nashindwa kuamini nnayoyasoma kuwa yanatoka kwenye "wasomi". Khaaaa!
Nna uhakika hayo kayaandika Mbowe.
Zitto uko wapi? tazama hawa wenzako wanavyokitia aibu chama ulichokipagania mpaka kwa afya yako. Pole sana Zitto najuwa una kazi kubwa sana, Mwenyeezi Mungu atakulinda na kukusaidia. Sikuwepo kwenye hicho kikao wala sijasikia zaidi ya hayo niliyoyasoma hapo juu, lakini nna uhakika hukutia hata lako moja. Hii si "calibre" yako.
nahic unaumwa,au ni mgeni hapa tz.mwisho wa siku ni wanaounga mkono waseme ndiyoooo,spika anachagua kipi asikilizehoja hizi zingetolewa bungeni pengine zingesaidia kuleta muafaka kama chadema wasingesusia bunge
Ndugu yangu upo sahihi KABISAA!Mkweche umesema kweli kuwa JK ni rais wa Tanzania hadi 2011. Lakini napingana nawe kuwa JK alichaguliwa na watanzania; Kiuhalisia JK alichaguliwa na watanzania takribani 5,000,000 baada ya mahesabu ya kura kuchakachuliwa na NEC. Najua unafahamu kuwa nchi yetu ina watu zaidi ya 46,000,000, na idadi ya watu walioandikishwa kupiga kura ilikuwa ni about 21,000,000. Hii inadhihirisha kuwa zaidi ya wapiga kura 15,000,000(76.2%) hawakumchagua JK. Ni katiba mbovu ndiyo inayohalalisha watu wengi kuchaguliwa rais na wachache. Rais wa namna hii hana Legitimacy ya kutawala Watanzania walio wengi. Ndio maana kila kona ya nchi hii kuna malalamiko kuhusu uongozi mbovu unalisababishia taifa hili matatizo mengi kama vile njaa(pamoja na kilimo kwanza), mfumuko wa bei, utawala kandamizi wa kutumia jeshi la polisi dhidi wananchi wanaodai haki zao za msingi, ufisadi uliokithiri nk.
Rais wa namna hii ataendelea kutumia nguvu ya dola na uwingi wa wabunge wa chama chake kutunga sheria ambazo wananchi wengi hawakubaliani nazo. Mswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba hauna maslahi kwa watanzania ndio maana umepingwa na watu walio wengi. CCM na wabunge wake walipaswa kusikiliza maoni ya wanachi kabla ya kupitisha msawada ule. CDM walifanya sahihi kukataa kushiriki kupitisha mswada uliolazimishwa kusomwa mara ya pili kwa lengo la kuwanyima wananchi uhuru wa kutoa maoni yao. CCM walijua wangeruhusu wananchi kutoa maoni yao, mswada ule ukipingwa na usingepita. Hivyo Wabunge wa CCM na spika wao aliyewekwa na mafisadi(kwa mujibu wa Samweli Sitta) wakatumia wingi wao badala ya hoja kupitisha mswada ule.
Kwa mtazamo wangu JK na CCM hawana dhamira ya dhati ya kuwawezesha watanzania kupata katiba mpya itayokidhi mahitaji ya watanzania; wanachofanya(CCM) ni kuhakikisha inapatikana katiba itakayolinda maslahi ya chama chao na mafisadi ili waendelee kutawala kwa mabavu. Kamwe kwa utaratibu huu haitapatikana katiba bora.
kwa kifupi hii ni NGO ya kichaga.
CUF wanaitwa CCM B, so na CDM tuwaite CCM C!!!
Ndugu yangu upo sahihi KABISAA!
Shaka yangu ni kumfata mtu ambaye system yake ipo Kazini!sidhani kama ya Bungena yatatofautiana na atakayosema!Vinginevo ni bora kukiri yeye ndio Last Say katika hili