Tamko la Kamati Kuu ya CCM; Muda waongezwa kujivua gamba

Kamati kuu "CC" ya chama tawala imeishauri serikali kuangalia namna itakavyoweza ili bei ya mafuta ya taa iweze kupungua. Ninawapongeza kwa kuliona hilo ila nataka kujua kama waziri wa fedha Mkulo alipokuwa anapanga haya ya kuongeza bei ya mafuta ya taa alikuwa peke yake? Hakuwa na viongozi wenzie wa chama tena wengi wao wako ndani ya CC? Kwa maana hiyo basi maamuzi yao huwa ni ya kukurupuka? Hivi hawakujua kuwa mafuta ya taa yanamgusa kila Mtz na sana sana yule wa hali ya chini kabisa. Nafurahi kwamba wamejikosoa wenyewe ila katika hili la kuongeza bei ya mafuta ya taa eti kwa ajili ya kuwathibiti wachakachuaji halikuwa na maana yeyote ile ya msingi.. serikali kama imeshindwa kuwathibiti wanaochakachua hivyo mbadala wake ni kupandisha kodi? Kodi ndio mbadala wa kuwathibiti wezi? Sio kwenye mafuta ya taa tu hata kwenye sukari serikali imeshindwa kuthibiti mfumuko wa bei.. je nako tuongeze kodi ili bei ya sukari isichakachuliwe?
Nilimpenda Mbunge mmoja ndani ya Bunge linaloendelea pale aliposema "CHAMA LEGE LEGE HUZAA SERIKALI LEGE LEGE" hivyo chama tawala kiko lege lege na ndio haya tunayoyaona ya kuwa na serikali yenye ufikiri mdogo usio na maslai kwa wananchi wake kwa kuongeza kodi kwenye mafuta ya taa ili kuwathibiti wachakachuaji.
Tuamke na kubadilika na tukumbuke ya kwamba chama tawala ndicho kimeshika dola lkn vile vile vyama vya upinzani viko na mambo mazuri sana basi tuyachukue na kuyafanyia kazi na wala si kwa kubeza, tumesikia kule Marekani Bunge la Congress limepitisha muswada muhimu ili kuiepusha hatari iliyokuwa inainyemela serikali ya Obama kukosa pesa.. wameungana wakaweka tofauti zao pembeni ili kuinusuru serikali yao. Sisi hapa mazuri yakitoka kwa wapinzani ni kubeza tu, hatutafika kwa mtindo huu tunatakiwa tubadilike na nchi hii ni yetu sote haikuzaliwa kwa ajili ya ccm pekee hapana ni yetu sote.
Tafadhali bei ya mafuta ishuke haraka sana kwani inatutesha tuliowengi.

Mungu ibariki Tanzania,.. sana sana viongozi wake ili wajue namna ya kuwatumikia wananchi wake.. Mbarikiwe!
 
Hili tamko la kamati kuu ya CCM lingekuwa na uzito kama Raisi na Mwenyekiti wa chama wangekuwa watu wawili tofauti. Vinginevyo hili ni tamko la Sekretariat inayoongozwa na Katibu mkuu na siyo tamko ya CC inayoongozwa na mwenyekiti wa chama.
 
Hapa sasa ndo kifo cha magamba make Nape ajiandae kujibu maswali magumu juu ya mapacha wa3,huyu Vasco kweli ni 'changanya za kwako',sasa balaza la mawazili ni ccm tupu walipokaa wakaona mafuta ya taa yapande bei,leo kwenye cc anawaongoza wenzie waseme mafuta ya taa yashushwe bei,sasa sijuhi huku alimwogopa nani kubadilika hivi ama anaonesha uzuzu wa cabinet yake kwamba hawakumshauri rais wao?

a contradicting decision,na ndo maana hata mawaziri wake hawamwelewi kwa maana anakaa nao wanaelewana hivi alafu akienda huku anaongea vinginevyo,kumbe yeye ndo chanzo namba1 cha serikali yake kupwaya hivi na hata kama ni hujuma yeye ndo anajihumu,maamuzi ya hivi nayakumbuka kama ile ishu ya bomoabomoa pale Ubungo,uzinduzi hoteli pale Arusha n.k

Nalazimika kukiri kwamba kwa stairi hii si ajabu hii nchi yetu ikawa imeuzwa kiasi ambacho hatujajua na tukija kujua tutakuja kujuta na tutalia sana!

Kwenye nyekundu
Inawezekana yalipanda bei kwa shinikizo la "lobbyist" ndani ya baraza la mawaziri kama alivyodai Mh. Zitto
 
Watu wazima na familia zao wanakuja na solutions za kitoto namna hii katika masuala ya kitaifa?
 
...Kweli haya sasa ni maigizo, Mhe. amepitisha bajeti na kukubali bei ya mafuta ya taa ipande akiwa kama mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri, then huku akiwa kama mwenyekiti wa CC anasema hapana bei ya afuta ya taa ishushe tena anaiamuru serikali hiyo hiyo anayoongoza yeye!!

Waziri akiyapinga hadharani maamuzi ya Baraza la Mawaziri, anashinikizwa kujiuzuru. Sasa Rais akiyapinga hadharani maamuzi ya Baraza la Mawaziri, hali inatakiwa iweje?
Naombeni mwongozo.
 
Yani kwenye kikao cha baraza la mawaziri wameamua mafuta ya pande bei, kwenye halmashauri ya magamba wanasema bei ishuke eti inamuumiza mtu wa chini, vikao vyote hvyo mwenyekiti mmoja. Hakika bora tz bora hata tungempa DOVUTWA tujue moja.
Only in Tanzania
 
Ni mjinga ndio hataelewa mbinu hii ya kuwadanganya wananchi kuwa CCM inawajali kwa tamko ili; kwani serikali iliyoamua kuweka kodi kwenye mafuta na hatimaye bei kupanda ni ya CCM chini ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete ambaye ndiye yule yule mwenyekiti wa CCM, je hakuliona ili akiwa kama Rais na anakuja kuliona akiwa kama Mwenyekiti wa chama? Na hata kama ni kweli wameliona hilo kwa sasa ina maana wana-poor thinking na vision kwa maslahi ya walio wengi. Hivi inakuwaje JK anajisisitizia mwenyewe kuhusu EWURA?
 
Hapo kwenye Black, huyo kwisha habari yake hana lolote. hapo kwenye red hao wameshakula ban ni washenzi sana, na kwenye blue huyo ndio umsahau kabisa maana ana gari mpya Nissan yeye sasa hivi kazi yake ni misele tu kwenye mitaa ya New York, USA.
Huyo namba 9 ni kama katoon huwa hata hajui kama yupo facebook au yupo JF, huyo namba 10 kuondoka kwa Makamba kwenye secretarit kumemuathiri sana maana hayupo kwenye payroll ya Nape. sasa hivi anafanya propaganda kwa kinyongo

Mkuu namba mbili na tatu ni mtu mmoja.
 
"Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM imemaliza kikao chake cha siku moja usiku wa tarehe 31/07/2011 mjini Dodoma chini ya uenyekiti wa Mwenyekiti wa CCM Taifa, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete."
HALAFU
"Kamati Kuu haijaridhishwa na kiwango cha bei ya mafuta ya taa nchini kwa kuwa ndio nishati inayotumiwa na wananchi wengi wenye kipato cha chini. Aidha Kamati Kuu haikuridhishwa na maelezo ya kupandishwa kwa bei ya mafuta hayo kwa kisingizo cha kuzuia uchakachuaji wa mafuta mengine. Hivyo basi, Kamati Kuu imeiagiza Serikali kutafuta njia za kushusha bei ya mafuta ya taa na kuvitaka vyombo vya Serikali vinavyohusika na usimamiaji wa ubora wa mafuta, vihakikishe vinatimiza wajibu wake kuzuia kabisa mtindo wa uchakachuaji wa mafuta nchini na si kupandisha bei ya mafuta ya taa kama suluhisho"

-----------------------------------------------------------
SS WANAMLALAMIKIA NANI?
 
Hayo maamuzi yalitakiwa yafanye na nape pamoja na msekwa pekee ilitosha kuliko kupoteza muda na pesa za chana,hawana huruma kabisa na pesa za ruzuku za walipa kodi wa nchi hii.
 
Jamani..Kikwete hakujua kama mafuta yameongezwa bei,mnamuonea buree..hata yeye ameona kwenye magazeti hizi taarifa kama sisi tu!
 
Wana jf nisaidieni, kwenye nec kuna watu waliopo serikrini. Kwenye ccm kuna watu wliopo serikarini. Bungeni kuna watu waliopo serikarini. Sasa vikao vya juu magamba wanapo sema wataishauri serikari ipunguze bei ya mafuta ya taa na kusolve tatizo la umeme, je hao walioamua hayo, je,baadhi yao si ndo hao hao wamo humo humo serikarini? Wakiwa huku wanaamua hivi na wakiwa kule wanaamua vile. Je si ndio wale wale kwenye serikari ile ile? Sasa wataishauri serikari ipi? Au wakati hayo yanaamriwa na wananchi wanalalamika masikio yao na macho yao yalikuwa yameziba?
 
[h=2]By Florian Kaijage

2nd August 2011
[/h]



CCM Ideology and Publicity Secretary Nape Nnauye briefs the media in Dodoma yesterday on resolutions made by the ruling party�s Central Committee at its meeting held in the municipality at the weekend.



Two sitting Members of Parliament, both prominent members of the ruling CCM and former cabinet ministers, have been given until next month to relinquish their positions in the party or risk being shown the door.

Former Prime Minister Edward Lowassa and former Attorney General Andrew Chenge are associated – alongside businessman Rostam Aziz – with controversial transactions that have cost the country dearly financially and in various other ways as well as tainted the party’s image.

However, Aziz has since heeded calls by the party that he give way by recently resigning as member of the powerful CCM National Executive Committee (NEC) and as MP for Igunga constituency in Tabora Region.

The deadline just given is among the resolutions made here by the party’s Central Committee (CC) that also set the date for the next sitting of the NEC, the body empowered to take measures in line with the decision reached in April this year in connection with the matter.

At its April meeting, also held here, the committee resolved that all CCM leaders associated with corrupt practices resign from all party’s positions, failure which the party would act hard against them.

“NEC will meet again sometime in September where, among other things, it will evaluate the progress made in implementing previous decisions,” CCM Ideology and Publicity Secretary Nape Nnauye declared at a media briefing at the end of the CC meeting yesterday. “The party is determined to ensure that the party cultivates and promotes ethical practice within all its ranks and calls upon all those ordered to resign to use the time available to act accordingly in the party’s interest,” he said.

Commenting on widely circulating reports that CCM was reluctant to take measures against beleaguered bigwigs Lowassa and Chenge for fear that their popularity among MPs would see the party disintegrate, Nnauye said: “‘No individual within CCM is more famous, popular or important than CCM itself. CCM is not worried about or scared of anything or anyone. It’s much better that we lose a constituency or a ward in a by-election than continue embracing unethical leaders.”

He brushed aside “any possibility” of the party standing on dangerously shaky ground by taking the decisions it was taking, noting: “Let all those thinking or believing that they can lure CCM members to defect proceed with their plans. We once had strong leaders such as (former minister) Augustine Mrema and (former Zanzibar Chief Minister) Seif Shariff Hamad and they defected, yet CCM has weathered the storms and remained unshaken.”

Reacting to the trio’s pronouncements to the effect that NEC has never directed that they resign, as repeatedly reiterated by members of the party’s secretariat leaders, Nnauye said information on all resolutions is always relayed during formal meetings “and there was no way they can be altered at random”.

Lowassa resigned as PM in February 2008 after being associated with involvement in a controversially awarded tender for emergency power generation to Richmond Company, which had no capacity to deliver. He however, remains a NEC member and legislator for Monduli.

Chenge, who similarly still sits on the NEC and is MP for Bariadi West, is said to have benefited financially from the 1999 controversial purchase of radar from the UK at a cost of 40 million sterling pounds instead of the market value of around 12 million pounds. He resigned as Infrastructure minister in 2008 following intense pressure from the public.


Rostam Aziz is said to be closely connected to the company which many believe contributed to Lowassa’s fall from grace. This is none other than Kagoda Agricultural Ltd, one of the firms that benefited from the 133 billion/- suspiciously withdrawn from the Bank of Tanzania’s External Payment Arrears (EPA) account in 2005.


The trio’s suspicious practices and behaviour are widely believed to have contributed to CCM’s relatively poor performance in the October 2010 General Elections that saw eventual presidential poll winner Jakaya Kikwete to garner a mere 61 per cent of the total vote compared to 80 per cent in 2005.


CCM also suffered massive defeats in key urban constituencies in Mwanza, Mbeya, Arusha, Iringa and Dar es Salaam regions. The Opposition camp shone in some traditionally CCM strongholds in the rural parts of Shinyanga, Mwanza, Kigoma, Mbeya and Arusha regions.


Unlike Lowassa and Chenge, who have yet to heed CCM’s resignation orders, Rostam Aziz announced his resignation from the NEC and as MP on July 13.

Nnauye said CCM will soon draw up a timetable that would lead to the announcement of the party’s flag bearer in the Igunga by-election.

“CCM has received and accepted Aziz’s decision to relinquish his posts in the party and as an MP and has resolved that all campaign-related activities will be conducted under the leadership of our Tabora regional and Igunga district offices. We are confident that we will retain the constituency,” he added.




SOURCE: THE GUARDIAN
 
Wana jf nisaidieni, kwenye nec kuna watu waliopo serikrini. Kwenye ccm kuna watu wliopo serikarini. Bungeni kuna watu waliopo serikarini. Sasa vikao vya juu magamba wanapo sema wataishauri serikari ipunguze bei ya mafuta ya taa na kusolve tatizo la umeme, je hao walioamua hayo, je,baadhi yao si ndo hao hao wamo humo humo serikarini? Wakiwa huku wanaamua hivi na wakiwa kule wanaamua vile. Je si ndio wale wale kwenye serikari ile ile? Sasa wataishauri serikari ipi? Au wakati hayo yanaamriwa na wananchi wanalalamika masikio yao na macho yao yalikuwa yameziba?

Kweli Mkuu; usanii wa hawa jamaa unachekesha. Yaani Serikali (ya CCM) ilipeleka hoja Bungeni ==> wabunge (wa CCM kwa wingi wao) wakapitisha kwa NDIYOOOOOOOOOO ==> CC (ya CCM) inaitaka serikali (ya CCM) ipunguze bei. Then kama serikali (ya CCM) ikikubali itabidi tena ipeleke hoja Bungeni then wabunge (wa CCM) wataitikia tena NDIOOOOOOOO na bei ya mafuta itakuwa imepungua. Hii loop nashindwa kuielewa.

Lakini si ajabu CCM wanafanya hivyo strategically ili kutafuta UMAARUFU kwamba Serikali na Bunge walipitisha jambo ambalo halina maslahi kwa mnyonge lakini Chama kikaingilia kati. Si mnaona? CCM oyeeeeeeeeeeeeeee! Na usishangae, hawatakosa wajinga wawili watatu kwa mbinu hii ya kizamani.
 
<p style="text-align: center;"><span style="font-family: Times New Roman">TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI</span></p> <span style="font-family: Times New Roman">Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM imemaliza kikao chake cha siku moja usiku wa tarehe 31/07/2011 mjini Dodoma chini ya uenyekiti wa Mwenyekiti wa CCM Taifa, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.</span> <span style="font-family: Times New Roman">Pamoja na mambo mengine Kamati Kuu imeamua yafuatayo;</span> <span style="font-family: Times New Roman"><br />
<br />
1. Imefanya uteuzi wa makatibu ishirini na saba (27) kujaza nafasi zilizokuwa wazi katika wilaya hizo. (majina na wilaya zao yameambatanishwa). Pamoja na uteuzi huo, Kamati Kuu imetengua uteuzi wa Makatibu wa Wilaya watatu (3) katika kuboresha ufanisi wa kazi katika wilaya hizo.(majina na wilaya zao yameambatanishwa).</span> <br />
<br />
<span style="font-family: Times New Roman">2. Kamati Kuu imepokea na kuridhia taarifa ya kujiuzulu kwa aliyekuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kuwakilisha Mkoa wa Tabora, Ndugu Rostam Aziz. Aidha imempongeza kwa uamuzi huo uliozingatia maslahi mapana ya chama chake. </span> <span style="font-family: Times New Roman"><br />
<br />
3. Kamati Kuu imepokea pia taarifa ya kujiuzulu kwa aliyekuwa Mbunge wa Igunga, Ndugu Rostam Aziz na kuagiza chama kupanga ratiba ya mchakato wa kumpata mgombea ubunge wa Jimbo la Igunga itakayozingatia ratiba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi juu ya uteuzi wa mgombea.</span> <span style="font-family: Times New Roman">Aidha Kamati Kuu imeagiza shughuli zote za kampeni kutafanywa na CCM Mkoa, Wilaya na ngazi zote za chama wilayani Igunga. CCM Taifa watashiriki kuongeza nguvu. Chama kinatoa wito kwa wana CCM, wapenzi na wakereketwa wa chama chetu kushiriki kwa pamoja kuhakikisha jimbo linabaki kwa CCM.</span> <br />
<br />
<span style="font-family: Times New Roman">4. Kamati Kuu haijaridhishwa na kiwango cha bei ya mafuta ya taa nchini kwa kuwa ndio nishati inayotumiwa na wananchi wengi wenye kipato cha chini. Aidha Kamati Kuu haikuridhishwa na maelezo ya kupandishwa kwa bei ya mafuta hayo kwa kisingizo cha kuzuia uchakachuaji wa mafuta mengine. </span> <span style="font-family: Times New Roman">Hivyo basi, Kamati Kuu imeiagiza Serikali kutafuta njia za kushusha bei ya mafuta ya taa na kuvitaka vyombo vya Serikali vinavyohusika na usimamiaji wa ubora wa mafuta, vihakikishe vinatimiza wajibu wake kuzuia kabisa mtindo wa uchakachuaji wa mafuta nchini na si kupandisha bei ya mafuta ya taa kama suluhisho.</span> <span style="font-family: Times New Roman"><br />
<br />
5. Kamati Kuu inasikitishwa na tatizo la umeme nchini kwani athari zake kwa uchumi wa Taifa na mtu mmoja mmoja ni kubwa. Hivyo basi imeitaka Serikali kutumia muda iliyopewa wa kurekebisha Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kuja na mpango wa dharura wa kunusuru hali hii na kisha kulimaliza kabisa tatizo la umeme nchini. <br />
<br />
</span> <span style="font-family: Times New Roman">6. Aidha Kamati Kuu imejadili masuala mengine kama; migogoro ya ardhi, tatizo la bei ya pamba, tatizo la uuzaji wa mahindi, migogoro migodini, masuala yanayohusu kero za Muungano na kuagiza Serikali kuyashughulikia kwani yanatatulika.</span> <br />
<br />
<span style="font-family: Times New Roman">7. Kamati Kuu imeipongeza Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa kwa kazi nzuri ya kutekeleza maamuzi ya NEC na kuitaka iongeze kasi katika utekelezaji huo, ili kuhakikisha mageuzi yaliyokusudiwa yanatekelezwa kwa wakati. Aidha imejadili na kupitisha miundo mipya ya Idara ya Itikadi na Uenezi na Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa.</span> <span style="font-family: Times New Roman"><br />
<br />
8. Kuhusu suala la maadili ndani ya Chama, Chama kinaendelea kusimamia maadili, na kuwataka wale waliotakiwa kujipima na kuwajibika watumie muda huo, kujipima na kuwajibika kwa masilahi mapana ya chama.</span> <span style="font-family: Times New Roman">Aidha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa inatarajiwa kukutana wakati wowote mwezi Septemba, ambapo pamoja na mambo mengine itatathimini utekelezaji wa maamuzi yake. </span> <span style="font-family: Times New Roman">Imetolewa na:-</span> <p style="text-align: center;"><span style="font-family: Times New Roman"><br />
<br />
Nape M. Nnauye (MNEC)</span><br />
</p> <p style="text-align: center;"><b><span style="font-family: Times New Roman">KATIBU WA NEC, ITIKADI NA UENEZI</span></b><br />
</p> <p style="text-align: center;"><span style="font-family: Times New Roman"><b>DODOMA</b></span><br />
</p> <p style="text-align: center;"><span style="font-family: Times New Roman">1/8/2011</span><br />
</p>
<br />
<br />
acheni kuendekeza upumbavu, kama mtu kavunja kanuni na taratibu za chama kwanini mpaka ajipime? Fukuza kama mbwa, weka jinga nyingine muone kama atafaa. CCM wamebaki hao hakuna mwingine.
 
Back
Top Bottom