Tamko la Kamati Kuu ya CCM; Muda waongezwa kujivua gamba

shame! shame! shame! huyu dogo ndo anamalizia kuweka msumari wa mwisho kwenye jeneza, let me remind u one song. Baba kawasaki alinikanya, hapa mjini nenda polepole utavamia..... ila topic ni magamba sio mapenzi tena, what remains is Magamba HISTORY, omba uhai ushuhudie and prove me wrong.
 
Duh! Gamba limewaganda! Na bado, wataongeza muda mpaka 2015!
Hilo la mafuta ya taa si liliungwa mkono kwa 100% na wataalamu wa kugonga meza? Imekuwaje tena?
 
C'moon guyz let'sbe serious, did any of you expected anything more than that from CCM?????? Taarifa nzima ni vague statements with no specifics and someone tells me hii ndiyo CCM mpya? , CCM mpya my foot!!
 
Naomba comments za watu wafuatao;
1. Nnauye jr
2. Faiza Foxy
3. Jenifa
4. Mzee wa hoja
5. W. J. Malecela
6. Omr
7. Mr Mak
8. Muhadhir
9. Rejao
10. Nduka

Ahsanteni sana...
Siku hizi @NYC credibility yake imeshuka sana imefikia watu wanamuweka group moja na kina Rejao.
 
Bei ya mafuta ya taa wamepitisha bungeni waliposema ndiyooooo.sasa iweje waibane serikali wakati wanajua waliokosea ni wao.at least wameanza kusoma alama za nyakati.
<font size="4"><span style="font-family: book antiqua">Ni usanii wa hali ya juu!!!! Tangu bajeti ilipotangazwa kakaa kimya kuhusu kupanda kwa bei ya mafuta ya taa mpaka kwenye kikao cha CC!!! Ili kutaka kuonyesha kwamba Magamba inawajali Watanzania!!!! Ni kichekesho cha hali ya juu.</span></font>
<br />
<br />
 
5. Kamati Kuu inasikitishwa na tatizo la umeme nchini kwani athari zake kwa uchumi wa Taifa na mtu mmoja mmoja ni kubwa. Hivyo basi imeitaka Serikali kutumia muda iliyopewa wa kurekebisha Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kuja na mpango wa dharura wa kunusuru hali hii na kisha kulimaliza kabisa tatizo la umeme nchini.
Hivi dual citizenship itaanza lini ....... tusijeuzwa kwa dharura tukakosa pa kukimbilia.
 
Naona Fikra za mwenye kiti wa chama zinadumu duh huyo mwenyekiti watu wa magamba wanamuabudu kama Mungu.
Inatakiwa watu wa magamba mmbadilike sasa msome alama za nyakati kwa Pumba hizo mlizo kaa kujadili sidhani kama zinaingia akilini mwa watu
 
Hii Taarifa ni uozo mtupu unavyoonyesha jinsi serikali na chama cha CCM walivyokwenye nafasi ya kujitetea ,inafurahisha kwamba wanacheza ngoma ya chadema,sijawahi kuona kwamba serikali inayoandaa mipango,inatayarisha bajeti,inawatendaji,lakini serikali na CC yake nao wanalalamika kama sisi,Hivi huko CCM wamebaki madondocha matupu hawana mtu atakayewainua kila kukicha wanazidi kuzama kila siku,manake hilo tamko ni zaidi ya usanii

Pili CC na serikali ya CCM kwa Maamuzi hayo wanatuthibitishia kwamba hawana utatuzi wa jambo lolote kwa sasa,CC gani ambayo haijaongelea hali halisi ya njaa iliyoxuka kwenye wilaya nyingi jamani hawa wanalowanalolikua kweli au ndio kuchanganyikiwa baada ya magamba kukataa kuchubuka
CC na serukali yake inatuthibitishia kwamba Bajeti iliyopitishwa ni batili ha ha ha wote tuseme bye bye CCM
 
4. Kamati Kuu haijaridhishwa na kiwango cha bei ya mafuta ya taa nchini kwa kuwa ndio nishati inayotumiwa na wananchi wengi wenye kipato cha chini. Aidha Kamati Kuu haikuridhishwa na maelezo ya kupandishwakwa bei ya mafuta hayo kwa kisingizo cha kuzuia uchakachuaji wa mafuta mengine.

Hivyo basi, Kamati Kuu imeiagiza Serikali kutafuta njia za kushusha bei ya mafuta ya taa na kuvitaka vyombo vya Serikali vinavyohusika na usimamiaji wa ubora wa mafuta, vihakikishe vinatimiza wajibu wake kuzuia kabisa mtindo wa uchakachuaji wa mafuta nchini na si kupandisha beiya mafuta ya taa kama suluhisho.

Kweli haya sasa ni maigizo, Mhe. amepitisha bajeti na kukubali bei ya mafuta ya taa ipande akiwa kama mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri, then huku akiwa kama mwenyekiti wa CC anasema hapana bei ya afuta ya taa ishushe tena anaiamuru serikali hiyo hiyo anayoongoza yeye!![/QUOTE]

Rais wa TZ;Kanali Dr Mrisho Jakaya Kikwete huwa ananishangaza sana;ni nani aliye mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri ambaye ndiyo mwenye kauli ya mwisho kuhusu Bajeti ya Serikali?Sasa kama BOSS analalamika sisi hoe hae tufanyeje/Nchi imemshinda na ushahidi ni huu wa leo!
 
kwa maneno mengine cc nddio baraza la mawaziri.............kazi ipo......
 
Kamati haijaridhishwa.
Kamati inasikitishwa.
Kamati imejadili.
Kamati imeona.
Kamati imependekeza.
Kamati imeridhia.
Kamati imepongeza.
TUNGOJE.
 
Aibu tupu...... Wanajamvi hembu nijuzeni Ni wajumbe wangapi au ni akina nani ni Wajumbe wa CC ya CCM na pia ni Mawaziri ktk Serikali hii ya Sasa?
 
4. Kamati Kuu haijaridhishwa na kiwango cha bei ya mafuta ya taa nchini kwa kuwa ndio nishati inayotumiwa na wananchi wengi wenye kipato cha chini. Aidha Kamati Kuu haikuridhishwa na maelezo ya kupandishwa kwa bei ya mafuta hayo kwa kisingizo cha kuzuia uchakachuaji wa mafuta mengine. Hivyo basi, Kamati Kuu imeiagiza Serikali kutafuta njia za kushusha bei ya mafuta ya taa na kuvitaka vyombo vya Serikali vinavyohusika na usimamiaji wa ubora wa mafuta, vihakikishe vinatimiza wajibu wake kuzuia kabisa mtindo wa uchakachuaji wa mafuta nchini na si kupandisha bei ya mafuta ya taa kama suluhisho.

5. Kamati Kuu inasikitishwa na tatizo la umeme nchini kwani athari zake kwa uchumi wa Taifa na mtu mmoja mmoja ni kubwa. Hivyo basi imeitaka Serikali kutumia muda iliyopewa wa kurekebisha Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kuja na mpango wa dharura wa kunusuru hali hii na kisha kulimaliza kabisa tatizo la umeme nchini.

Haya yananifanya nihoji uhalali wa ccm kuendelea kutawala nchi hii. Inaingiaje akilini hao hao wenye sera na mashine za kuingoza nchi wanaandaa miswada kuiwakilisha bungeni na kuipitisha halafu wanarudi nyuma kwenye vikao vyao na kusema kuwa hawakubaliani nayo?

Mwenyekiti wa ccm, nec na hiyo wanayoiita cc, ndio pia mwenyekiti wa baraza la mawaziri, ambaye kimsingi lazima wakubaliane na yote kabla ya kufikishwa bungeni.

Sasa, hapa najiuliza mwenyekiti wa ccm anamwagiza tena rais na kiongozi wa serikali kuyaangalia haya!

Basi, ni bora mngeleta hoja ya kumnyanganya mwenyekiti wa ccm taifa nafasi ya yeye kuwa mwenyekiti wa chama ili aweze kuwajibika 1X1 kwa chama. Vinginevyo huu unakuwa ni upimbi!
 
Naomba comments za watu wafuatao;
1. Nnauye jr
2. Faiza Foxy
3. Jenifa
4. Mzee wa hoja
5. W. J. Malecela
6. Omr
7. Mr Mak
8. Muhadhir
9. Rejao
10. Nduka

Ahsanteni sana...
Hapo kwenye Black, huyo kwisha habari yake hana lolote. hapo kwenye red hao wameshakula ban ni washenzi sana, na kwenye blue huyo ndio umsahau kabisa maana ana gari mpya Nissan yeye sasa hivi kazi yake ni misele tu kwenye mitaa ya New York, USA.
Huyo namba 9 ni kama katoon huwa hata hajui kama yupo facebook au yupo JF, huyo namba 10 kuondoka kwa Makamba kwenye secretarit kumemuathiri sana maana hayupo kwenye payroll ya Nape. sasa hivi anafanya propaganda kwa kinyongo
 
Kikwete anaogopa kivuri chake, anakikwepa na kukikimbia. HANA MAAMUZI MAGUMU, hana ubavu wa kutamka chochote kwa Lowassa, anaogopa akimwaga ugali, Lowassa atamwaga mboga. Dawa ni 2015 ni kuitupa mbali sana CCM.
 
aaaaaaaaaaaaaaagh! Kikwete na akina Mkulo wake wakapanga bajeti ya nchi kule Ikulu,kina Chiligati na kina Lukuvi wakaipitisha kwa makofi manene na ndiyo kubwa kule mjengoni,kina Lissu na kina Wenje wakaipinga na kusema itaumiza wa TZ (wa hali ya chini na ya kati ambao ni 95%) nao wakaitwa wachochezi na wleta fujo bungeni, Tena leo kina Nape,Mukama,Kikwete,Chiligati na vilaza wenzao wanakuja na kuropoka eti bei ya mafuta ya taa na tatizo la umeme vinauma watanzania serikari irekebishe!........................................ivi mshatuona wa TZ ni vilaza saaaaaaaana wa kudanganywa kama mazezeta eeenh! 2015 sasa ndo mtatuona kuwa sisi ni mazezeta au tuna akili timamu. Nawashauri wapinzani wajipange vizuri ili tuwape nchi ili mazishi ya CCM yawe ya amani.
 
Back
Top Bottom