Hao nao si walizungumza kwa mitazamo yao?mbona hata sisi humu JF tumekisema vibaya CCJ kwa mitazamo yetu?hivi Chiligati,Msekwa kuzungumza hivyo ndio kukihujumu CCJ?jamani hawa walijisemea kama watanzania wengine ambao hatukuwa na imani na CCJ mimi nikiwa mmoja wapo..Hebu tupeni exactly walichokizungumza hasa..Na mwelekeo wao nini?
GS ninavyofahamu maneno anayoongea Msekwa, ambaye ni makamu mwenyekiti wa CCM na spika mstaafu, hayawezi kuwa na uzito sawa na unayoongea wewe humu ndani ya JF. Msekwa na Chiligati ni viongozi wa juu sana wa chama tawala na wanachosema wao kinachukuliwa kama ni maagizo na watendaji wa serikali akiwemo Tendwa na mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi.