Tamko la CCJ dhidi ya Kauli za Tendwa juu ya Usajili wa kudumu

Ukurasa wa Pili.
Wamezungumzia uwezo wa Msajili kuwa Hana uwezo wa kukataa kusajili kiholela.
Wamenukuu Ibara ya 10 ya Sheria ya Vyama vya Siasa ya 1992, inayotamka kuwepo kwa Msajili wa Vyama vya Siasa ambapo Ibara ya 8(5) inamlazimisha Msajili lazima atoe usajili wa kudumu kwa kila chama cha siasa kilichotimiza masharti ya usajili na kuaninisha vizuizi vinavyoweza kupelekea chama kunyimwa usajili wa kudumu, lakini kipengele cha ofisi ya Msajili kukosa bajeti hakipo kwenye vizuizi, hivyo siyo kizuizi, hayo ni matatizo ya ofisi yake.

Pia wameshutumu tamko la Msajili ati ana shughuli nyingine, wamesisitiza kazi kuu ya Msajili ni kusajili, mengine yote yatafuata.

Hicho kipengele kimenivutia sana. Hivi Kwani Msajili wa Vyama vya Siasa ana kazi nyingine zaidi ya kufanya usajili na kuhakikisha hivyo vyama vya siasa vinafuata taratibu na kanuni zinazoongoza vyama vya siasa?

Hoja za CCJ zimenivutia, naona wanaweza kumbana kwenye angle mbaya na akashindwa kuchomoka, ngoja tusubiri majibu yake.

Maana huu uhuni wa CCM kwa kushirikiana na NEC na Tendwa, sometimes unasikitisha sana.
 
Mimi nafikiri baada ya kutoa tamko wangeelekea mahakamani kuomba ufafanuzi wa kisheria kwa nini wasisajiliwe wakati tayari wametimiza masharti kwa mujibu wa sheria. Ikiwezekana hata kuomba kusimamisha uchaguzi mkuu ujao.
 
Ukurasa wa Tatu.
Wametoa mapendekezo 2.
Kwanza. Ofisi ya Msajili isahihishe kauli yake kwa waandishi wa habari na kuanza mara moja kutimiza wajibu wake kwa kuhakiki CCJ na kuwapatia usajili wa kuduma mara moja ili waweke viongozi wa kudumu na kujiandaa kwa uchaguzi.
Pili. Kama Ofosi ya Msajili ni kweli haina pesa, wasema wanahitaji kiasi gani, CCJ iwachangishe wafuasi wake, waikopeshe serikali, impatie Msajili ili aihakiki CCJ na kuipatia aisajili wa kudumu. Deni hilo litalipwa na riba kwenye bajeti ya mwaka ujao wa fedha. Wameomba wajulishwe mara moja ili walete hizo pesa.
 
Pasco na MMKJ nafurahi kuona mnavyojitahidi kuwafanya watu waone Ccj ni mkombozi, ni kama vile namona Pasco alivyokaa akisubiria hilo tamko. Jamani tumeona na kusikia matamko mangapi we need physical action now na si blaa blaa, leo Ccj wakimaliza tamko lao kesho Tendwa anatoa tamko lake keshokutwa Ccj watakuja na tamko kali maradufu baadaye Tendwa atawapuuza na sinema itakuwa imefika tamati. Mwisho Ccj kwa kujitetea watasema mnaona wasingenishika shati ningemgaragaza, ngumi za utotoni hizo.

Kula tano....Naunga mkono hoja...
 
Ukurasa wa Nne.
Wametoa uthibitisho wa matamko matatu ya Tendwa aliyonukuliwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari na matamko matatu ya viongozi wa juu wa CCM kama ushahidi wa jinsi CCJ inavyohujumiwa.
 
Matamko Matatu ya Tendwa kuihujumu CCJ.
1. 22/01/2010-Tanzania Daima-" CCJ haitaweza kushiriki uchaguzi mkuu...Haiwezekani". By then CCJ hata hakijaomba usajili wa muda.
2.03/03/2010-Jambo Leo "Kupata usajili wa muda ni ndoto za kufika uchaguzi mkuu, kama wana ndoto za aina hiyo, wanapoteza muda"
3.03/03/2010-Nipashe amenukuliwa akiiambia ITV kuwa atafanya uchunguzi wa kina kama ni kweli CCJ kilianzishwa miaka 2 iliyopita na ikibainika, atakifuta mara moja.
 
Matamko 3 ya CCM kuihujumu CCJ.
1. 30/01/2010-Tanzania Daima. " Watakaokwenda CCJ, wamepotea kama boti iliyotoboka!, hakiwezi kusajiliwa" -John Chiligati, Katibu
Mwenyezi CCM.
2. 02/02/2010-Changamoto. "Watakaojiunga na CCJ watakiona, kwanza wanajidanganya na kwanini wahangaikie chama ambacho hakitapata
usajili kabla ya uchaguzi mkuu?"-Pius Mswekwa, M/M/Kiti, CCM.
3. 01/02/2010-Nipashe, " CCJ inatumika kama njama za kujenga chuki kwa wananchi dhidi ya ya CCM"- Pius Msekwa.
 
Hitimisho.
CCJ imesema kucheleweshwa kwa makusudi kupatiwa usajili wa kudumu, ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binaadamu, hasa haki za kiraia, hivyo kinatafakari huku kikishauriana na wanachamaa na Watanzania kwa ujumla juu ya hatua za kuchukua ili kuhakikisha haki inapatikana kwa mujibu wa sheria na katiba.

NB. Kama niliover hear, wanaende mahakamani.
Kisheria wanatakiwa kuomba kwa hati ya dharura kitu kinachoitwa 'Certiorari Mandamus' ambayo ni hati inayotolewa na mahakama kuu kuilazimisha serikali itimize wajibu wake.
 
, vyama vyote 18 vya upinzani vimeshindwa kufanya kinachotakiwa. .

Haya maneno ni aibu kubwa sana kutamkwa na wewe hasa unapoyasema hadharani namna hii utakuja kulamba matapishi siku moja, wewe endelea kumwona mwanakijiji kuwa kila analosupport ni sahihi tu . Nakumbuka usemi wa mwalimu wangu mmoja pale boarding school aliyekuwa anasema " angalieni sana kila mtu hapa alikuja na begi lake hapa" naona wewe hilo ujalitambua.

Pasco umenifadhahisha sana.
 
Matamko Matatu ya Tendwa kuihujumu CCJ.
1. 22/01/2010-Tanzania Daima-" CCJ haitaweza kushiriki uchaguzi mkuu...Haiwezekani". By then CCJ hata hakijaomba usajili wa muda.
2.03/03/2010-Jambo Leo "Kupata usajili wa muda ni ndoto za kufika uchaguzi mkuu, kama wana ndoto za aina hiyo, wanapoteza muda"
3.03/03/2010-Nipashe amenukuliwa akiiambia ITV kuwa atafanya uchunguzi wa kina kama ni kweli CCJ kilianzishwa miaka 2 iliyopita na ikibainika, atakifuta mara moja.
Jamani sasa hili ni tamko au nukuu ya magazeti?je hayo magzeti yalimnukuhu sahihi Tendwa?Hili ndio tamko kali?
 
Matamko 3 ya CCM kuihujumu CCJ.
1. 30/01/2010-Tanzania Daima. " Watakaokwenda CCJ, wamepotea kama boti iliyotoboka!, hakiwezi kusajiliwa" -John Chiligati, Katibu
Mwenyezi CCM.
2. 02/02/2010-Changamoto. "Watakaojiunga na CCJ watakiona, kwanza wanajidanganya na kwanini wahangaikie chama ambacho hakitapata
usajili kabla ya uchaguzi mkuu?"-Pius Mswekwa, M/M/Kiti, CCM.
3. 01/02/2010-Nipashe, " CCJ inatumika kama njama za kujenga chuki kwa wananchi dhidi ya ya CCM"- Pius Msekwa.

Hao nao si walizungumza kwa mitazamo yao?mbona hata sisi humu JF tumekisema vibaya CCJ kwa mitazamo yetu?hivi Chiligati,Msekwa kuzungumza hivyo ndio kukihujumu CCJ?jamani hawa walijisemea kama watanzania wengine ambao hatukuwa na imani na CCJ mimi nikiwa mmoja wapo..Hebu tupeni exactly walichokizungumza hasa..Na mwelekeo wao nini?
 
Katika majibu hayo yenye kurasa nne ambayo nimeheshimiwa kuona CCJ inatundika ushahidi wa kimazingira wa jinsi gani uongozi wa juu wa CCM ndio wamefanya uamuzi wa kuzuia CCJ isipate usajili wa kudumu ili isiweze kushiriki uchaguzi mkuu. ..Habari ndiyo hiyo...
Mzee Mwanakijiji, nimebahatika kuhudhuria hii press conference, kwa vile wewe umeheshimiwa kuona CCJ inatundika ushahidi wa kimazingira, jinsi uongozi wa juu wa CCM wamefanya uamuzi wa kuizuia CCJ isipate usajili wa kudumu. Kwa vile nimetoa kidogo tongotongo kwenye sheria, kwa ushahidi huo waliouandika, kwa mujibu wa Law of Evidence, hapo hakuna kitu!, hakuna ushahidi, ni nil!. Unless CCJ wana sensetive data za vikao vya ndani vya CCM vilivyofanya maamuzi hayo kuzuia CCJ isisajiliwe, na maamuzi yenyewe yakapelekwa kwa Tendwa kwa utekelezaji, hizo nukuu zote zinaishia kuwa ni matamko binafsi ya hao WaCCM.
 
Hitimisho.
CCJ imesema kucheleweshwa kwa makusudi kupatiwa usajili wa kudumu, ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binaadamu, hasa haki za kiraia, hivyo kinatafakari huku kikishauriana na wanachamaa na Watanzania kwa ujumla juu ya hatua za kuchukua ili kuhakikisha haki inapatikana kwa mujibu wa sheria na katiba.

NB. Kama niliover hear, wanaende mahakamani.
Kisheria wanatakiwa kuomba kwa hati ya dharura kitu kinachoitwa 'Certiorari Mandamus' ambayo ni hati inayotolewa na mahakama kuu kuilazimisha serikali itimize wajibu wake.


Waaa,yale yale hakuna jipya ni blah blah kama wengine tu..Kuliko kwenda mahakamani bora wafanya maandamano ya nguvu au waende kwa wananchi..Kama Tendwa kawanyima je Serikali na mahakama wanaweza kuwatenganisha?
 
hahahah hii inanikumbusha ule msemo usemao, " Amlipae mpiga zumali ndie huchagua wimbo".. tendwa si analipwa na serikali ya CCM!
 
Haya maneno ni aibu kubwa sana kutamkwa na wewe hasa unapoyasema hadharani namna hii utakuja kulamba matapishi siku moja, wewe endelea kumwona mwanakijiji kuwa kila analosupport ni sahihi tu . Nakumbuka usemi wa mwalimu wangu mmoja pale boarding school aliyekuwa anasema " angalieni sana kila mtu hapa alikuja na begi lake hapa" naona wewe hilo ujalitambua.

Pasco umenifadhahisha sana.
Shalom, naomba unisome kwa makini in between the lines, mimi ni mimi na Mwanakijiji ni Mwanakijiji, japo nakubaliana nae kwenye mambo ya msingi, natofautiana naye sana kwenye aproach, namuona kama more idealist than realist fighting by strategic fighting technics from a distance wakati mimi ni realist niko kwenye battle field on the war zone.

Kuhusu CCJ, hebu tembelea ile thread ya https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/61539-ccj-kuanza-charm-offensive-ask-your-questions.html uone jinsi nimetofautiana na Mwanakijiji.
 
Pasco na MMKJ nafurahi kuona mnavyojitahidi kuwafanya watu waone Ccj ni mkombozi, ni kama vile namona Pasco alivyokaa akisubiria hilo tamko. Jamani tumeona na kusikia matamko mangapi we need physical action now na si blaa blaa, leo Ccj wakimaliza tamko lao kesho Tendwa anatoa tamko lake keshokutwa Ccj watakuja na tamko kali maradufu baadaye Tendwa atawapuuza na sinema itakuwa imefika tamati. Mwisho Ccj kwa kujitetea watasema mnaona wasingenishika shati ningemgaragaza, ngumi za utotoni hizo.

Mkuu Luteni, labda utoe mfano ni physical actions gani ambazo ungependa kuziona. Kumbuka kwamba wanachokitafuta CCJ ni kuingia kundini ndipo waweze kuonyesha makucha yao kisawasawa na bila shaka hizo physical actions unazoziwaza utaziona tu.

Mkuu Pasco, asante kwa kutupa yaliyojiri. Hata kama unatofautiana na MMKJ hapa na pale la muhimu kuwa na lengo moja la kutaka kulikwamua taifa kutoka kwenye tope.
 
Zaidi zile kurasa 4 za tamko kali la CCJ, pia walitoa kurasa moja iliyandikwa Nyongeza nayo ilikuwa na hadithi ya Mhalifu na Mfalme.
Hadithi ...hadithi...
 
Shalom, naomba unisome kwa makini in between the lines, mimi ni mimi na Mwanakijiji ni Mwanakijiji, japo nakubaliana nae kwenye mambo ya msingi, natofautiana naye sana kwenye aproach, namuona kama more idealist than realist fighting by strategic fighting technics from a distance wakati mimi ni realist niko kwenye battle field on the war zone.

Kuhusu CCJ, hebu tembelea ile thread ya https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/61539-ccj-kuanza-charm-offensive-ask-your-questions.html uone jinsi nimetofautiana na Mwanakijiji.

wewe futa usemi wako hapo juu zaidi hakuna. Kuna vyama vya upinzani ambavyo vimethubutu vingi tu sawa?
 
Back
Top Bottom