Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,498
- 9,279
OFISI ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), imewataka walimu kujiepusha kuweka rehani kadi zao za benki(ATM), wanapokopa mikopo kwenye Taasisi za Fedha.
Aidha, imeagiza kuchukuliwa hatua za kinidhamu ikiwamo kufukuzwa kazi mwalimu yeyote atakayebainika mlevi na mtoro kazini.
Naibu Katibu, Mkuu wa Ofisi hiyo, anayeshughulikia Elimu, Gerald Mweli ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumza na walimu na watumishi wa Shule ya Sekondari Ilboru, jijini hapa Arusha.
Alisema kuna taarifa za walimu wanapokopa wanaacha ATM zao.
“Mara nyingi nilikuwa nikitembea kwenye Halmashauri nasikia kuna tatizo la walimu wanakopa hadi wanaacha ATM kadi, najua hapa hawapo, eti kuna wale wa kuacha ATM kadi hapa?, tukisema tuweke mezani zipo?,”alihoji.
Aliongeza “Nashukuru nilipofika hapa Ilboru nimeambiwa walimu wote wana ATM sio kama wale wa maeneo mengine kule wanapokopa, niwapongeze sana.”
Chanzo: IPP Media
Aidha, imeagiza kuchukuliwa hatua za kinidhamu ikiwamo kufukuzwa kazi mwalimu yeyote atakayebainika mlevi na mtoro kazini.
Naibu Katibu, Mkuu wa Ofisi hiyo, anayeshughulikia Elimu, Gerald Mweli ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumza na walimu na watumishi wa Shule ya Sekondari Ilboru, jijini hapa Arusha.
Alisema kuna taarifa za walimu wanapokopa wanaacha ATM zao.
“Mara nyingi nilikuwa nikitembea kwenye Halmashauri nasikia kuna tatizo la walimu wanakopa hadi wanaacha ATM kadi, najua hapa hawapo, eti kuna wale wa kuacha ATM kadi hapa?, tukisema tuweke mezani zipo?,”alihoji.
Aliongeza “Nashukuru nilipofika hapa Ilboru nimeambiwa walimu wote wana ATM sio kama wale wa maeneo mengine kule wanapokopa, niwapongeze sana.”
Chanzo: IPP Media