Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,010
- 9,875
Serikali yaanika sababu kasoro majina kwenye ajira za walimu
SERIKALI imeeleza sababu zilizochangia kuwapo kwa kasoro mbalimbali kwenye majina ya ajira za walimu 13,000 zilizowekwa kwenye tovuti hivi karibu.
Hali hiyo ilizua mjadala na maswali mengi katika mitandao ya kijamii, huku ikibainisha hatua zilizochukulia na zikazochukuliwa kuanzia jana.
Ufafanuzi huo ulitolewa jana na makatibu wakuu watatu kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhandisi Joseph Nyamhanaga, Katibu Mkuu Utumishi, Dk. Laurean Ndumbaro na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk. Leonard Akwilapo.
Mhandisi Nyamhanga alisema kuwa kutokana na kuwapo kwa maswali mengi katika mitandao ya kijamii kuhusu majina ya walimu waliopata ajira za ualimu, wameshazifanyika kazi baadhi ya dosari.
Alisema maswali ambayo yalikuwa yakihojiwa ni mwalimu mmoja jina lake kujitokeza zaidi ya mara 196, hivyo kuibua mjadala.
“Hili tayari tumeshalifanyia kazi na hii ilitokana na tulivyokuwa tukiandaa orodha hii ili kupandisha kwenye tovuti… kuna tatizo la kiufundi lilitokea, lakini hali hii siyo kama imeathiri lolote au mwalimu huyo kuchukua nafasi za wengine 195, tumeshalifanyika kazi tumeona leo tuwaite ili kuwaeleza suala hili namna ambavyo tumelitatua,” alisema Nyamhanga.
Aidha, alisema dosari nyingine mbayo ilikuwa ikilalamikiwa ni majina ya baadhi ya watu waliopata ajira kuonekana ni wahitimu wa kidato cha nne mwaka jana.
“Tayari tumefanya uhakiki kubaini kuwa hii ilitokana na waombaji kukosea kuandika taarifa zao, wengi wao waliandika miaka waliyomaliza kidato cha nne na mwaka waliopata shahada yao basi… lakini ukweli ni kwamba hakuna mhitimu wa mwaka 2019, 2018 wala 2017 aliyechaguliwa kwenye ajira hizi,” alifafanua Nyamhanga.
Alisema kwa mujibu wa vielelezo walivyovipitia, kwa waliochaguliwa kupata nafasi hizo ualimu wengi wao ni wahitimu wa kidato cha nne kuanzia mwaka 2010 hadi 2014.
Vile vile, Katibu Mkuu huyo alisema wanaendelea na uhakiki wa majina yote ili kujiridhisha kama ni watu wanaostahili na kuondoa dosali zote.
“Uhakiki huu utaanza leo (jana) na tunatarajia ukamilike ndani ya siku mbili ili watakaostahili waripoti katika maeneo yao na kupatiwa stahiki zao kama ambavyo taarifa ya awali ilivyokuwa inabainisha,” alieleza.
Katibu Mkuu Utumishi, Dk. Laurean Ndumbaro, alisema wao ndio wenye mamlaka ya kutoa vibali vya ajira na katika mwaka huu wa fedha, jumla ya walimu 13,000 watapatiwa ajira.
Alisema katika ajira hizo 13,000, walimu 8,000 ndiyo ambao majina yao yametolewa kwenye mtandao na wengine 5,000 watatangazwa baadaye.
Akizungumza kuhusu uhakiki, Dk. Ndumbaro alisema walimu ambao watabainika kuwa wamepata nafasi hizo kwa udanganyifu wataondolewa, na nafasi zao kupatiwa mtu mwingine mwenye sifa.
“Mfumo huu uliotumika kuomba ajira kuna baadhi ya walimu ambao walikuwa ni wa Historia, lakini wamejaza na somo la Hisabati ili mfumo uwatambue,” alisema na kuongeza:
“Sasa niseme tu kwa yeyote atakayebainika amepata ajira kwa somo ambalo hajalisomea, ataondolea na kumzuia asipate tena ajira serikalini.”
Chanzo: NIPASHE
SERIKALI imeeleza sababu zilizochangia kuwapo kwa kasoro mbalimbali kwenye majina ya ajira za walimu 13,000 zilizowekwa kwenye tovuti hivi karibu.
Hali hiyo ilizua mjadala na maswali mengi katika mitandao ya kijamii, huku ikibainisha hatua zilizochukulia na zikazochukuliwa kuanzia jana.
Ufafanuzi huo ulitolewa jana na makatibu wakuu watatu kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhandisi Joseph Nyamhanaga, Katibu Mkuu Utumishi, Dk. Laurean Ndumbaro na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk. Leonard Akwilapo.
Mhandisi Nyamhanga alisema kuwa kutokana na kuwapo kwa maswali mengi katika mitandao ya kijamii kuhusu majina ya walimu waliopata ajira za ualimu, wameshazifanyika kazi baadhi ya dosari.
Alisema maswali ambayo yalikuwa yakihojiwa ni mwalimu mmoja jina lake kujitokeza zaidi ya mara 196, hivyo kuibua mjadala.
“Hili tayari tumeshalifanyia kazi na hii ilitokana na tulivyokuwa tukiandaa orodha hii ili kupandisha kwenye tovuti… kuna tatizo la kiufundi lilitokea, lakini hali hii siyo kama imeathiri lolote au mwalimu huyo kuchukua nafasi za wengine 195, tumeshalifanyika kazi tumeona leo tuwaite ili kuwaeleza suala hili namna ambavyo tumelitatua,” alisema Nyamhanga.
Aidha, alisema dosari nyingine mbayo ilikuwa ikilalamikiwa ni majina ya baadhi ya watu waliopata ajira kuonekana ni wahitimu wa kidato cha nne mwaka jana.
“Tayari tumefanya uhakiki kubaini kuwa hii ilitokana na waombaji kukosea kuandika taarifa zao, wengi wao waliandika miaka waliyomaliza kidato cha nne na mwaka waliopata shahada yao basi… lakini ukweli ni kwamba hakuna mhitimu wa mwaka 2019, 2018 wala 2017 aliyechaguliwa kwenye ajira hizi,” alifafanua Nyamhanga.
Alisema kwa mujibu wa vielelezo walivyovipitia, kwa waliochaguliwa kupata nafasi hizo ualimu wengi wao ni wahitimu wa kidato cha nne kuanzia mwaka 2010 hadi 2014.
Vile vile, Katibu Mkuu huyo alisema wanaendelea na uhakiki wa majina yote ili kujiridhisha kama ni watu wanaostahili na kuondoa dosali zote.
“Uhakiki huu utaanza leo (jana) na tunatarajia ukamilike ndani ya siku mbili ili watakaostahili waripoti katika maeneo yao na kupatiwa stahiki zao kama ambavyo taarifa ya awali ilivyokuwa inabainisha,” alieleza.
Katibu Mkuu Utumishi, Dk. Laurean Ndumbaro, alisema wao ndio wenye mamlaka ya kutoa vibali vya ajira na katika mwaka huu wa fedha, jumla ya walimu 13,000 watapatiwa ajira.
Alisema katika ajira hizo 13,000, walimu 8,000 ndiyo ambao majina yao yametolewa kwenye mtandao na wengine 5,000 watatangazwa baadaye.
Akizungumza kuhusu uhakiki, Dk. Ndumbaro alisema walimu ambao watabainika kuwa wamepata nafasi hizo kwa udanganyifu wataondolewa, na nafasi zao kupatiwa mtu mwingine mwenye sifa.
“Mfumo huu uliotumika kuomba ajira kuna baadhi ya walimu ambao walikuwa ni wa Historia, lakini wamejaza na somo la Hisabati ili mfumo uwatambue,” alisema na kuongeza:
“Sasa niseme tu kwa yeyote atakayebainika amepata ajira kwa somo ambalo hajalisomea, ataondolea na kumzuia asipate tena ajira serikalini.”
Chanzo: NIPASHE