TAMISEMI mnakosea sana mnapotaka kutoa ajira za walimu kwa upendeleo

msovero

JF-Expert Member
Jun 30, 2019
839
1,472
Naibu waziri-Tamisemi, mhe. David silinde akiongea na kituo kimoja cha redio huko Lindi ametoa agizo kwa walimu wakuu kuorodhesha majina ya walimu wanaojitolea kwenye shule zao ili wapatiwe kipaumbele cha ajira kila zinapotangazwa na serikali. In fact ni agizo ambalo linahitaji tafakuri ya kina kabla ya kufanyiwa utekelezaji kwa sababu,

Kutoa kipaumbele kwa walimu waliojitolea ni ubaguzi wa wazi katika utoaji wa ajira za walimu kwa sababu kitendo hicho kinachochea rushwa,undugu na kujuana.

Kwa maana kinatoa mwanya kwa wakuu wa shule na maafisa elimu kata kuchomeka watu kwa hongo au ndugu zao kwa lengo la kuwasaidia kupata ajira serikalini kwa haraka.

Secondly, walimu wanaojitolea sio kwamba wanafundisha bure bila malipo yoyote isipokuwa wanalipwa,hivyo wana uhakika wa kupata chochote kitu kila mwisho wa mwezi.

Kwahiyo malipo wanayopata ingetosha kuwa motisha kwao lakini kwenye ajira washindane kwa usawa na walimu wengine bila kupewa upendeleo.

Thirdly, kutokana na kutokuwa na uwezo wa kuwalipa, shule nyingi zinapokea walimu wachache sana kati ya mwalimu mmoja hadi watatu jambo linalopelekea walimu wengine kukosa nafasi za kujitolea japo Nia wanakuwa nayo.

Fourthly, ni ukweli usiopingika kwamba vijana wengi wanapitia kipindi kigumu cha ukali wa maisha kiasi cha mavazi waliyonunua wakiwa vyuoni kuchoka au kuchanika kabisa hivyo inawawia vigumu kwenda kujitolea kwa sababu hata viwalo vya kuvaa hawana.

Kufuatia ukweli huo, ndio maana Rais alitoa tamko vijana wote waajiriwe kwa usawa bila upendeleo kwa sababu anajua magumu wanayopitia, iweje leo tamisemi mtake kukinzana na agizo hili la mheshimiwa Rais?

Fifth, suala la kujitolea linawezekana kwa kijana anayeishi nyumbani na kuhudumiwa na wazazi wake lakini kwa kijana aliyeanza maisha ya kujitegemea na kulea familia mathalani watoto au wazazi wake ni gumu kwa kiasi chake.

Ni gumu kwa sababu nyuma yake kuna familia inamtegemea sasa akisema aache kibarua chake cha kujiegesha ili akajitolee kufundisha hamuoni kama anakuwa anaiweka familia yake rehani?

Kadhalika, kijana aliyepanga kama akienda kujitolea atalipaje kodi ya pango achilia mbali kumudu gharama za maisha?....Tamisemi kuweni na huruma toeni ajira kwa haki na usawa
 
Alieshiba hamjui mwenye njaa.Waache waendelee kuleta siasa kwenye ajira.Mtu huna hata senti ya kula.Unaposema ukapambane hata na kibarua cha kubeba zege anajitokeza mtu anakwambia ujitolee ndipo akuajiri.PATHETIC
 
Unasema wanaojitolea wanalipwa?

Kuwa mzalendo kijana kajitolee ndo upate ajira hahaha me binafsi siafiki hili swala ila kama mtu kajitolea lazima apewe kipaombele.
 
Jipende na uijue thamni yako kisha itunze thamani yako kwa gharama yoyote.

Jifunze kujua wakati gani unachezewa na wakati gani unatumika ipasavyo.

Ni kweli umesoma na unahitaji elimu yako ilete matunda, ila usisahau kuthathmini njia ambayo matunda hayo yatapatikana. Usiwe mnyonge na wa kujinyenyekeza KINAFKI ili hali unaelewa ukweli kwamba unatumiwa ndivyo sivyo.

Kuwa tayari kufuata njia ngumu kufikia malengo LAKINI ni yenye kulinda UTU wako na THAMANI yako. Tumia nguvu zako kufanya kazi ngumu pamoja na elimu yako ila upate kile ambacho MOYO wako utaridhia nacho hatakama ni kidogo ilimradi THAMANI yako na UTU wako uendelee kuutunza ipasavyo.

Usigeuke mtumwa kutumika vibaya na watu wasiojali UTU wako na hata THAMANI yako maana WAO pia wanafanya maamuzi magumu kutunza UTU wao na THAMANI zao bila kujali hatima ya wengine.

Sitoruhurusu UTU wangu na THAMANI yangu kutumiwa kisa elimu yangu au umaskini wangu.

Wengi waliofanikiwa walijifunza jinsi ya KUJISIMAMIA VEMA NA IPASAVYO.

Pambana sana katika maisha ila usitoe mwanya wa mtu kuchezea UTU wako na THAMANI yako.

Wewe ni zaidi ya unavyojiona hivyo usijichukulie poa.

Na Mr. Purpose
 
Hivi sasa hakuna mtu ye yote anayeajiriwa bila maombi yake kupitia CCM. Ili uajiriwe lazima uwe mwana CCM.

Hivyo tayari nchi hii tulishaingia katika ubaguzi wa kichama na kiitikadi. Itachukua muda kuja kijikwamua hapa tulipofikishwa na huu utawala wa CCM.
 
“Inawezekana pia kufanikiwa mpaka kuwa millionaire bila kuajiria popote toka uzaliwe” By Regent.

Ningependa walimu kama moja ya taaluma yenye maslahi finyu kuishi katika msemo huu siku moja watanishukuru.
 
Wanalipwa,kuna s/m huku wazazi/walezi tunalipa tsh 1500 kila mwezi kwa ajili ya mwalimu anayejitolea.
Kweli mzazi huoni aibu kulipa 1,500/= kwa mwezi kwa ajili ya elimu ya mtoto wako? Hivi huwa mnategemeaga nini? Mi ningekuwa mwalimu mkuu wote mngelipa 10,000/= kwa mwezi
 
Tatizo halikuanzia huko,, tatizo lilianzia pale, neno haki halikutumika, sababu walioingia madarakani ni feki na hata viongozi ni feki, hawezi kufanya kazi kwa ufasaha.
 
Serikali kama hamjui inapenda mseleleko sanaaaaa, wanataka mjitolee ili wasolve tatizo la ukosefu wa ajira indirectly. Mmesahau zile ajira 13,000 walisema hivohivo kuwa watapewa kipaumbele, vipi mbona mpk sasa tupo nao badala yake wameajiriwa wengine bila kujar alijitolea au la! Wanawajua walimu wengi ni choka mbaya alafu hawajiongezi kuwaza zaidi.

Na kama ikiwa hivo bc ngoja nitafte namba ya mjomba headmaster aniweke kwenye document la kwenda tamisemi😄😄😄
 
Kweli mzazi huoni aibu kulipa 1,500/= kwa mwezi kwa ajili ya elimu ya mtoto wako? Hivi huwa mnategemeaga nini? Mi ningekuwa mwalimu mkuu wote mngelipa 10,000/= kwa mwezi

Jaribu kutumia akili,mzazi mwenye watoto wanne na kuendelea una mzungumzia vipi? Au kwa kuwa wewe upo upande wapili unaropoka?
 
Unasema wanaojitolea wanalipwa?

Kuwa mzalendo kijana kajitolee ndo upate ajira hahaha me binafsi siafiki hili swala ila kama mtu kajitolea lazima apewe kipaombele.
Hakuna anayefundisha bila malipo wote wanalipwa.
 
Jaribu kutumia akili, mzazi mwenye watoto wanne na kuendelea una mzungumzia vipi? Au kwa kuwa wewe upo upande wapili unaropoka?
Inabidi afanye kazi kwa bidii zake zote, hii nchi ina fursa nyingi na ndio maana akaweza kuzaa watoto wanne, maana yake kaona fursa, uvivu sio kitu kizuri.
 
Back
Top Bottom