Komando tamimy
Senior Member
- Nov 18, 2020
- 108
- 121
Habari wanajukwaaa.
Mimi ni mdau wa elimu na pia wa maendeleo ya wananchi kwa nimekuwa mfatiliaji mzuri wa maswala ya ujenzi hasa kipindi hiki ambacho tamisemi kupitia Rais wetu Samia Suluhu wamezamilia wanafunzi wote watakaoanza kidato cha kwanza mwakani waripoti wote.Lakini nimegundua kuna mambo ambayo tamisemi nadhani hawakuyaweka sawa kwani baada ya kuweka fedha kwenye akaunti za halmashauri tamisemi ilitakiwa itoe miongozo ifuatayo.
1. itoe ramani ya majengo ambayo yanatakiwa kujengwa.
2. Materials ambayo yatakayotumika.
3. Wakandarasi wa Halmashauri ambao wameajiriwa na serikali wahusishwe.
4. Pesa ziwe chini ya bodi ya shule zisiwe chini ya DMO/RMO/MKUU WA SHULE/MWALIMU MKUU.
5. Tamisemi iunde Task force ya kufutilia utekelezaji wa miradi yao nawapite kila zone ambayo pesa ilipelekwa na serikali.
Ikumbukwe ujenzi ambao uko chini ya kiwango uigharimu sana serikali kwani uhitaji ukarabati wa mara kwa mara pia ikumbukwe hospitali na madarasa tunayojenga ni kwa ajili ya jamii yetu na vizazi vijavyo.
Kwanini nimeshauri hayo ni kutokana nimepita baadhi ya sehemu nimeoa yafuatayo.
Msingi wa jengo futi 1. Yaaani futi1 na wametandaza tofali jengo la serikali? Halafu linajengwa kwa tope!? Tena tofali zenyewe za kuchoma?!
Kuna sekondari ambazo zilijengwa na wakoloni mpaka leo ziko imara sasa sijui wakoloni walikuwa wazalendo kuliko sisi.?
Pia nimewaona baadhi ya wakuu wa shule/Dmo/Rmo/ wakilipa pesa bila kushirikisha bodi ya shule au vikao vya maamuzi sasa sijajua umakini wao katika mambo ya hela. Halafu itasababisha upotevu mwingi wa pesa. Kwani most of them are legalized bandits.
Kuna wengine nimeskia wabane pesa zitakazobakia watazipangia matumizi. Na hapo ndo shida kubwa ipo pia wengine wanadai badala ya kujenga madarasa ma2 wajenge ma3 sasa sijajua tamisemi imejipangaje nakumbuka nilikuwa kwenye ziara mkuu wa wilaya Songwe tukaenda shule siikumbuki tukakuta mtendaji mmoja anadai ameibiwa pesa yote ambayo ilitakiwa imalizie nyumba ya mwalimu tafsiri yake ni kwamba mtendaji huyo aliikabidhiwa pesa yote matokeo yake kaibiwa ila kama ni kweli.
Pia nikabahatika kuwa kwenye ziara ya nadhani peramiho daaaah tulioyakuta huko ni zaidi ya kilio bwalo la chakula la wanafunzi zaidi ya 700 linajengwa kwa tofali za tope hela na wakati huo pesa yote imeliwa.
Tamisemi njooo ni na mifumo na utaratibu sahihi wa kufanya kazi najua wizara ni kubwa lakini pia watendaji ni wengi.
Kuna taarifa ambazo ambazo nimepenyezewa na mmoja watu ambao ni reliable source kwamba wakuu wa shule wanatakiwa kutafuta mafundi naiona hatari na ubora hafifu wa majengo yatakayojengwa kwa sababu wengi wao watatafuta mafundi wenye kiwango cha chini.
Mimi ni mdau wa elimu na pia wa maendeleo ya wananchi kwa nimekuwa mfatiliaji mzuri wa maswala ya ujenzi hasa kipindi hiki ambacho tamisemi kupitia Rais wetu Samia Suluhu wamezamilia wanafunzi wote watakaoanza kidato cha kwanza mwakani waripoti wote.Lakini nimegundua kuna mambo ambayo tamisemi nadhani hawakuyaweka sawa kwani baada ya kuweka fedha kwenye akaunti za halmashauri tamisemi ilitakiwa itoe miongozo ifuatayo.
1. itoe ramani ya majengo ambayo yanatakiwa kujengwa.
2. Materials ambayo yatakayotumika.
3. Wakandarasi wa Halmashauri ambao wameajiriwa na serikali wahusishwe.
4. Pesa ziwe chini ya bodi ya shule zisiwe chini ya DMO/RMO/MKUU WA SHULE/MWALIMU MKUU.
5. Tamisemi iunde Task force ya kufutilia utekelezaji wa miradi yao nawapite kila zone ambayo pesa ilipelekwa na serikali.
Ikumbukwe ujenzi ambao uko chini ya kiwango uigharimu sana serikali kwani uhitaji ukarabati wa mara kwa mara pia ikumbukwe hospitali na madarasa tunayojenga ni kwa ajili ya jamii yetu na vizazi vijavyo.
Kwanini nimeshauri hayo ni kutokana nimepita baadhi ya sehemu nimeoa yafuatayo.
Msingi wa jengo futi 1. Yaaani futi1 na wametandaza tofali jengo la serikali? Halafu linajengwa kwa tope!? Tena tofali zenyewe za kuchoma?!
Kuna sekondari ambazo zilijengwa na wakoloni mpaka leo ziko imara sasa sijui wakoloni walikuwa wazalendo kuliko sisi.?
Pia nimewaona baadhi ya wakuu wa shule/Dmo/Rmo/ wakilipa pesa bila kushirikisha bodi ya shule au vikao vya maamuzi sasa sijajua umakini wao katika mambo ya hela. Halafu itasababisha upotevu mwingi wa pesa. Kwani most of them are legalized bandits.
Kuna wengine nimeskia wabane pesa zitakazobakia watazipangia matumizi. Na hapo ndo shida kubwa ipo pia wengine wanadai badala ya kujenga madarasa ma2 wajenge ma3 sasa sijajua tamisemi imejipangaje nakumbuka nilikuwa kwenye ziara mkuu wa wilaya Songwe tukaenda shule siikumbuki tukakuta mtendaji mmoja anadai ameibiwa pesa yote ambayo ilitakiwa imalizie nyumba ya mwalimu tafsiri yake ni kwamba mtendaji huyo aliikabidhiwa pesa yote matokeo yake kaibiwa ila kama ni kweli.
Pia nikabahatika kuwa kwenye ziara ya nadhani peramiho daaaah tulioyakuta huko ni zaidi ya kilio bwalo la chakula la wanafunzi zaidi ya 700 linajengwa kwa tofali za tope hela na wakati huo pesa yote imeliwa.
Tamisemi njooo ni na mifumo na utaratibu sahihi wa kufanya kazi najua wizara ni kubwa lakini pia watendaji ni wengi.
Kuna taarifa ambazo ambazo nimepenyezewa na mmoja watu ambao ni reliable source kwamba wakuu wa shule wanatakiwa kutafuta mafundi naiona hatari na ubora hafifu wa majengo yatakayojengwa kwa sababu wengi wao watatafuta mafundi wenye kiwango cha chini.