Tambua wakati mzuri wa kutafuta mwanamke wa maisha!

Dah....msijidanganye nyie....hakuna mwanamke anayependa maisha magumu....labda awe na kasoro au ameona kuna future nzuri mbeleni...
 
Habari wana jf!

Je ni wakati gani mzuri wa kutafuta mwanamke wa maisha yake kwa mwanaume?

1)je ni wakati ambao mwanaume ana maisha magumu ,hana Ajira,yani kipindi ambacho mwanaume anapambana na hali yake kutoka kwenye dimbwi la umaskini?au!

2)je ni wakati ambao mwanaume ana maisha mazuri,ana ajira nzuri,ameshatoka kwenye Dimbwi la umaskini na mwenye mafanikio ya kiuchumi?

Binafsi naona wakati mzuri wa mwanaume kutafuta mwanamke wa maisha yake,ni wakati ule mwanaume anapokuwa na maisha magumu,kwa sababu Dunia nzima hakuna mtu anaependa maisha magumu na umaskini labda awe chizi,na hapa Duniani kuna uchizi wa aina mbili tu "uchizi wa matatizo ya akili na uchizi wa mapenzi"lakini uchizi wa mapenzi ni mzuri maana huwa ni kiwango cha juu sana cha upendo, kwa mantiki hiyo ukimuona mwanamke amekubali kuishi maisha magumu na mwanaume maskini wakati kuna wanaume wenye maisha mazuri wanahitaji kuwa nae,unatakiwa ujue huyo mwanamke amechizika na mapenzi yani kwa tafsri nyingine "amependa kweli"na wahenga husema "Rafiki wa kweli ni yule akufaae kwa dhiki",ni bahati mbaya sana siku hizi wanaume wengi hutafuta wachumba pindi wanapokuwa wamefanikiwa ndio maana ndoa nyingi siku hizi hazidumu!

Hakika nawaambieni"ukweli ni vigumu kumpata mwanamke anaekupenda kweli ukiwa maskini lakini ni vigumu zaidi kumpata mwanamke anaekupenda kweli ukiwa Tajiri"sasa wewe subiri ufanikiwe ndipo utafute mchumba wa kuoa halafu uone mara ume filisika baada ya kuoa,hapo ndipo utakapojua kuwa kuna wanawake wenye Destiny ya umaskini,kwa sababu wanajua kutumia tu pesa hawajui kuzalisha na hawana upendo wa kweli!


Huu ni mtizamo wangu sio sheria,toa na wewe mtizamo wako!
Karibu futari jioni,

Umenifanya nianze upya mapambano maana nishapoteza mara 3!

NARUDI TENA, VITA INAANZA
 
Wapo lakini wengi wao ni polygon kwa hali ya sasa watoto wazuri utaishia kuwaita shemeji na ukizifuma yule aliyekuvumilia utamuona km Mzee na jinsi mlivyo wanaume ukiwa vizuri kiuchumi basi hata kula utataka ule vilivyonona ni hayo tu
Ukute wewe mwenyewe umbo sanamu la Micheline umbo kuanzia juu mpaka chini vyote vipo sawa,
 
Haijarishi uwe maskini au tajiri lakini Mke mwema ni vipindi vyote huweza kupatikana . Umaskini si kipimo cha Mke mwema .
 
Habari,

Mimi nilikua nna pesa sana last year and kiukweli sijisifii ila mimi sina tabia ya umalaya sanaa kiivi na nlivyokua na pesa nlijitahid sana kupata mwanamke atakae nielwa au kunifaa kuishi nae sikupata .Japo niliingia kwenye mahusiano kadhaa lakni hayakudumu.Sasa hivi nimefulia kabisa yaan sina kitu lakin kuna msichana ananipenda sanaa na mimi nlishajua kama nlikosa kipindi nna hela sa hv ndo sipati kabisa yaani hat huyu mschna nilikutana nae kiajabu ajab na kuzoeaba nae kiajbu pia ...anasema ananipenda nashangaa imekuaje and she is very beautiful as well.Daah haya maisha lakni...acha tuuu.
Huyo mwanamke yuko real na wewe mzee, kama anakukomalia sana just check afya yake kwa ujumla kisha kaa nae kwa kutulia tu.
Wanawake real wapo ila tatizo men are too blind to see 'em! Ukiwa na pesa wengi wanafata maisha mepesi na umaarufu tu ila kupata alie na upendo 100% ni ngumu sana. Rember a womans loyalty is tested when a man has nothing bruh
 
Mahusiano ya siku hizi asilimia 96% ya wanawake wanataka penye maisha mazuri tu. Sio mwanaume anapendwa, vinavyo pendwa ni vilivyomo those material things kama utakuwa huna gari, huna nyumba na gari, huna kazi ya maana, huna mshahara, basi huwezi kuoa kirahisi hizi jamii zetu za kibantu. 96% yes likes money, hizo 4% zilizobaki ndio mazali ya mentali yapo huko kibahati bahati. Mimi nimexperience hii hali sana.
 
35 Reactions
Reply
Back
Top Bottom