Tambua wakati mzuri wa kutafuta mwanamke wa maisha!

nyaggad

JF-Expert Member
Dec 28, 2014
1,159
691
Habari wana jf!

Je ni wakati gani mzuri wa kutafuta mwanamke wa maisha yake kwa mwanaume?

1)je ni wakati ambao mwanaume ana maisha magumu ,hana Ajira,yani kipindi ambacho mwanaume anapambana na hali yake kutoka kwenye dimbwi la umaskini?au!

2)je ni wakati ambao mwanaume ana maisha mazuri,ana ajira nzuri,ameshatoka kwenye Dimbwi la umaskini na mwenye mafanikio ya kiuchumi?

Binafsi naona wakati mzuri wa mwanaume kutafuta mwanamke wa maisha yake,ni wakati ule mwanaume anapokuwa na maisha magumu,kwa sababu Dunia nzima hakuna mtu anaependa maisha magumu na umaskini labda awe chizi,na hapa Duniani kuna uchizi wa aina mbili tu "uchizi wa matatizo ya akili na uchizi wa mapenzi"lakini uchizi wa mapenzi ni mzuri maana huwa ni kiwango cha juu sana cha upendo, kwa mantiki hiyo ukimuona mwanamke amekubali kuishi maisha magumu na mwanaume maskini wakati kuna wanaume wenye maisha mazuri wanahitaji kuwa nae,unatakiwa ujue huyo mwanamke amechizika na mapenzi yani kwa tafsri nyingine "amependa kweli"na wahenga husema "Rafiki wa kweli ni yule akufaae kwa dhiki",ni bahati mbaya sana siku hizi wanaume wengi hutafuta wachumba pindi wanapokuwa wamefanikiwa ndio maana ndoa nyingi siku hizi hazidumu!

Hakika nawaambieni"ukweli ni vigumu kumpata mwanamke anaekupenda kweli ukiwa maskini lakini ni vigumu zaidi kumpata mwanamke anaekupenda kweli ukiwa Tajiri"sasa wewe subiri ufanikiwe ndipo utafute mchumba wa kuoa halafu uone mara ume filisika baada ya kuoa,hapo ndipo utakapojua kuwa kuna wanawake wenye Destiny ya umaskini,kwa sababu wanajua kutumia tu pesa hawajui kuzalisha na hawana upendo wa kweli!


Huu ni mtizamo wangu sio sheria,toa na wewe mtizamo wako!
 
Kiukweli mwanamke anaekupenda na kukuthamini ukiwa huna kitu hasa ktk hii hali ya vyuma kukaza nindio chaguo bora tatizo linakuja wewe unamuona kimuonekano hakuvutii sasa hapo ndo unapofeli.
Hilo nalo neno mkuu!
 
Habari wana jf!

Je ni wakati gani mzuri wa kutafuta mwanamke wa maisha yake kwa mwanaume?

1)je ni wakati ambao mwanaume ana maisha magumu ,hana Ajira,yani kipindi ambacho mwanaume anapambana na hali yake kutoka kwenye dimbwi la umaskini?au!

2)je ni wakati ambao mwanaume ana maisha mazuri,ana ajira nzuri,ameshatoka kwenye Dimbwi la umaskini na mwenye mafanikio ya kiuchumi?

Binafsi naona wakati mzuri wa mwanaume kutafuta mwanamke wa maisha yake,ni wakati ule mwanaume anapokuwa na maisha magumu,kwa sababu Dunia nzima hakuna mtu anaependa maisha magumu na umaskini labda awe chizi,na hapa Duniani kuna uchizi wa aina mbili tu "uchizi wa matatizo ya akili na uchizi wa mapenzi"lakini uchizi wa mapenzi ni mzuri maana huwa ni kiwango cha juu sana cha upendo, kwa mantiki hiyo ukimuona mwanamke amekubali kuishi maisha magumu na mwanaume maskini wakati kuna wanaume wenye maisha mazuri wanahitaji kuwa nae,unatakiwa ujue huyo mwanamke amechizika na mapenzi yani kwa tafsri nyingine "amependa kweli"na wahenga husema "Rafiki wa kweli ni yule akufaae kwa dhiki",ni bahati mbaya sana siku hizi wanaume wengi hutafuta wachumba pindi wanapokuwa wamefanikiwa ndio maana ndoa nyingi siku hizi hazidumu!

Hakika nawaambieni"ukweli ni vigumu kumpata mwanamke anaekupenda kweli ukiwa maskini lakini ni vigumu zaidi kumpata mwanamke anaekupenda kweli ukiwa Tajiri"sasa wewe subiri ufanikiwe ndipo utafute mchumba wa kuoa halafu uone mara ume filisika baada ya kuoa,hapo ndipo utakapojua kuwa kuna wanawake wenye Destiny ya umaskini,kwa sababu wanajua kutumia tu pesa hawajui kuzalisha na hawana upendo wa kweli!


Huu ni mtizamo wangu sio sheria,toa na wewe mtizamo wako!
Tatizo wanaume tukiwapenda katika nyakati za shida mnajiona wa maana sana na kutudharau kwamba tuko cheap, baadae mnaona hatuna hadhi... apandacho mtu ndicho atakachovuna
 
Sio zama hz aisee, unamkubali mwanaume hana kitu, unamsaport kwa kila hali, hela za nauli za kwenda kwny interview unamtafutia hata kwa kukopa, unamsaidia kutafuta matangazo ya kazi, kuaply, kusaka vibarua huku na huku, lkn akishainuka na kupata ajira na hela basi wewe unaonekana screpa!!! Anaanza kushoboka na wavaa mawigi wanaojua kujichubua na kutumia hela wasizozitafuta!!!! Mwisho wa siku anakubwaga kweupe na kashfa juu ati wewe sio hadhi yangu...wasengerema kweli hawa viumbe.
 
kwa akili za fasta kuna wanawake wa aina mbili 1. anayeweza kuwa na wewe wakat wa msoto hapa pagumu kidogo kwa wadada wapenda snapt chart au kuhudhuria vikao vya fried chicken pale mliman city KFC na mary brown 2. kuna wanawake ili uwe nao lazima uwe na kitu flan ndo ukweli hapa tunawaitaga wadada wa finished project
swala la kutafuta mwenza halina wakati maalum moyo wako utakwambia kwa sasa nimechoka kuhudhuria gest naitaji pumziko
 
Sio zama hz aisee, unamkubali mwanaume hana kitu, unamsaport kwa kila hali, hela za nauli za kwenda kwny interview unamtafutia hata kwa kukopa, unamsaidia kutafuta matangazo ya kazi, kuaply, kusaka vibarua huku na huku, lkn akishainuka na kupata ajira na hela basi wewe unaonekana screpa!!! Anaanza kushoboka na wavaa mawigi wanaojua kujichubua na kutumia hela wasizozitafuta!!!! Mwisho wa siku anakubwaga kweupe na kashfa juu ati wewe sio hadhi yangu...wasengerema kweli hawa viumbe.
Kweli,lakini usihukumu hivo kama umempenda mpende.sisi sio samaki akioza mmoja tumeoza wote wengine tumejaaliwa kujali na kuthamini fadhila zenu
 
35 Reactions
Reply
Back
Top Bottom