Michael Dalali
Member
- Jun 15, 2007
- 12
- 3
WanaJF,
Asasi ya vijana ya Tanzania Youth Vision Association-TYVA kupitia mradi wao wa Kijana na Kura Yako 2010 baada ya kutembelea mashuleni na vijiweni katika mikoa ya DSM, Pwani, Dodoma, Kilimanjaro, Tanga na Arusha sasa inaleta matamasha ya wazi kwa wananchi hususan vijana.
Oktoba 23, 2010 Tamasha litakuwa jijini Dar-es-Salaam kwenye viwanja vya Posta, eneo la Sayansi-Kijitonyama kuanzia saa nane mchana hadi 12 jioni. Wasanii wengi wameshahamasika na wanaendelea kujitokeza kujitolea kuhamasisha wananchi kushiriki kupiga kura. Wasanii ambao mpaka sasa wameshathibitisha ushiriki; Mkoloni, G-Solo, Vitalis Maembe, Baby Madaha, Parapanda Arts, Nick wa pili,Afande Sele, Nyandison, Latinga, Jumanne Iddi, Rogers, Malfred.
Tunaendelea kukaribisha wasanii ambao watakuwa na moyo wa kujitolea (pasi malipo) kuhamasisha wananchi kwani mradi huu ni wa kujitolea hauna ufadhili toka shirika ama nchi yoyote. Vijana wamechanga fedha kuuwezesha.
Baada ya Tamasha hili, litafata tamasha jingine Mkoani Kilimanjaro siku ya Oktoba 30!
Shiriki sasa!Jitokeze! Wahabarishe na wengine.
Asasi ya vijana ya Tanzania Youth Vision Association-TYVA kupitia mradi wao wa Kijana na Kura Yako 2010 baada ya kutembelea mashuleni na vijiweni katika mikoa ya DSM, Pwani, Dodoma, Kilimanjaro, Tanga na Arusha sasa inaleta matamasha ya wazi kwa wananchi hususan vijana.
Oktoba 23, 2010 Tamasha litakuwa jijini Dar-es-Salaam kwenye viwanja vya Posta, eneo la Sayansi-Kijitonyama kuanzia saa nane mchana hadi 12 jioni. Wasanii wengi wameshahamasika na wanaendelea kujitokeza kujitolea kuhamasisha wananchi kushiriki kupiga kura. Wasanii ambao mpaka sasa wameshathibitisha ushiriki; Mkoloni, G-Solo, Vitalis Maembe, Baby Madaha, Parapanda Arts, Nick wa pili,Afande Sele, Nyandison, Latinga, Jumanne Iddi, Rogers, Malfred.
Tunaendelea kukaribisha wasanii ambao watakuwa na moyo wa kujitolea (pasi malipo) kuhamasisha wananchi kwani mradi huu ni wa kujitolea hauna ufadhili toka shirika ama nchi yoyote. Vijana wamechanga fedha kuuwezesha.
Baada ya Tamasha hili, litafata tamasha jingine Mkoani Kilimanjaro siku ya Oktoba 30!
Shiriki sasa!Jitokeze! Wahabarishe na wengine.