Waridi
JF-Expert Member
- Mar 30, 2008
- 1,025
- 172
Watanzania wenzangu,napendekeza tuachane na kuadhimisha sikukuu ya wajinga.
Mjinga ni mtu asiyejua kusoma au kuandika au vyote viwili.Namna nzuri ya kuadhimisha siku yake basi ingekuwa ni kumsaidia aonokane na ujinga wake na pengine kumsaidia hapate kila ambacho kwa sababu ya ujinga alionao anakikosa,matharani kushindwa kupata taarifa muhimu zilizoko katika maandishi nk.
Cha kusikitisha eti duniani kuna sikukuu ya wajinga na inaadhimishwa kwa kudanganyana-kupeana habari za uongo-kupumbazana.
Kwangu mimi maadhimisho ya namna hiyo ni upumbavu.Heri basi siku hiyo ingeitwa sikukuu ya WAPUMBAVU,kwa maana ya kwamba ni siku ambayo waongo na wapumbavu wanapata fursa ya kusema uongo wao hadharani.
Najiuluza ni nini kisa cha watanzania kushabikia sikukuu hii,hadi hata vyombo vya habari vinaamua kuwauzia wanunuzi wa magazeti na wasikilizaji wao habari za uongo.
Maadhimisho haya ni upuuzi,tamaduni ya kuachana nayo.
Mjinga ni mtu asiyejua kusoma au kuandika au vyote viwili.Namna nzuri ya kuadhimisha siku yake basi ingekuwa ni kumsaidia aonokane na ujinga wake na pengine kumsaidia hapate kila ambacho kwa sababu ya ujinga alionao anakikosa,matharani kushindwa kupata taarifa muhimu zilizoko katika maandishi nk.
Cha kusikitisha eti duniani kuna sikukuu ya wajinga na inaadhimishwa kwa kudanganyana-kupeana habari za uongo-kupumbazana.
Kwangu mimi maadhimisho ya namna hiyo ni upumbavu.Heri basi siku hiyo ingeitwa sikukuu ya WAPUMBAVU,kwa maana ya kwamba ni siku ambayo waongo na wapumbavu wanapata fursa ya kusema uongo wao hadharani.
Najiuluza ni nini kisa cha watanzania kushabikia sikukuu hii,hadi hata vyombo vya habari vinaamua kuwauzia wanunuzi wa magazeti na wasikilizaji wao habari za uongo.
Maadhimisho haya ni upuuzi,tamaduni ya kuachana nayo.