kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 266
Msanii mmoja wa Hip Hop wa kike anayechipukia wa Uingereza amefariki dunia baada ya kujidunga sindano ya kuongeza makalio ili aweze kutamba kwenye anga za muziki kama kina Beyonce au Jennifer Lopez.
Kwa wale dada zetu wanaotamani kuwa na makalio makubwa na kuamua kujidunga sindano za kuongeza makalio basi wajifunze kutokana na habari hii ya mrembo wa Uingereza aliyezaliwa Nigeria mwenye umri wa miaka 20, Claudia Aderotimi ambaye amefariki wiki hii baada ya kudungwa sindano za kuongeza makalio.
Claudia alitamani kuwa na makalio makubwa ili yaweze kumuongezea jina kwenye anga ya muziki wa Hip-hop kama wanavyotamba kwa makalio yao Beyonce na Jennifer Lopez.
Mbali ya usanii wa muziki Claudia alikuwa pia na ndoto ya kuwa msanii mkubwa wa maigizo na mcheza dansi kwenye video za muziki.
Claudia aliamua kuongeza ukubwa wa makalio yake baada ya kutimuliwa kwenye dili la kudansi kwenye video ya msanii mmoja wa muziki nchini Uingereza.
Taarifa zilisema kuwa Claudia alipata dili la kudansi kwenye video ya muziki, siku ya kwanza alienda akiwa amesunda nguo kwenye makalio yake ili kuyafanya makalio yake yaonekane makubwa.
Siku hiyo alipokelewa vizuri na alitamba kwenye maandalizi ya video hiyo lakini alipogundulika kuwa alikuwa akiweka nguo kuyafanya makalio yake yaonekane makubwa alitimuliwa na kuambiwa asirudi tena.
Ili kuzitimiza ndoto zake za muziki, Claudia alisafiri kutoka London hadi Philadelphia, Marekani ili aweze kudungwa sindano za kuongeza makalio ambazo zilimgharimu dola 2000.
Claudia alidungwa sindano hizo ambazo zimepigwa marufuku nchini Marekani ndani ya hoteli moja mjini humo.
Muda mfupi baada ya kudungwa sindano hizo, Claudia alilamika maumivu makali kifuani na alipowahishwa hospitali alifariki.
Polisi nchini Marekani wanamtafuta daktari feki aliyemdunga Claudia sindano hizo huku wakiwa tayari wameishamtia mbaroni mwanamke anayedaiwa kulifanikisha dili la Claudia kusafiri kutoka Uingereza kwenda kwenye hoteli hiyo kuongeza makalio yake.
"Tumemhoji mwanamke aliyekuwa akiwasiliana kwa email na Claudia kufanikisha Claudia kuja hapa", alisema msemaji wa polisi na kuongeza "Kwa sasa tunamtafuta daktari aliyemchoma sindano hizo".
Kwa wale dada zetu wanaotamani kuwa na makalio makubwa na kuamua kujidunga sindano za kuongeza makalio basi wajifunze kutokana na habari hii ya mrembo wa Uingereza aliyezaliwa Nigeria mwenye umri wa miaka 20, Claudia Aderotimi ambaye amefariki wiki hii baada ya kudungwa sindano za kuongeza makalio.
Claudia alitamani kuwa na makalio makubwa ili yaweze kumuongezea jina kwenye anga ya muziki wa Hip-hop kama wanavyotamba kwa makalio yao Beyonce na Jennifer Lopez.
Mbali ya usanii wa muziki Claudia alikuwa pia na ndoto ya kuwa msanii mkubwa wa maigizo na mcheza dansi kwenye video za muziki.
Claudia aliamua kuongeza ukubwa wa makalio yake baada ya kutimuliwa kwenye dili la kudansi kwenye video ya msanii mmoja wa muziki nchini Uingereza.
Taarifa zilisema kuwa Claudia alipata dili la kudansi kwenye video ya muziki, siku ya kwanza alienda akiwa amesunda nguo kwenye makalio yake ili kuyafanya makalio yake yaonekane makubwa.
Siku hiyo alipokelewa vizuri na alitamba kwenye maandalizi ya video hiyo lakini alipogundulika kuwa alikuwa akiweka nguo kuyafanya makalio yake yaonekane makubwa alitimuliwa na kuambiwa asirudi tena.
Ili kuzitimiza ndoto zake za muziki, Claudia alisafiri kutoka London hadi Philadelphia, Marekani ili aweze kudungwa sindano za kuongeza makalio ambazo zilimgharimu dola 2000.
Claudia alidungwa sindano hizo ambazo zimepigwa marufuku nchini Marekani ndani ya hoteli moja mjini humo.
Muda mfupi baada ya kudungwa sindano hizo, Claudia alilamika maumivu makali kifuani na alipowahishwa hospitali alifariki.
Polisi nchini Marekani wanamtafuta daktari feki aliyemdunga Claudia sindano hizo huku wakiwa tayari wameishamtia mbaroni mwanamke anayedaiwa kulifanikisha dili la Claudia kusafiri kutoka Uingereza kwenda kwenye hoteli hiyo kuongeza makalio yake.
"Tumemhoji mwanamke aliyekuwa akiwasiliana kwa email na Claudia kufanikisha Claudia kuja hapa", alisema msemaji wa polisi na kuongeza "Kwa sasa tunamtafuta daktari aliyemchoma sindano hizo".