Taliban waanza mazungumzo na Maafisa wa Magharibi nchini Norway

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,000
9,862
Wajumbe wa Taliban wanakutana na maafisa wa nchi za magharibi nchini Norway kwa ajili ya mazungumzo ya kwanza Ulaya tangu kundi hilo lichukue udhibiti wa nchi ya Afghanstan.

Mazungumzo hayo, yaliyopangwa kufanyika kwa muda wa siku tatu, yatakijita katika suala la haki za binadamu pamoja na mzozo wa kibinadamu katika nchi hiyo.
Umoja wa Mataifa unasema 95% ya Waafghanstan hawana chakula cha kutosha.

Maandamano kadhaa yamefanyika Ulaya huku wakosoaji wakidai kuwa Taliban haipaswi kuzawadiwa kwa mazungumzo.

Jumapili, wajumbe wa Taliban walikutana na wanaharakati wa haki za binadamu lakini maelezo ya mazungumzo hayo bado hayajafichuliwa.

Leo Jumatatu inasemekana kuwa siku muhimu ya mazungumzo baina ya wajumbe wa Taliban na maafisa wa magharib. Kikundi hicho kimepanga kuomba kupata mabilioni yake ya dola yaliyofujwa katika benki za Marekani.

Afghanistan imeshuhudia ukosefu wa ajira na mfumuko wa bei za bidhaa, huku thamani yasarafu yake ikiporomoka na benki zimeweka ukomo wa kiasi cha pesa ambazo zinaweza kutolewa kwenye akaunti ya benki.

1643005730138.gif
 
Yaan hivyo vikundi vya kigaidi ni uhuni mtupu tu , ni mapicha picha tu, wazungu wanaunda vikundi hlf baadhi ya waislamu wasiojielewa wanashabikia eti wapigania dini yao , hv watu waliosababisha mauaji ya watu leo wanakaa nao meza moja , wkt hao hao walimpinga Muller na Taliban yake ya awali , waafrika tunaopotezwa na hao wahuni tujitafakari sn ,ujinga wa mwafrika ndo mtaji wa mzungᴜ
 
Yaan hivyo vikundi vya kigaidi ni uhuni mtupu tu , ni mapicha picha tu, wazungu wanaunda vikundi hlf baadhi ya waislamu wasiojielewa wanashabikia eti wapigania dini yao , hv watu waliosababisha mauaji ya watu leo wanakaa nao meza moja , wkt hao hao walimpinga Muller na Taliban yake ya awali , waafrika tunaopotezwa na hao wahuni tujitafakari sn ,ujinga wa mwafrika ndo mtaji wa mzungᴜ
Kwani Afaghanistan ipo Africa?
 
Back
Top Bottom