Taliban: Tupo tayari kushirikiana na nchi zote duniani isipokuwa Israel

Sam Gidori

Senior Member
Sep 7, 2020
165
414
Uongozi wa Taliban nchini Afghanistan umesema upo tayari kufanya kazi na nchi zote duniani isipokuwa Israel.

Msemaji wa Kundi hilo, Suhail Shaheen ameliambia Shirika la Habari la Sputnik News la nchini Urusi kuwa Taliban ipo tayari kufanya kazi na Marekani hata baada ya kusubiri kwa miaka 20 kuchukua madaraka tena nchini Afghanistan.

“Tupo katika zama mpya, ikiwa Marekani ipo tayari kurudisha uhusiano wa kidiplomasia na sisi, itakuwa kwa faida ya nchi zote mbili, na kama wapo tayari kuijenga Afghanistan, tunawakaribisha,” Shaheen alisema, akisisitiza kuwa Israel si nchi zilizopo katika orodha yao ya mataifa wanayopanga kushirikiana nayo.

Taliban imetangaza serikali mpya, ikiwahusisha watu walio katika orodha ya kimataifa ya wahalifu wanaosakwa kwa kujihusisha na ugaidi, akiwamo Waziri Mkuu, Mullah Mohammad aliye katika orodha ya waliowekewa vikwazo na Umoja wa Mataifa kwa kujihusisha na utawala wa kikatili kati ya mwaka 1996 hadi 2001.

Chanzo: Times of Israel

1631259072587.png
 
Marekani siku zote huwa hapigani vita vya hasara. Ukiona kakimbia ujue hasara imepatikana.

Vita ni biashara km biashara zingine na hili watu wengi hawalijui.

Kwa watu waamini mwezi na nyota wanaamini ktk machafuko na hii ndiyo silaha kubwa anayoitumia Marekani

Hawa wengi hawana shule, ukiangalia vyeti vyao ni vya madrasa.

Kwanini nchi za watu waamini mwezi na nyota kuna machafuko ya kivita? Watakuambia ni Marekani. Unajiuliza kwann Marekani.

Hata wewe hapo ukiwa na hela yako, unaweza kulipiga taifa lolote la waamini nyota na mwezi kwasababu uwezo wao wa kifikiri ni mdogo.

Libya wanapigana, Marekani anawangalia jinsi wapumbav wanapigana. Kumbe wanajikomoa wenyewe. Angalia Marekani wanavyojijenga, nenda ukalipue hata jengo moja uone. Utatafutwa popote ulipo na utauliwa

Marekani na Israel nani Baba?Kakimbia Baba Mtu unadhani ataweza Mtoto?
 
Wala siyo watata. Hapo Marekani waliona hakuna faida wanayopata zaidi ya hasara waakamua kusepa.

Vita ni biashara km biashara zingine. Hili wachache sana wanalolijua. Vita vya ufahari, havipo siku hizi.

Taliban ni viumbe watata sana. Haitaji buti kupigana , anataka tu open shoes zinatosha kukimbizana na adui yao. Noma sana "Talibs" kama wanavyojulikana Kabul.
 
Taliban wanalipa fadhila ni tatizo kubwa sana endapo mhusika kafanya vibaya kwenye Serikali. Ukimtoa kwenye nafasi yake anaondoka na watu wake anaenda kutengeneza kundi lake la kupinga Serikali.
 
Back
Top Bottom