John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,373
Mara baada ya kuelezwa kuwa Taasisi ya Mifupa (MOI), Dar es Salaam imekuwa na ongezeko kubwa la wagonjwa wa kupooza ndani yam waka mmoja imeelezwa kuwa moja ya sababu kubwa inayochangia hali hiyo ni aina ya maisha ambayo watu wanaishi kwa miaka ya hivi karibuni.
Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Dkt. Respicious Boniphace amesema takwimu zilizopo ni kuwa idadi ya wagonjwa kwa kupooza kwa mwaka hospitalini hapo ni 120-150 wakati miaka ya nyuma idadi ilikuwa wagonjwa 70-80 kwa mwaka.
Dkt. Respicious Boniphace
Anafafanua: “Asilimia kubwa chanzo ni magonjwa ya presha kutoka na mtindo wa maisha uliopo sasa kwa watu wengi, kubwa ikiwa ni mwili kutokuwa na mazoezi.
“Watu wengi sasa hivi wanatumia magari, bodaboda na aina nyingine za usafiri kila sehemu wanapokwenda hata kama kuna umbali mfupi, tofauti na ilivyokuwa zamani.
“Zamani watu walikuwa lazima watembee hata kwenda kwenye kituo cha daladala ilikuwa kawaida mtu kutembea kwa umbali fulani, lakini sasa hivi mtu anapanda boda kwenda kwenye kituo cha daladala hata kama hakuna umbali wa kiwango hicho.
“Hata watoto watoto wadogo nao hawapati muda wa kutembea, sehemu ndogo tu anatumia usafiri, wengine hawapati muda wa kuacheza na kuufanya mwili kuwa active.
“Hali hiyo ndiyo inachangia magonjwa mengi kama presha au sukari, sasa hivi kuna vijana wengi tu wa miaka 30-35 wanapata magonjwa ambayo zamani tulikuwa tunaona wanapata watu wazima kuanzia miaka 60 na kuendelea.
“Vyakula navyo vinachangia, mfano matumizi mengi ya nyama choma, unywaji wa pombe nyingi, sigara na matumizi ya shisha huku wakiwa hawafanyi mazoezi. Hiyo inaweza kusababisha mishipa ya damu kusinyaa na kuwa hatarini kupata stroke.”
Aidha, Dkt. Boniphace ametoa ushauri kwa kusema: “Niwaambie Wananchi kuwa kama haujisikii vizuri kama vile kichwa kinauma mara kwa mara, kuchokachoka, waende hospitali mapema kabla haijafikia levo mbaya.
“Wasiishie kununua dawa mtaani tu pasipokuwa na maelekezo ya daktari, waende hospitali wakafanyiwe vipimo na kubaini tatizo mapema kama lipo.
Pamoja na hivyo, amebainisha kuwa kawaida kwa siku wamekuwa wakitoa huduma kwa wagonjwa waliopooza 7 hadi 10.
Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Dkt. Respicious Boniphace amesema takwimu zilizopo ni kuwa idadi ya wagonjwa kwa kupooza kwa mwaka hospitalini hapo ni 120-150 wakati miaka ya nyuma idadi ilikuwa wagonjwa 70-80 kwa mwaka.
Dkt. Respicious Boniphace
Anafafanua: “Asilimia kubwa chanzo ni magonjwa ya presha kutoka na mtindo wa maisha uliopo sasa kwa watu wengi, kubwa ikiwa ni mwili kutokuwa na mazoezi.
“Watu wengi sasa hivi wanatumia magari, bodaboda na aina nyingine za usafiri kila sehemu wanapokwenda hata kama kuna umbali mfupi, tofauti na ilivyokuwa zamani.
“Zamani watu walikuwa lazima watembee hata kwenda kwenye kituo cha daladala ilikuwa kawaida mtu kutembea kwa umbali fulani, lakini sasa hivi mtu anapanda boda kwenda kwenye kituo cha daladala hata kama hakuna umbali wa kiwango hicho.
“Hata watoto watoto wadogo nao hawapati muda wa kutembea, sehemu ndogo tu anatumia usafiri, wengine hawapati muda wa kuacheza na kuufanya mwili kuwa active.
“Hali hiyo ndiyo inachangia magonjwa mengi kama presha au sukari, sasa hivi kuna vijana wengi tu wa miaka 30-35 wanapata magonjwa ambayo zamani tulikuwa tunaona wanapata watu wazima kuanzia miaka 60 na kuendelea.
“Vyakula navyo vinachangia, mfano matumizi mengi ya nyama choma, unywaji wa pombe nyingi, sigara na matumizi ya shisha huku wakiwa hawafanyi mazoezi. Hiyo inaweza kusababisha mishipa ya damu kusinyaa na kuwa hatarini kupata stroke.”
Aidha, Dkt. Boniphace ametoa ushauri kwa kusema: “Niwaambie Wananchi kuwa kama haujisikii vizuri kama vile kichwa kinauma mara kwa mara, kuchokachoka, waende hospitali mapema kabla haijafikia levo mbaya.
“Wasiishie kununua dawa mtaani tu pasipokuwa na maelekezo ya daktari, waende hospitali wakafanyiwe vipimo na kubaini tatizo mapema kama lipo.
Pamoja na hivyo, amebainisha kuwa kawaida kwa siku wamekuwa wakitoa huduma kwa wagonjwa waliopooza 7 hadi 10.