Takwimu hii ni sahihi? - Idadi ya wapiga kura TZ

Ninadhani kama vyama vya siasa viko makini ni rahisi kujua idadi kamili sababu kubwa ni kwamba vyama vingi vya uchaguzi vina mawakala katika sehemu za kupiga/kujiandikisha na lile daftari huwekwa wazi kwenye maeneo ya kura ili wapiga kura wa sehemu husika waweze kuthibitisha uhalali wa waliojiandikisha [katika sehemu husika] ninadhani ni suala la coordination tu na wakikuta hesabu zao na nec zimetofautiana basi inakuwa rahisi kushughulikiwa. lakini iwapo vyama vimelala basi idadi iliyotolewa na nec ndiyo inayotambulika.

Mkuu Abunuwas,
Wazo lako ni zuri. Tatizo ni kwamba kunakuwa na vituo hewa vingi ambavyo havisimamiwi na mawakala.Mawakala wanakuwa pia hewa, huko ndiko uchakachaji hufanyika. Na hapo ndio CCM inapojivunia kwamba watapatra %ge kubwa, kwani kama kura halali ni 10 million, basi hizo mtagawana vyama vyote, na wao wataongeza hizo dummy votes 9million. Hapo ndipo REDET wanapopatia vigezo vya kupika hizo data zao maana wana uhakika hao dummy voters ni wa CCM.
 
Tusilete wasiwasi kwenye mambo visible!! Ni ujinga kusumbua akili zetu kwenye vitu possible vingekuwa imposible angalau kungekuwa na hoja ya kupasua kichwa kutafuta utatuzi. Cha kufanya ni vyama kwa kutumia mawakala wao (Waaminifu) wapate idadi ya wakazi katika maeneo yao na kuyalinganisha na kwenye daftari la kudumu la wapiga kura then tuyajumlishe ili tulinganishe na hizo takwimu za NEC.

Angalizo, Inasemekana pamoja na mbinu ya kura hewa kuna mbinu nyingine ya kutengeneza kura feki. Mtu anapiga kura kwenye karatasi feki tangu alikotoka anahifadhi mfukoni na kwa kuwa vituoni hakuna utaratibu wa kusachiwa, anakuja kituoni anachanganya na aliyopewa then anazikunja kwa pamoja then anatumbukiza kwenye box. Mimi nadhani Mbinu hii ni rahisi kudhibitiwa iwapo vyama vitaweka mawakala waaminifu. Mawakala wahakikishe kila mpiga kura akisha andaa karatasi yake kabla ya kuitumbukiza aikunjue kuthibitisha kuwa ni karatasi moja bila kuonyesha aliyemchagua (sehemu yenye tiki) then atumbukize. Atakayekataa lazima atuhumiwe kuwa ana sintofahamu
 
Jamani, tuna tatizo kubwa sana sana sana kuliko tulivyotegemea, inakuwaje watu mnashindwa kutumia dakika moja kusoma wenzenu walichoandika kazi ni kukurupuka tu?

How do we get into conversations kwa tabia hii ya uvivu wa kusoma na papara zinazoonyesha umbumbumbu wetu na hatuoni haya? This is very embarassing, hivi wachangiaje mmesoma swali na hoja anayoiweka hapa mwenzetu Nyambala? Inahusina vipi na waliyoweka wachangiaji? tatizo letu hatutulii soma between the line tunaulizwa kama hizi takwimu zinaaminika?

Tuongee hilo sio swala la kutaka vitambulisho wala kujiandikisha kwenye daftari. Huu ndio uzembe unaoendeana na kuwa anonymous, tujirekebishe jamani tunawapa faida wanaosema kuwa ukitaka kumtoa mtanzania kwenye majadiliano mpatie habari kwa maandishi.

Hichi ndio nilichokiona hapa, tukosoane ili turekebishane sasa nyie ndio mngekua kwenye negotiation teams za mikataba si kungekua na tofauti na hii tunayoilalamikia?

Nyambala anatupa angalizo kwamba tume imeanza ku doctor tangu base line, hakuna mwaka watanzania wamejiandikisha kwa idadi inayotangazwa na electoral commission wakati wanadia tayari mwaka huu watu wengi zaidi ya mwaka jana hawajajiandikisha.

Tusome taarifa za tume kwa dar es salaam kwa mfano walishasema watu waliomba siku ziongezwe kwa sababu siku zilikua chache sana hivyo kuwanyima watu nafasi ya kupiga kura. Huko zanzibar tumesikia daftari la wapiga kura lilivyosababisha watu wengi zaidi ya miaka ya nyuma kushindwa kujiandikisha sasa hii overwehlming response imetoka wapi?

Wana-cook ndio maana wana guts za kusema hawahitaji kura za civil service kwa wao kuendelea kuongozia nchi.

Unajua mapungufu yaliyopo ktk taarifa (thread) ni takwimu mbili tofauti. Takwimu ya uchaguzi wa mwaka huu inaonyesha watu waliojiandikisha kupiga kura, wakati ile ya mwaka 2005 yaonyesha watu waliopiga kura. Kutokana na taarifa hizo mbili tofauti na za kuchanganya sioni kosa la wachangiaji.

Fikiria kama waliopiga kura mwaka 2005 walikuwa 60% ya wale waliojiandikisha. Kama hivyo ndivyo basi tunatafakari kuwa waliojiandikisha walikuwa takriban 16 milion. Na ukizingatia taarifa ya 'Clark' ambaye alikuwepo ktk mchakato 2005, na amekiri kuwa huu mwaka tuko makini sana si tu ktk uandikishaji bali vile vile katika kutoa elimu ya urai. Hii inamaanisha kwamba kiwango cha watanzania kuelewe umuhimu wa kujiandikisha na kupiga kura itaongezeka.

Binafsi sioni ajabu kwa 21 mil kuandikishwa katika nchi yenye jumla ya watu 40 mil. Tuendelee kuiamini tume tutafanya uchaguzi vizuri na kwa amani. Wakati mwingine nafikiri kuwa wapinzani wapo tayari kupinga lolote lisemwalo na Tume hata wakisema kuwa walimkaribisha Clark kwa kunywa Chai na maandazi, vitumbua, sambusa na chapati.
 
Nazani ingekuwa vizuri watu wa takwimu wangezinyambua na kuweka wazi data zao, let's say kwa kila mkoa wangetuwekea kuna jumla ya idadi ya watu wangapi, wa chini ya 18 ni wangapi na waliojiandikisha kupiga kura ni wangapi.
 
hiyo idadi inawezekana kweli imefikiwa, na hapa lazima tuwe makini kuhakiki nani na nani ndio wamepiga kura siku hiyo ya 31 oct, ni ukweli usiopingika kuwa watu wengi wamekuwa na interest ya kujiandikisha ili kupata hiyo kadi na si kwa sababu ya kupigia kura, na hapa ndipo Vyama vya upinzani vinatakiwa kuwa makini mno, kama kutakuwa hakuna uhakiki mzuri siku ya kupiga kura, basi kama watu 10,000,000 ndio wamepiga kura, Chama tawala wanaweza kuweka hata ziada ya 5,000,000 ili isomeke waliopiga kura ni 15,000,000 na hapo tayari hizo 5,000,000 zitakuwa ni za CCM
 
Nakumbuka nilipokwenda kujiandikisha kuwa mpiga kura, SIKUULIZWA VITU VIFUATAVYO
(1) Cheti cha kuzaliwa
(2)Cheti cha ndoa
(3)Cheti cha ubatizo
(4) Pasipoti
(5) Document yoyote ambayo angalau inaonyesha umri wangu.
(6) Kitambulisho chochote chenye kuonyesha umri wangu na jina.

Je kwa mantiki hiyo, tume ya uchaguzi haioni kwamba iliandikisha wasio kuwa na sifa ya kupiga kura wakiwemo.
(1) wale ambao si raia?
(2) wale ambao hawajafikisha umri wa kupiga kura?
(3) Kuandikisha mara mbili au zaidi, watu wale wale kwa majina tofauti?

Je tume ya uchaguzi haioni kwamba uwingi wa wapiga kura hao milioni 19 wakawa ni kutokana na hitilafu hizo?.

ANGALIZO
(1) Zoezi la kuandikisha wapiga kura halikwenda vizuri sana kama NEC inavyotaka tuamini. kuna vitu vya msingi kabisa ambavyo vilikuwa havizingatiwi vizuri(chukulia mfano wa kituo nilipojiandikisha mimi), mfano wa vitu nilivyovitaja hapo juu.

Wakati ule najiandikisha kupiga kura nilihisi kabisa kwamba ile ni "time bomb" na kwamba something was wrong.,
Inawezekana vipi kusajili namba simu mtu unatakiwa upeleke photocopy ya kitambulisho cha kukutambulisha lakini kwenye kusajili kitambulisho cha mpiga kura usipeleke document yoyote ya kukutambulisha? kipi ni muhimu zaidi kwa mustakbali wa nchi, namba ya simu au kadi ya mpiga kura?

(2) Je tume(NEC) haioni kwamba Wakati ule ilipokuwa katika hatua za mwisho za kuandikisha mpiga kura, kuna vijana wasio na umri wa kupiga kura lakini wanamiliki simu, na ili kusajili namba zao za simu walitakiwa kuwa na vitambulisho, kwa hiyo wakajiandikisha(bila uthibitisho wa vigezo vya mpiga kura) ili kupata kitambulisho cha mpiga kura ili iwe rahisi kwa wao kusajili simu zao?

otherwise tume itueleze hao wapiga kura milioni 19 wametoka wapi?
 
Ndugu zangu hainiingii akilini. wapiga kura zaidi ya millioni 19 tanzania wametokea wapi? kuna kiwanda cha kufyatua wapiga kura? nauliza hivi kwa sababu kulingana na sensa ya mwaka 2002 ni kuwa watu waliokuwa na miaka 10 kwa kwa mwaka 2010 wanamiaka 18 hivyo wana haki ya kupiga kura . Tukichukua hizo age groups kuanzia miaka 10 mpaka zaidi ya miaka 80 tunapata wapiga kura millioni 23. hapo ni kuwa kila mtu alijiandikisha na hakuna aliyefariki. Hii turn up ya watu waliojiandikisha imetoka wapi? Ni nchi gani ulimwenguni imewahi kuandikisha watu karibia wate wenye haki ya kupiga kura kama si maajabu mengine ya Dunia?

Nimeambatanisha jedwari hapa chini halafu mpime wenyewe

AGE
Total (M&F)

10-14
4,443,257

15-19
3,595,735

20-24
3,148,513

25-29
2,801,965

30-34
2,229,046

35-39
1,669,873

40-44
1,348,508

45-49
984,823

50-54
883,820

55-59
590,667

60-64
604,956

65-69
439,671

70-74
377,852

75-79
221,354

80 and over
308,208
Total
23,648,248
 
Hata mimi nashangaa wakati kila mtu hapa jf ana watoto si chini ya 2 ambao umri wao hauwaruhusu kupiga kura!population ipo in pyramid,vinginevyo watanzania wengi hawazai kwa sasa
 
Kutokana na kuwepo wapiga kura hewa kama nyzi moja ilivyoonesha ni wazi kuwa hii si idadi sahihi ya wapiga kura. Hoja ya Prof. Baregu kuwa kuna wapiga kura hewa milioni tatu ni sahihi. Hivyo Makame, Kiravu na Ikulu wamefanya kazi hii ya kuiba kura. Hii ni dhambi kubwa sana
 
Ndugu zangu hainiingii akilini. wapiga kura zaidi ya millioni 19 tanzania wametokea wapi? kuna kiwanda cha kufyatua wapiga kura? nauliza hivi kwa sababu kulingana na sensa ya mwaka 2002 ni kuwa watu waliokuwa na miaka 10 kwa kwa mwaka 2010 wanamiaka 18 hivyo wana haki ya kupiga kura . Tukichukua hizo age groups kuanzia miaka 10 mpaka zaidi ya miaka 80 tunapata wapiga kura millioni 23. hapo ni kuwa kila mtu alijiandikisha na hakuna aliyefariki. Hii turn up ya watu waliojiandikisha imetoka wapi? Ni nchi gani ulimwenguni imewahi kuandikisha watu karibia wate wenye haki ya kupiga kura kama si maajabu mengine ya Dunia?

Nimeambatanisha jedwari hapa chini halafu mpime wenyewe

AGE
Total (M&F)

10-14
4,443,257

15-19
3,595,735

20-24
3,148,513

25-29
2,801,965

30-34
2,229,046

35-39
1,669,873

40-44
1,348,508

45-49
984,823

50-54
883,820

55-59
590,667

60-64
604,956

65-69
439,671

70-74
377,852

75-79
221,354

80 and over
308,208
Total
23,648,248

Dah, hizi ni hesabu za ngumbaru. Ukitaka kutuhabarisha juu ya idadi ya wapiga kura Tz lazima ujumulishe factors zifuatazo;

(i) Usahihi wa sensa ya 2002 na achano sanifu (standard deviation/error)
(ii) Idadi ya wahamiaji tangu 2002 ambao wana haki kisheria kupiga kura
(iii) Idadi ya watanzania waliorudi nchini kutoka ng'ambo kuanzia 2002

Tanzania ya leo inakadiriwa kuwa na watu 44 million, roughly tuki assume kwamba 43% wana umri wakupiga kura tutapata roughly 19 milion
 
Jamani, tuna tatizo kubwa sana sana sana kuliko tulivyotegemea, inakuwaje watu mnashindwa kutumia dakika moja kusoma wenzenu walichoandika kazi ni kukurupuka tu?

How do we get into conversations kwa tabia hii ya uvivu wa kusoma na papara zinazoonyesha umbumbumbu wetu na hatuoni haya? This is very embarassing, hivi wachangiaje mmesoma swali na hoja anayoiweka hapa mwenzetu Nyambala? Inahusina vipi na waliyoweka wachangiaji? tatizo letu hatutulii soma between the line tunaulizwa kama hizi takwimu zinaaminika? .


I wish wengi wetu tungeliona hili na kutambua kuwa wakati mwengine hata sisi tunaojua kugonga keyboards za Kopyuta hatuna tofauti na watanzania tunaowaita mbumbumbu waliokosa maono ya UKOMBOZI katika kufikia maamuzi.........We do not read between the lines, I mean we don't read at all .....
 
Dah, hizi ni hesabu za ngumbaru. Ukitaka kutuhabarisha juu ya idadi ya wapiga kura Tz lazima ujumulishe factors zifuatazo;

(i) Usahihi wa sensa ya 2002 na achano sanifu (standard deviation/error)
(ii) Idadi ya wahamiaji tangu 2002 ambao wana haki kisheria kupiga kura
(iii) Idadi ya watanzania waliorudi nchini kutoka ng'ambo kuanzia 2002

Tanzania ya leo inakadiriwa kuwa na watu 44 million, roughly tuki assume kwamba 43% wana umri wakupiga kura tutapata roughly 19 milion

Kwa mujibu ya State of The World Population Report 2010 ya United Nations iliyotolewa tarehe 20 Oktoba 2010, idadi ya watanzania ni watu milioni 45 na ushehe.....
 
Ndugu zangu hainiingii akilini. wapiga kura zaidi ya millioni 19 tanzania wametokea wapi? kuna kiwanda cha kufyatua wapiga kura? nauliza hivi kwa sababu kulingana na sensa ya mwaka 2002 ni kuwa watu waliokuwa na miaka 10 kwa kwa mwaka 2010 wanamiaka 18 hivyo wana haki ya kupiga kura . Tukichukua hizo age groups kuanzia miaka 10 mpaka zaidi ya miaka 80 tunapata wapiga kura millioni 23. hapo ni kuwa kila mtu alijiandikisha na hakuna aliyefariki. Hii turn up ya watu waliojiandikisha imetoka wapi? Ni nchi gani ulimwenguni imewahi kuandikisha watu karibia wate wenye haki ya kupiga kura kama si maajabu mengine ya Dunia?

Nimeambatanisha jedwari hapa chini halafu mpime wenyewe

AGE
Total (M&F)

10-14

4,443,257






15-19
3,595,735







20-24

3,148,513



25-29

2,801,965



30-34

2,229,046



35-39

1,669,873



40-44

1,348,508



45-49

984,823



50-54

883,820



55-59

590,667



60-64

604,956



65-69

439,671



70-74

377,852



75-79

221,354



80 and over

308,208


Total
23,648,248

Idadi ya wapiga kura feki wa CCM ni kati ya milioni 7,000,000 na 11,000,000 kwa kadirio la juu. Hivi hakuna afisa wa Chadema aliyepewa Jukumu la kuangalia hii JF. Hii data inaonyesha kuwa watu wote wenye umri wa kupiga kura wamejiandikisha kupiga kura na hakuna aliyekufa tangu mwaka 2002 sensa ilipofanyika. Huu ni uchakachuaji wa wazi na tunaomba suala hili Chadema walitolee ufafanuzi hapa namna ya kulikabili maana yake ni kuwa CCM na NEC wameshafanya uchakachuaji wa hali ya juu. Tukichukulia kuwa asilimia 60% ya watu waliofikia umri wa kupiga kura hujiandikisha kupiga kura, idadi ya waliojiandikisha ilitakiwa iwe milioni 14, 188, 949 kutokana na data ya sensa ya mwaka 2002 hapo juu ambayo imejumuisha hata watu waliofikisha miaka 18 kutoka umri wa miaka 10 waliyokuwa nayo mwaka 2002. Na kama asilimia 80% ya watu wenye umri wa kupiga kura hujiandikisha basi idadi ya watu waliojiandikisha kutokana na takwimu ya watu wenye umri wa kupiga kura ingekuwa 18,918,598. Kwa takwimu hizi idadi ya wapiga kura feki ni kati ya milioni tisa yaani 9,459,299 na karibia milioni tano 4,729,650.

Lakini idadi halisi ya kura zinazochakachuliwa ni zaidi ya milioni tano 5,000,000 kwa kadirio la chini na zaidi ya milioni tisa 9,500,000 kwa kadirio la juu kwa sababu haiwezekani karibia watu wote waliofikia umri wa kupga kura wawe wamejiandikisha. Kwa hiyo uchakachuaji unaweza kuzalisha kura feki za CCM kati ya milioni 7,000,000 na milioni 11,000,000. Chadema hii taarifa ya Kindundulima ifanyieni kazi. Mwafrika, Quinine, Mwanakijiji, Maxene Melo, tafadhali wajulisheni Chadema kuhusu data hii ya wapiga kura na kadirio la kura zinazotegemewa kuchakachuliwa. Huu uchakachuaji unatisha.
 
Kwa mujibu ya State of The World Population Report 2010 ya United Nations iliyotolewa tarehe 20 Oktoba 2010, idadi ya watanzania ni watu milioni 45 na ushehe.....

Hey buddie where the f..k is that report???????
 
Hii ishu imeongelewa wiki 2 zilizopita na Profesa Baregu lkn NEC ilimwambia kuwa takwimu ni sahihi na yeye Prof Baregu amefanya makosa.

Mkuu Susu tulijadili hii ishu humu JF kuanzia May!
 
Back
Top Bottom