TAKUKURU yawashikilia Wafanyakazi 30 wa Bohari ya Madawa (MSD) na Mmoja wa Wizara ya Afya kwa Ubadhilifu wa Mil. 54

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,807
11,969

1592912701402.png

Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mwanza, Emmanuel Stenga

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) inawashikilia wafanyakazi 30 wa Bohari ya Dawa (MSD) Mkoa wa Mwanza kwa tuhuma za ubadhirifu wa dawa na vifaa tiba zenye thamani ya zaidi ya Sh. 254 milioni.

Mbali na wafanyakazi hao, pia kuna mtumishi mmoja wa Wizara ya Afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto.

Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mwanza, Emmanuel Stenga akitoa taarifa ya kushikiliwa kwa watumishi hao leo Jumanne tarehe 23 Juni 2020 amesema, uchunguzi unaendelea na watakaobainika wafanyikishwa Mahakamani.

“Natoa wito kwa wafanyakazi wa umma kuridhika na vipato vyao,” amesema Stenga.
 
Nitapambana Na Rushwa Bila Kigugumizi Chochote Na Dawa Ya Jipu Ni Kulitumbua Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
 
"Natoa wito kwa wafanyakazi wa umma kuridhika na vipato vyao,” amesema Stenga.
 
Hao taka kuku wenyewe wanaridhika na vipato vyao...au huu wimbo unanoga ukiwa unawaimbia wenzako..
 
  • Thanks
Reactions: a45
Ili ufisadi ukome kwa watumishi basi kwa hatua ya kwanza waweke mishahara sawa kwa kada au kwa wenye elimu level moja. Pili maslahi nyinginezo kama pango, lunch na usafiri wapewe wote kwa ujumla.
Binafsi sipendi rushwa na ufisadi ila nikiona pesa imezubaa naigeuza kuwa yangu
 
Nimesikia Manyara wengine wanashikiliwa na Takukuru kwa makosa ya mwaka 2014,nilishangaa sana mbona zamani!

Maana ukisema ufuatilie miaka hiyo mbona mtaani kutanuka!
 
Hayo mapendekezo yako ni ya kitoto.
Watu wanaweza kuwa na elimu moja ila mmoja amefanya kazi miaka mingi bila shaka uzoefu wake hauwezi kuwa sawa na mtu katoka Chuo jana.

Kama huutambui uzoefu kazini na kwamba unaweza kuwa na tija zaidi basi unaonekana una matatizo na ninyi ndio wezi wakubwa
Ili ufisadi ukome kwa watumishi basi kwa hatua ya kwanza waweke mishahara sawa kwa kada au kwa wenye elimu level moja. Pili maslahi nyinginezo kama pango, lunch na usafiri wapewe wote kwa ujumla.
Binafsi sipendi rushwa na ufisadi ila nikiona pesa imezubaa naigeuza kuwa yangu
 
Hayo mapendekezo yako ni ya kitoto.
Watu wanaweza kuwa na elimu moja ila mmoja amefanya kazi miaka mingi bila shaka uzoefu wake hauwezi kuwa sawa na mtu katoka Chuo jana.

Kama huutambui uzoefu kazini na kwamba unaweza kuwa na tija zaidi basi unaonekana una matatizo na ninyi ndio wezi wakubwa
Hujanielewa.
Hivi muhasibu wa TBA mwenye shahada na ana uzoefu wa miaka 5 unajua kuwa anazidiwa kwa mshahara na fresh graduate anayeanza kazi Tanesco?.
Waboreshe muundo wa mshahara kwa kuweka uwiano sawia
 
Nimestushwa na Taarifa ya TAKUKURU. Wafanyakazi wa Bohari 30 wapo Mahabusu kwa kile kinachodaiwa kuwa walikuwa katika maandalizi ya kupiga mzigo wa Mil 254!

IMG_2352.jpg

Huku aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa MSD akiendelea kutumikia mahabusu, wafanyakazi wake 30 wameingia kwenye kundi lilelile la kujaribu kuhujumu uchumi.

Taasisi ina Mkurugenzi Mkuu, ina Wakurugenzi, ina meneja, ina wasimamizi; hayo yote inawezekana vipi kutokea?

Sasa najaribu kuuliza zoezi la kuhesabu mali kwa miaka ya nyuma lilikuwa na udanganyifu kiasi gani? Bila shaka reconciliation ya miaka ya nyuma ilikuwa fake hatari.

Kuna haja ya serikali kutolea macho sana hiyo taasisi bado haijakaa sawa kabisa.

TAKUKURU wanadai kwamba hao wafanyakazi wanajitetea kuwa Dawa hizo zilikuwa zimeshamaliza muda wake wa matumizi.

Dawa zilizokufa zinahifaziwa vipi ndani ya ghala ? halafu humo humo kuna wafanyakazi, Je TMDA, OSHA mpo wapi kuhusu usalama wa maisha ya watu, hawa watu hawapo makini kabisa! Kuhifadhi Dawa zilizomaliza muda wake ni kuhifadhi sumu.

Matokeo yake ni wafanyakazi kufa na Saratani na kutojua chanzo chake ni nini.

Wizara ya Afya inapotoa takwimu za kuongezeka kwa ugonjwa wa Saratani, kuna haja pia kujumuisha sababu kama hizo za kukaa na madawa yaliyomaliza muda wa matumizi.

Ila Ukistaajabu ya Firauni, Utayaona ya MSD, Hospitali hazina Dawa, nyie dawa zinawafia humo humo. Aisee JPM kazi anayo sana.

Ushauri wa wazi kabisa kwa Mkurugenzi Mkuu Mpya, tunajua hili pia sio lake, ni lazima litakuwa ni muendelezo wa Utawala uliopita; lakini pia Brigedia Mhidze alichunguze vema hili tukio. Isijekuwa ni katika harakati za kumtia DOA huyo Mkurugenzi Mpya. Sehemu yoyote yenye Ulaji Fitna hazikosi. Kuna kitu hakipo sawa hapo Bohari Kuu!

Kubwa kuliko, Mkurugenzi Mpya akitaka kufaulu afumue hiyo taasisi kichwa chini miguu juu. Ni wazi kuwa tatizo sio watu, tatizo ni mfumo. Kama utabadili watu na mfumo ni uleule, bado ni tatizo.

Kama utabadili mfumo na ukabadili na watu hasa wale ambao ni bogasi na wapo sehemu za maamuzi, hapo utakuwa umefaulu.

Vinginevyo drama zitakuwa nyingiiiii mwishowe wote mnadondokea pua.

Ila TAKUKURU, hii ishu ya Kangi Lugola imeishia wapi? mnakomaa na vi Mil 254, mnaacha Tril za pesa na perdiem za nje ya nchi walizokuwa wakilipana, acheni drama na muwe Serious. Kama mnapambana na Rushwa pambaneni na Rushwa kwa Wote.

Au kupambana na Rushwa kuna matabaka?

I hate kuona dagaa wakisumbuliwa halafu wale masterminder wanazungushiwa mlango wa nyuma. Acheni hiyo mambo. Tatizo la Rushwa hapo Tanzania ni kubwa.

IMG_2352.jpg
Lifanyieni kazi kumsaidia Rais majukumu yake.
 
Back
Top Bottom