Jibaba Bonge
JF-Expert Member
- May 6, 2008
- 1,246
- 401
Wednesday, 06 October 2010
Na Leon Bahati
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imepinga kauli aliyotoa askofu mkuu wa Kanisa la Anglikana, Valentino Mokiwa kwamba wananchi wakipewa fedha za rushwa na wagombea wapokee kwa kuwa si dhambi kula fedha za wajinga.
Takukuru, ambayo inalalamikiwa kwa kutofanyia kazi taarifa za rushwa kwenye uchaguzi zinazotolewa na wananchi, imesema kwamba itamchukulia hatua kali mtu yeyote atakayetekeleza kauli hiyo ya Askofu Mokiwa kwa kuwa kupokea rushwa na kuvunja sheria.
Akizindua mpango wa Bima ya Afya ya Imani kwa Watu Wenye Kipato cha Chini jijini Dar es Salaama juzi, Askofu Mokiwa aliwataka waumini wa kupokea na kula pesa zote zinazotolewa na wagombea wa nafasi mbalimbali katika kampeni zinazoendelea nchi nzima akisema "fedha za namna hiyo si dhambi, si haramu wala si rushwa".
Lakini Askofu Mokiwa aliwaonya waumini kwamba fedha hizo zisiwafanye wawapigie kura wagombea wanaowapa fedha kwa kuwa wanaotoa rushwa hiyo ni "wajinga na kula fedha ya mjinga bila ya kumtekelezea azma yake si kosa".
Kauli kama ya Askofu Mokiwa zimekuwa zikitolewa na hata wanasiasa ambao huwaeleza wananchi kuwa wapokee fedha zinazotolewa na wagombea, lakini waadhibu siku ya kupiga kura.
Jana, ofisa uhusiano wa Takukuru, Doreen Kapwani aliiambia Mwananchi kwamba sheria ya rushwa iko wazi na kwamba mtoaji na mpokeaji ni wahalifu.
Kapwani alisema watakaofuata kauli zinazotolewa majukwaani wanaweza kujikuta matatani kwa sababu Takukuru ni chombo kilichoundwa kisheria na kinaongozwa kwa kanuni za sheria hiyo.
"Sheria hii katika kifungu cha 15 inatamka wazi kuwa mtu yeyote anayetoa au kupokea hongo atakuwa ametenda kosa chini ya sheria hii," alisema.
Kutokana na hali hiyo, Kapwani aliwataka wananchi wanapowaona wagombea au mtu yeyote anayetoa rushwa watoe taarifa Takukuru ili hatua zinazofaa zichukuliwe.
SOURCE : MWANANCHI
Hawa Takukuru ni wapuuzi sana. Wanapelekewa taarifa hawazifanyii kazi kwa sababu wahusika ni CCM. Mbaya zaidi wanawapigia simu kuwaambia waondoke haraka kwenye eneo la tukio kama alivyosema Lema pale Arusha. Sasa wanajifanya kumjia juu Askofu.
Siku zao zinahesabika.
Na Leon Bahati
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imepinga kauli aliyotoa askofu mkuu wa Kanisa la Anglikana, Valentino Mokiwa kwamba wananchi wakipewa fedha za rushwa na wagombea wapokee kwa kuwa si dhambi kula fedha za wajinga.
Takukuru, ambayo inalalamikiwa kwa kutofanyia kazi taarifa za rushwa kwenye uchaguzi zinazotolewa na wananchi, imesema kwamba itamchukulia hatua kali mtu yeyote atakayetekeleza kauli hiyo ya Askofu Mokiwa kwa kuwa kupokea rushwa na kuvunja sheria.
Akizindua mpango wa Bima ya Afya ya Imani kwa Watu Wenye Kipato cha Chini jijini Dar es Salaama juzi, Askofu Mokiwa aliwataka waumini wa kupokea na kula pesa zote zinazotolewa na wagombea wa nafasi mbalimbali katika kampeni zinazoendelea nchi nzima akisema "fedha za namna hiyo si dhambi, si haramu wala si rushwa".
Lakini Askofu Mokiwa aliwaonya waumini kwamba fedha hizo zisiwafanye wawapigie kura wagombea wanaowapa fedha kwa kuwa wanaotoa rushwa hiyo ni "wajinga na kula fedha ya mjinga bila ya kumtekelezea azma yake si kosa".
Kauli kama ya Askofu Mokiwa zimekuwa zikitolewa na hata wanasiasa ambao huwaeleza wananchi kuwa wapokee fedha zinazotolewa na wagombea, lakini waadhibu siku ya kupiga kura.
Jana, ofisa uhusiano wa Takukuru, Doreen Kapwani aliiambia Mwananchi kwamba sheria ya rushwa iko wazi na kwamba mtoaji na mpokeaji ni wahalifu.
Kapwani alisema watakaofuata kauli zinazotolewa majukwaani wanaweza kujikuta matatani kwa sababu Takukuru ni chombo kilichoundwa kisheria na kinaongozwa kwa kanuni za sheria hiyo.
"Sheria hii katika kifungu cha 15 inatamka wazi kuwa mtu yeyote anayetoa au kupokea hongo atakuwa ametenda kosa chini ya sheria hii," alisema.
Kutokana na hali hiyo, Kapwani aliwataka wananchi wanapowaona wagombea au mtu yeyote anayetoa rushwa watoe taarifa Takukuru ili hatua zinazofaa zichukuliwe.
SOURCE : MWANANCHI
Hawa Takukuru ni wapuuzi sana. Wanapelekewa taarifa hawazifanyii kazi kwa sababu wahusika ni CCM. Mbaya zaidi wanawapigia simu kuwaambia waondoke haraka kwenye eneo la tukio kama alivyosema Lema pale Arusha. Sasa wanajifanya kumjia juu Askofu.
Siku zao zinahesabika.