TAKUKURU yakamata dawa za Binadamu ambazo zimeisha muda wake zikiwa zinauzwa kwa ajili ya matumizi ya binadamu

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,499
9,279
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Mara imekamata dawa za binadamu zenye thamani ya zaidi ya Sh155.1 milioni ambazo zimeisha muda wake zikiwa zinauzwa kwa ajili ya matumizi ya binadamu.

Kamanda wa Takukuru wa mkoa huo, Alex Kuhanda alisema jana kuwa dawa hizo zilikamatwa katika vituo vya kutolea huduma za afya vya Serikali na binafsi kuanzia Oktoba mwaka jana.

Alisema baada ya kupata taarifa za uwepo wa dawa hizo, ofisi yake iliamua kufanya uchunguzi na kubaini dawa hizo mbali na kuwepo katika vituo hivyo vya kutolea huduma.

Kuhanda alisema dawa hizo ziliisha matumizi tangu Agosti mwaka jana.

“Kutokana na hali hiyo, madaktari wawili walikamatwa na hivi sasa wako nje kwa dhamana huku uchunguzi ukiendelea, uchunguzi ukikamilika hatua za kisheria zitachukuliwa,” alisema Kuhanda.

Pia, alisema uchunguzi wa awali umebaini dawa hizo zilisambazwa muda mchache kabla ya kuisha muda wake kwa maelekezo ya kugawiwa bure ingawa zilipofika katika vituo hivyo zilianza kuuzwa kwa watumiaji.

Alisema dawa walizokamata ni za ‘antibayotiki’ kama vile ‘Amoxyline, Ampisiline na Chlorofenical’ dawa ambazo kiuhalisia zina uhitaji mkubwa katika jamii.

Alisema endapo utaratibu ungefuatwa ni vigumu kwa dawa kiasi hicho kuisha muda wake wa matumizi kabla ya kufikia watumiaji.

“Dawa zote, ni zile zinazotumiwa sana, hivyo ni vigumu kwa dawa kiasi hiki kuisha muda wake kabla ya kumfikia mtumiaji, hivyo kwa haraka haraka unaweza kubaini hapa kuna hujuma ya makusudi ilifanyika; kwa hiyo tunachunguza ili tubaini nani alizuia hizi dawa kugawiwa kwa wahitaji zikiwa bado muda wake wa matumizi unaendelea,” alisema Kuhanda.

Katika hatua nyingine, Kuhanda alisema ofisi yake pia inafanya uchunguzi wa tuhuma za ufisadi wa zaidi ya Sh15 bilioni fedha zilizotolewa na Serikali kwa Wakala wa Maji Vijijini (Ruwasa) kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maji ndani ya mkoa huo.

Alisema wamebaini fedha hizo zimetumika kinyume cha utaratibu kwa kuwa lengo la upatikanaji wa maji bado halijafanikiwa katika maeneo yaliyolengwa, lakini fedha zimetumika bila kufuata utaratibu na kuzingatia thamani ya fedha.
 
Mambo kama hayo siikuwa hayapo,ila ni kuwa hayasikiki,ama hayana msemaji,kwanui wasemaji wakweli midomo imeshonwa,pia yafaa twende mbali zaidi,ni miongoni mwa njia nyingi haramu za kuongeza vipato vya watu.
 
TAKUKURU HIYO SIO KAZI YENU WAZEE HIYO NI KAZI YA TMDA

Roles and Functions of TMDA​

Pursuant to the Tanzania Medicines and Medical Devices Act, Cap 219, TMDA discharges the following functions:-

  1. Regulating the manufacturing, importation, distribution and selling of medicines, medical devices and diagnostics;
  2. Prescribing standards of quality, safety and effectiveness for medicines, medical devices and diagnostics;
  3. Inspecting manufacturing industries and business premises dealing with regulated products and make sure the standards required are attained;
  4. Evaluating and registering medicines, medical devices and diagnostics so as to reach the required standards before marketing authorization;
  5. Issuance of business permits for premises dealing with regulated products;
  6. Assessing the quality, safety and efficacy of controlled drugs;
  7. Conducting laboratory investigations for regulated products to ascertain their quality specifications;
  8. Conducting pharmacovigilance of medical products and vigilance of medical devices and diagnostics circulating on the market;
  9. Promoting rational use of medicines, medical devices and diagnostics; and
  10. Educating and sharing accurate and reliable information to stakeholders and the general public on regulatory matters.
 
Takukuru imeingia kuchunguza kwanini hizo dawa zimefika kwenye matumizi zikiwa zikiwa zimekaribia ku expire ili hali ni dawa zenye uhitaji mkubwa isije kuwa walifanya ujanja watu walibadirisha mzigo zile zenye expire date ya mbali zilibadilishwa na zile zinazikaribia kuexpire
 
Hiyo ni kazi ya TFDA au polisi,acheni kujipa kazi sio zenu au hamna kazi huko ofisini,
Kweli kabisa! Polisi wanahangaika kuilinda ccm, kazi zao zinafanywa na wazuia rushwa, wala na watoa rushwa wakuu ni ccm na polisi. Hapo ni kukwepa majukumu kwa kwenda mbele.
 
Hizi kazi zinafanywa na TMDA au maafisa waidhiniwa wa hakmashauri husika hususani..mafamaisia..maafisa afya n.k

Inashangaza TAKUKURU kufanya hizi kazi..?
Maswali ya kujiuliza je hakuna mamlaka husika katika ukaguzi wa madawa?
Je takukuru anahusika vipi na ukaguzi wa madawa?

#MaendeleoHayanaChama
 
Back
Top Bottom