KakaJambazi
JF-Expert Member
- Jun 5, 2009
- 18,713
- 12,063
Acheni wawasafishe ili CDM izidi kupeta. Riport ya Jairo ipo wapi?! Huenda ni mpango wa Mungu ya wao kuwapa wananchi hasira zaidi.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tanzania nchi ya usanii na kudanganyana. Nani angeamini kuwa TAKUKURU ingekuja na kamba kuwa itawachunguza mawaziri watuhumiwa wa ripoti ya CAG. Hivi Takukuru walikuwa wapi wakati wote huu au wanatafuta kuwatoa chochote kitu? Je Takukuru licha ya kupaswa kuvunjwa ina udhu wa kumchunguza mtu tena kigogo wa CCM na serikali? Nani anamdanganya nani?
Vyombo vya habari vilimnukuu mkurugenzi wa Takukuru Edward Hosea akisema, Sheria inatutaka tufanye uchunguzi wa tuhuma zozote na katika hili, CAG alitakiwa atupe taarifa. Lakini sisi baada ya kusikia bungeni tulimwandikia barua (CAG) kumwomba atupatie ripoti ya mambo yanayotuhusu tuanze kuyashughulikia haraka
Hakuna kitu hapo. Ni maigizo ya sanaa asilia. Hivi Hosea naye si alikuwa mtuhumiwa wakati fulani?