TAKUKURU wachunguze mkataba tata kati ya Mahindra Tech na TANESCO. Huenda kuna harufu kubwa ya ufisadi

Inafanya nini cha ajabu ? Inazalisha umeme? Wape watanzania 1/20 ya hiyo hela wangekutengenezea hiyo software. Ni wizi tu, period.
Ila kujenga international airport Chato bila pesa kuidhinishwa na bunge ndio uadirifu?

Magufuli alikuwa fisadi kuliko kiumbe yeyote nchini Tanzania.
 
Inafanya nini cha ajabu ? Inazalisha umeme? Wape watanzania 1/20 ya hiyo hela wangekutengenezea hiyo software. Ni wizi tu, period.


Software hazitengenezwi kwa majaribio, software kwa makampuni makubwa ambayo yapo kwa ajili ya kugenerate faida na kufanya operations zinapaswa kuwa tayari sokoni ready kwa matumizi... nitajie software moja ambayo unafikiri tayari iko sokoni Tanzania hapa na tukiwapa Tanesco basi immediately itakuwa kazini..

Chief, siwatetei Tanesco, ila najaribu kuwa tofauti na mtoa maada labda na wewe ambao ni kama mnachukulia hivi vitu kirahisi rahisi wakati ni mambo makubwa yanayohitaji utaalam uliobobea..

Swali: Tanzania kuna magari meeengi ya kisasa yanayohitaji diagnostic software's , mtanzania gani au kampuni gani ya kitanzania imeshadevelop hizo softwares na kuziuza kwa bei rahisi hapa tanzania...
Hizi software zinazozungumziwa hapa sio hizi za kuzimia taa, kuwashia taa au kufungulia mageti mtaani huku...
 
Kwa taifa masikini kama Tanzania ambalo raia wake maskini wanakamuliwa kodi na tozo za kila aina kuingia mkataba wa bil 60+ ili kukodi software ya gharama ya bil 60+ ili hali wanafunzi hawana madarasa, maji ya uhakika, umeme na hata makazi mazuri ni kukosa busara.

Hivi kweli Tanesco wanahitaji software kama hii kwa wakati huu? Ok kama wanauhitaji ndio kusema hakuna watanzania waliosoma Computer science?

Je, ndio gharama kubwa namna hii.

Kukodi Software kama kwa gharama kubwa ni dalili kubwa kuwa kuna ufisadi mkubwa. Maana bil 60+ kwa taifa letu masikini ni pesa nyingi ambazo zingetumika.

Kuhusu mkataba, soma: TANESCO yaingia mkataba wa kukodi software kutoka India kwa USD 30M
Takukuru waingie kazini. Pia inafaa kuangalia sera ya serikali kusimsmia mashirika. Je ni sawa tanesco kuingia mkataba kama huo au zipo taratibu zinahusu kuidhinishwa na wenye kumiliki shirika yaani serikali kwa niaba ya wananchi. Kuna dalili ya kuanza kuendeshwa shirika kihuni kwa matakwa ya wahuni wenye nia kulihujumu shirika kwa mara nyingine.
Kwa hivyo serikali itume takukuru kama haitoshi bunge lifuatilie ikibidi kuunda kamati.
Ukiweka mwenyekiti wa bodi mpigaji na mhuni tu hua hawajali sheria wala taratibu. Niliwahi ona hilo kwenye bodi ya Uda.
 
Mkuu, nafahamu vizuri sana maana ya software, hebu tueleze sasa hiyo software waliokodi Tanesco ni kwa ajili ya kazi gani?...

Binafsi kitaalam nafahamu gharama ya software tofauti tofauti na gharama zake na umuhimu wa kazi zake.....moja ya mambo yanayotufanya tushindwe kwenda mbele pia ni kupenda kwetu kuendesha mambo kienyeji na kuuweka utalaam pembeni..
Cmr
 
Kwa taifa masikini kama Tanzania ambalo raia wake maskini wanakamuliwa kodi na tozo za kila aina kuingia mkataba wa bil 60+ ili kukodi software ya gharama ya bil 60+ ili hali wanafunzi hawana madarasa, maji ya uhakika, umeme na hata makazi mazuri ni kukosa busara.

Hivi kweli Tanesco wanahitaji software kama hii kwa wakati huu? Ok kama wanauhitaji ndio kusema hakuna watanzania waliosoma Computer science?

Je, ndio gharama kubwa namna hii.

Kukodi Software kama kwa gharama kubwa ni dalili kubwa kuwa kuna ufisadi mkubwa. Maana bil 60+ kwa taifa letu masikini ni pesa nyingi ambazo zingetumika.

Kuhusu mkataba, soma: TANESCO yaingia mkataba wa kukodi software kutoka India kwa USD 30M
ERP COST.png
 
TAKUKURU wanajua kuchunga vicoba tu hiyo mikataba ya kimataifa hawaiwezi.
 
Kwa nini mataga mmekomalia sana hii software? Nini kipo nyuma ya pazia?
 
Back
Top Bottom