Takukuru sasa watakiwa kuwafuatilia mafisadi CCM, walikuwa wanawaogopa?

Halisi

JF-Expert Member
Jan 16, 2007
2,802
613
uvuaji gamba ni ovyo, wewe ndiye wa ovyo-Kikwete

RAIS Jakaya Kikwete, amekiri wazi kuwepo kwa vuguvugu la upinzani lenye nguvu kubwa hapa nchini, na kuonya kwamba, iwapo Chama cha Mapinduzi (CCM), hakitajirekebisha katika mienendo yake inayoonekana kuwaudhi wananchi, chama hicho kipo hatarini kupoteza hatamu ya kuliongoza Taifa na kusisitiza nia ya chama hicho kuwaondoa mafisadi.

Kadhalika, Rais Kikwete ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM Taifa, ametetea uamuzi wa kujivua gamba ndani ya chama hicho, uliopewa baraka zote na Halmashauri Kuu ya chama hicho (NEC), dhidi ya viongozi mafisadi kuhakikisha wanajiondoa ndani ya chama kabla hawajaondolewa, na kusema uamuzi huo haukuwalenga watu fulani wanaotuhumiwa kwa ufisadi, bali viongozi wote wasio na maadili mema ndani ya CCM.

Mkuu huyo wa nchi, aliyathibitisha hayo leo Jijini Mwanza, wakati akihutubia maelfu ya wanachama wa CCM katika sherehe za maadhimisho ya miaka 35 ya kuzaliwa kwa CCM, iliyofanyika Kitaifa kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini hapa.

Katika sherehe hizo, CCM ililazimika kutumia mtindo wake wa kukodi mabasi na maroli, kwa ajili ya kusomba watu kutoka maeneo mbali mbali ndani na nje ya mkoa huo, kwa ajili ya kuhudhuria maadhimisho hayo, ambayo hata hivyo yalionekana kughubikwa na imani za kishirikina ndani ya uwanja huo wa CCM Kirumba.

Katika hotuba yake kwa wana CCM, Rais Kikwete alisema kwamba, kwa sasa nchi imekumbwa na mtikisiko mkubwa wa vuguvugu la upinzani, na kwamba viongozi wa CCM na Serikali kwa ujumla wasiwe watu walioganda.

“Wapo wanaobeza mafanikio tuliyofikia, nasema huo ni uroho mbaya. Sisi tuwapuuze. Lakini tutambueni kwamba kwa sasa vuguvugu la upinzani limezidi kuwa na nguv kubwa hapa nchini.

“Kushika ama kuendelea kushika madaraka inatokana na ridhaa ya wananchi wenyewe. Hivyo wana CCM tutambueni hilo kwamba wananchi ndiyo wenye uwezo wa kutupa ama kutukataa kuwaongoza. Tukishindwa hilo tutashindwa”, alisema Rais Kikwete ambaye wakati wa kuingia uwanjani CCM Kirumba wasaidizi wake kitengo cha usalama wa taifa waliona chupa mbili zilizokuwa zimejazwa vitu vilivyodaiwa dawa za kishirikina, kisha mmoja wa saidizi wake hao kuipiga teke chupa moja.

Chupa hizo mbili za kampuni moja ya kutengeneza maji (jina tunalihifadhi), zenye ujazo wa lita 1.5, zilionekana moja kuwekwa upande wa zuria na nyingine upande wa pili wa zuria lililotandikwa uwanjani hapo kwa ajili ya mgeni rasmi na wageni wengine wanapopita kwenda meza kuu (V.I.P), kwa ajili ya shughuli hiyo ya maadhimisho hayo.

Alisema, lazima viongozi wa CCM na Serikali wawajibike kikamilifu katika kusimamia maendeleo ya wananchi, ili kuendelea kuwajengea imani raia hao dhidi ya chama chao tawala na Serikali kwa ujumla, na kwamba chama hicho tawala kimeathiriwa sana na viongozi wake wasiokuwa waaminifu mbele ya jamii ya Kitanzania.

Kuhusu kujivua gamba.
Mwenyekiti huyo wa CCM Taifa alisema: “Hivi karibuni nikiwa na NEC hapo Dodoma, nilitumia neno nyoka kujivua gamba. Usemi huo ulienezwa tofauti kabisa. Kimsingi tulipitisha maazimio mengi, lakini wenzetu wameona azimio moja tu la kujivua gamba.

Alisema, hoja ya kujivua gamba iliyopitishwa na NEC mwaka jana si ya ovyo, hivyo kiongozi na mwanachaa yeyote ndani ya CCM anayeuona uamuzi huo ni wa ovyo, basi yeye ndiyo wa ovyo mbele ya jamii.

“Uamuzi wa kujivua gamba ndani ya CCM si wa ovyo. Ukiuona wa ovyo wewe ndiyo wa ovyo. Haiwezekani tukaendelea kuwa na watu wa ovyo. Lazima chama kijipange na kujiweka sawa ili kisipoteze sifa kwa jamii”, alisema mwenyekiti huyo wa CCM taifa ambaye alipokea wanachama wapya wapatao 1,847.

Kwa mujibu wa Rais Kikwete ambaye alianza kuhutubia saa 8:45 mchana na kumaliza saa 9:37 alasiri, alikiri pia ajenda ya watu ndani ya chama hicho kujivua gamba imegonga mwamba, na amewatupia mzigo wanachama wake kuwawajibisha viongozi hao na wale wanaowaona hawaendani na maadili wala sera za chama hicho tawala.

Alisema, maamuzi ya kujivua gamba hayakulilenga kundi ama watu fulani ndani ya CCM, bali linawahusu wanachama wote wanaojitambua kwamba si waaminifu kujiondoa wenyewe ndani ya chama kwa kuachia nyadhifa za kiuongozi badala ya kusubiri kuondolewa na mamlaka za juu.

“Wito wa kujivua gamba haujapewa mwitikio mzuri. Tumetupa mpira huo kwa wanachama kuwawajibisha viongozi hao, maana tunawafahamu. Sasa kazi kwetu sote”, alisema Rais Kikwete pia alishuhudia uwanja huo wa CCM Kirumba kutokujaa watu kama ilivyokuwa mwaka 2005 wakati alipowasili kwa ajili ya kuomba kura ya kuwa mtawala wa nchi.

Uchaguzi wajumbe wa NEC.
Mwenyekiti huyo na Rais wa nchi alisisitiza kwamba, lazima wajumbe wa Halmashauri kuu ya chama (NEC), wachaguliwe kutoka kwenye wilaya zao, na si vinginevyo, na kusema hiyo itasaidia zaidi kukiimarisha chama chake hicho kinachonyemelewa na vuguvugu kali la upinzani nchini.

Hata hivyo, alikwenda mbali na kuwataka wanachama wasiokuwa wasafi, wenye upeo mfupi, wabakaji na mafisadi wasijidanganye kuomba uongozi huo wa NEC, maana wanachama hawatawachagua kutokana na matendo yao mabaya ndani ya jamii inayowazunguka.

Mwenyekiti huyo wa CCM aliiagiza Taasisi ya Kuzuia Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), kuanza kunyemelea nyendo za baadhi ya wanasiasa wanaotaka kugombea UNEC ndani ya chama hicho, kwani wapo baadhi yao wamepanga kutumia rushwa kuwahonga wanachama ili wawachague kushika nafasi hiyo ya juu.

Katiba mpya.
Rais Kikwete aliwapongeza wabunge wa CCM kwa uamuzi wao wa kuitetea Sheria ya Mabadiliko ya Katiba mpya 2011, na kwamba muswaada huo umeshawasilishwa tena bungeni, hivyo ataunda tume ya kukusanya maoni kwa Watanzania, ambapo aliwaomba wana CCM kujitokeza kwa wingi kutoa maoni yao, maana mmbamba ngoma huvutia kwake.

“Hili la Katiba mpya tumechukuwa mapendekezo ya vyama vya upinzani, kikiwemo CCM ambacho nacho kimetoa mapendekezo manane. Nawashukuru sana wabunge wa CCM katika hili, lakini wana CCM jitokezeni kwa wingi kutoa maoni yenu maana mmbamba ngoma huvutia kwake”.

Hata hivyo, Rais Kikwete alikwepa waziwazi kuzungumzia tatizo la mgomo wa Madaktari linaloikumba nchi kwa sasa, na kuahidi kulitolea ufafanuzi na maelezo muda si mrefu.

Alikitaka pia kitengo cha propoganda ndani ya chama hicho kufanya kazi vizuri, maana chama hicho kinaonekana kuzidiwa nguvu na wapinzani ambao wao hutumia propoganda za aina mbali mbali, hivyo wananchi kuanza kuamini maneno ya wapinzani.

Habari hii imeandaliwa na Sitta Tumma – Mwanza.
Ukiona uvuaji gamba ni ovyo, wewe ndiye wa ovyo-Kikwete | Fikra Pevu | Kisima cha busara!
 
uvuaji gamba ni ovyo, wewe ndiye wa ovyo-Kikwete

RAIS Jakaya Kikwete, amekiri wazi kuwepo kwa vuguvugu la upinzani lenye nguvu kubwa hapa nchini, na kuonya kwamba, iwapo Chama cha Mapinduzi (CCM), hakitajirekebisha katika mienendo yake inayoonekana kuwaudhi wananchi, chama hicho kipo hatarini kupoteza hatamu ya kuliongoza Taifa na kusisitiza nia ya chama hicho kuwaondoa mafisadi.

Kadhalika, Rais Kikwete ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM Taifa, ametetea uamuzi wa kujivua gamba ndani ya chama hicho, uliopewa baraka zote na Halmashauri Kuu ya chama hicho (NEC), dhidi ya viongozi mafisadi kuhakikisha wanajiondoa ndani ya chama kabla hawajaondolewa, na kusema uamuzi huo haukuwalenga watu fulani wanaotuhumiwa kwa ufisadi, bali viongozi wote wasio na maadili mema ndani ya CCM.

Mkuu huyo wa nchi, aliyathibitisha hayo leo Jijini Mwanza, wakati akihutubia maelfu ya wanachama wa CCM katika sherehe za maadhimisho ya miaka 35 ya kuzaliwa kwa CCM, iliyofanyika Kitaifa kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini hapa.

Katika sherehe hizo, CCM ililazimika kutumia mtindo wake wa kukodi mabasi na maroli, kwa ajili ya kusomba watu kutoka maeneo mbali mbali ndani na nje ya mkoa huo, kwa ajili ya kuhudhuria maadhimisho hayo, ambayo hata hivyo yalionekana kughubikwa na imani za kishirikina ndani ya uwanja huo wa CCM Kirumba.

Katika hotuba yake kwa wana CCM, Rais Kikwete alisema kwamba, kwa sasa nchi imekumbwa na mtikisiko mkubwa wa vuguvugu la upinzani, na kwamba viongozi wa CCM na Serikali kwa ujumla wasiwe watu walioganda.

“Wapo wanaobeza mafanikio tuliyofikia, nasema huo ni uroho mbaya. Sisi tuwapuuze. Lakini tutambueni kwamba kwa sasa vuguvugu la upinzani limezidi kuwa na nguv kubwa hapa nchini.

“Kushika ama kuendelea kushika madaraka inatokana na ridhaa ya wananchi wenyewe. Hivyo wana CCM tutambueni hilo kwamba wananchi ndiyo wenye uwezo wa kutupa ama kutukataa kuwaongoza. Tukishindwa hilo tutashindwa”, alisema Rais Kikwete ambaye wakati wa kuingia uwanjani CCM Kirumba wasaidizi wake kitengo cha usalama wa taifa waliona chupa mbili zilizokuwa zimejazwa vitu vilivyodaiwa dawa za kishirikina, kisha mmoja wa saidizi wake hao kuipiga teke chupa moja.

Chupa hizo mbili za kampuni moja ya kutengeneza maji (jina tunalihifadhi), zenye ujazo wa lita 1.5, zilionekana moja kuwekwa upande wa zuria na nyingine upande wa pili wa zuria lililotandikwa uwanjani hapo kwa ajili ya mgeni rasmi na wageni wengine wanapopita kwenda meza kuu (V.I.P), kwa ajili ya shughuli hiyo ya maadhimisho hayo.

Alisema, lazima viongozi wa CCM na Serikali wawajibike kikamilifu katika kusimamia maendeleo ya wananchi, ili kuendelea kuwajengea imani raia hao dhidi ya chama chao tawala na Serikali kwa ujumla, na kwamba chama hicho tawala kimeathiriwa sana na viongozi wake wasiokuwa waaminifu mbele ya jamii ya Kitanzania.

Kuhusu kujivua gamba.
Mwenyekiti huyo wa CCM Taifa alisema: “Hivi karibuni nikiwa na NEC hapo Dodoma, nilitumia neno nyoka kujivua gamba. Usemi huo ulienezwa tofauti kabisa. Kimsingi tulipitisha maazimio mengi, lakini wenzetu wameona azimio moja tu la kujivua gamba.

Alisema, hoja ya kujivua gamba iliyopitishwa na NEC mwaka jana si ya ovyo, hivyo kiongozi na mwanachaa yeyote ndani ya CCM anayeuona uamuzi huo ni wa ovyo, basi yeye ndiyo wa ovyo mbele ya jamii.

“Uamuzi wa kujivua gamba ndani ya CCM si wa ovyo. Ukiuona wa ovyo wewe ndiyo wa ovyo. Haiwezekani tukaendelea kuwa na watu wa ovyo. Lazima chama kijipange na kujiweka sawa ili kisipoteze sifa kwa jamii”, alisema mwenyekiti huyo wa CCM taifa ambaye alipokea wanachama wapya wapatao 1,847.

Kwa mujibu wa Rais Kikwete ambaye alianza kuhutubia saa 8:45 mchana na kumaliza saa 9:37 alasiri, alikiri pia ajenda ya watu ndani ya chama hicho kujivua gamba imegonga mwamba, na amewatupia mzigo wanachama wake kuwawajibisha viongozi hao na wale wanaowaona hawaendani na maadili wala sera za chama hicho tawala.

Alisema, maamuzi ya kujivua gamba hayakulilenga kundi ama watu fulani ndani ya CCM, bali linawahusu wanachama wote wanaojitambua kwamba si waaminifu kujiondoa wenyewe ndani ya chama kwa kuachia nyadhifa za kiuongozi badala ya kusubiri kuondolewa na mamlaka za juu.

“Wito wa kujivua gamba haujapewa mwitikio mzuri. Tumetupa mpira huo kwa wanachama kuwawajibisha viongozi hao, maana tunawafahamu. Sasa kazi kwetu sote”, alisema Rais Kikwete pia alishuhudia uwanja huo wa CCM Kirumba kutokujaa watu kama ilivyokuwa mwaka 2005 wakati alipowasili kwa ajili ya kuomba kura ya kuwa mtawala wa nchi.

Uchaguzi wajumbe wa NEC.
Mwenyekiti huyo na Rais wa nchi alisisitiza kwamba, lazima wajumbe wa Halmashauri kuu ya chama (NEC), wachaguliwe kutoka kwenye wilaya zao, na si vinginevyo, na kusema hiyo itasaidia zaidi kukiimarisha chama chake hicho kinachonyemelewa na vuguvugu kali la upinzani nchini.

Hata hivyo, alikwenda mbali na kuwataka wanachama wasiokuwa wasafi, wenye upeo mfupi, wabakaji na mafisadi wasijidanganye kuomba uongozi huo wa NEC, maana wanachama hawatawachagua kutokana na matendo yao mabaya ndani ya jamii inayowazunguka.

Mwenyekiti huyo wa CCM aliiagiza Taasisi ya Kuzuia Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), kuanza kunyemelea nyendo za baadhi ya wanasiasa wanaotaka kugombea UNEC ndani ya chama hicho, kwani wapo baadhi yao wamepanga kutumia rushwa kuwahonga wanachama ili wawachague kushika nafasi hiyo ya juu.

Katiba mpya.
Rais Kikwete aliwapongeza wabunge wa CCM kwa uamuzi wao wa kuitetea Sheria ya Mabadiliko ya Katiba mpya 2011, na kwamba muswaada huo umeshawasilishwa tena bungeni, hivyo ataunda tume ya kukusanya maoni kwa Watanzania, ambapo aliwaomba wana CCM kujitokeza kwa wingi kutoa maoni yao, maana mmbamba ngoma huvutia kwake.

“Hili la Katiba mpya tumechukuwa mapendekezo ya vyama vya upinzani, kikiwemo CCM ambacho nacho kimetoa mapendekezo manane. Nawashukuru sana wabunge wa CCM katika hili, lakini wana CCM jitokezeni kwa wingi kutoa maoni yenu maana mmbamba ngoma huvutia kwake”.

Hata hivyo, Rais Kikwete alikwepa waziwazi kuzungumzia tatizo la mgomo wa Madaktari linaloikumba nchi kwa sasa, na kuahidi kulitolea ufafanuzi na maelezo muda si mrefu.

Alikitaka pia kitengo cha propoganda ndani ya chama hicho kufanya kazi vizuri, maana chama hicho kinaonekana kuzidiwa nguvu na wapinzani ambao wao hutumia propoganda za aina mbali mbali, hivyo wananchi kuanza kuamini maneno ya wapinzani.

Habari hii imeandaliwa na Sitta Tumma – Mwanza.
Ukiona uvuaji gamba ni ovyo, wewe ndiye wa ovyo-Kikwete | Fikra Pevu | Kisima cha busara!
big up.Jk
 
Back
Top Bottom