TAKUKURU mulikeni NSSF Ubungo wanatesa wastaafu

njeeseka

JF-Expert Member
Oct 19, 2012
1,371
976
Kuna unyanyasaji na mateso makubwa wanafanyiwa wastaafu wa private sector pindi wanapoomba kupewa mafao yao. Kuna watu zaidi wa watano nimewasikiliza na kuona kuna bomu kubwa hapo NSSF UBUNGO.

Kuna wanaolalamika kwamba ukiomba kulipwa michango yako utazungushwa sana mpaka uwape kuanzia laki tano (500,000) hadi milioni.

Imefikia hatua maafisa wanaoshughulikia madai ya wastaafu/walioachishwa kazi WANAFICHA MAFAILI na pindi pesa ikitolewa mafaili yanaonekana.

Hii sio tabia mzuri piatabia inayokera sana hasa ukizingatia hiyo ni michango halali ya wanachama.

Yupo aliyediriki kusema ni bora kwenda kuanzishia madai yako mkoani kuliko hapo UBUNGO.

Niwaombe TAKUKURU hizi ni tuhuma zifanyieni kazi kama kuna mafaili yanafichwa mtajua tu -ombeni orodha ya maombi yaliyowasilishwa hapo na muone yamelipwa lini, mtaona kuna waliotoa pesa wakalipwa haraka na kuna walioomba tarehe sawa na aliyelipwa na bado mafaili yamefichwa.

Uongozi wa hapo inaonekana umeshindwa kusimamia watendaji wanaodhalilisha ofisi hiyo.

Inakera sana usiombe ukutane na mtu aliyefanyiwa hivyo utamuonea huruma.

TAFAKARINI NA MJIULIZE ENDAPO SERIKALI TULIYO NAYO YA MHE. MAGUFULI KAMA INARUHUSU HAYO WANAYOYAFANYA
 
Hayo mambo ya mafao yanaenda kuisha sheria ya kikokotoo inapoenda kupitishwa kesho kutwa.Forget about it.CCM walilawiti uchaguzi lakini watu badala ya kukataa dhuluma na kutetea haki zao wakawa wanakenua meno.Baada ya CCM kulawiti uchaguzi sasa hivi wanaenda kulawiti mwananchi mmoja mmoja.Stay tuned,the worst is yet to come!
 
NSSF nchi nzima ndio michezo yao hio,Sio Takukuru wala serikali yenye habari nao.

Nadhani Mhe. Magufuli ana watu wanaoweza kupita humu na kufumua fumua huko NSSF nashukuru kama tatizo hili limekuwa kubwa kiasi hiki.
Serikali lazima ilinde watu wake, hii sio sahihi kwa nchi inayopewa watu wake.
 
Hayo mambo ya mafao yanaenda kuisha sheria ya kikokotoo inapoenda kupitishwa kesho kutwa.Forget about it.CCM walilawiti uchaguzi lakini watu badala ya kukataa dhuluma na kutetea haki zao wakawa wanakenua meno.Baada ya CCM kulawiti uchaguzi sasa hivi wanaenda kulawiti mwananchi mmoja mmoja.Stay tuned,the worst is yet to come

Ukibahatika kukaa na muathirika wa hii kero hata mmoja tu nadhani utabadili mtazamo na badala yake utajenga hoja kipi kifanyike hata kwa short term.
Hakuna kitakacho badili matokeo ya Uchaguzi sasa, tukubali Mhe. RAIS ni mmoja tu na tumkabidhi kero zetu azitatue.
 
Ukibahatika kukaa na muathirika wa hii kero hata mmoja tu nadhani utabadili mtazamo na badala yake utajenga hoja kipi kifanyike hata kwa short term.
Hakuna kitakacho badili matokeo ya Uchaguzi sasa, tukubali Mhe. RAIS ni mmoja tu na tumkabidhi kero zetu azitatue.
'Hakuna kitakacho badili matokeo ya Uchaguzi sasa, tukubali Mhe. RAIS ni mmoja tu na tumkabidhi kero zetu azitatue.'

Sasa wewe endelea kumuamini hivyo hivyo,ni sawa kusubiri treni Airport.
 
Nadhani Mhe. Magufuli ana watu wanaoweza kupita humu na kufumua fumua huko NSSF nashukuru kama tatizo hili limekuwa kubwa kiasi hiki.
Serikali lazima ilinde watu wake, hii sio sahihi kwa nchi inayopewa watu wake.
Huyu si ndo alikuja na kikokotoo? au umesha sahau?
 
Pamoja na matatizo ya mfanyakazi mmoja mmoja wa NSSF, tatizo kubwa liko kwenye mfumo wa ONE MAN SHOW. NSSF wao wanachofanya ni "delaying tactics" wakisubiria DAILY ORDER.

Tuendelee kuwa wavumilivu na wanyenyekevu mpaka miaka mitano iishe!
 
TAKUKURU anzieni Ubungo ndio mje Ilala. Ubungo anzeni na kabinti keupe kenye kujiona kako kwenye chati sana. Kapo keupe hivi kazoefu kwa rushwa, dharau, kuchati kwenye simu na kutoa mimba.

Ubungo pameoza panahitaji kufanyiwa reshafo hasa ukizingatia DSM ndio kioo cha TZ, ninaimani JAMII FORUM bado ina nguvu na ushawishi mkubwa hivyo Maafisa wa TAKUKURU watachukua hili km ni jambo lao la kuanza nalo pia MAAFISA KIPENYO kama wapo humu walibebe hili na wao wana nafasi ya kulifanyia kazi.
 
Takukuru ubungo kweli ni jipu, kuna kabinti kamoja keupe kapo hapo sijui kuna mkubwa anakatafuna maana sio kwa dharau hizo
 
TAKUKURU anzieni Ubungo ndio mje Ilala. Ubungo anzeni na kabinti keupe kenye kujiona kako kwenye chati sana. Kapo keupe hivi kazoefu kwa rushwa, dharau, kuchati kwenye simu na kutoa mimba.
Haaa😁😂😅😀😁😂😄😄😄
 
Huyo dada Hadi asubuhi habari zinakuwa zimemfikia ataanza kunyenyekea
 
Back
Top Bottom