TAKUKURU, Mtumishi wa Umma anaponunua kipindi kwenye radio au TV kujadili masuala ya utendaji wa Serikali ni rushwa au si rushwa?

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Awamu ya sita inalo Jambo la kutafakari kuhusu mmomonyoko wa maadili unaoendelea Nchini. Tumewalea watu wachache wameafika mahali wananguvu kuliko Viongozi wa kitaifa. Tunaweza tukadhani tunapambana na wapinzani kumbe tunapambana kuuwa usawa katika jamii.

Tuna vyombo vya dola ambavyo kwa kiasi kikubwa vimeshindwa kutekeleza majukumu yao bila kuelekezwa na Rais au Waziri Mkuu. Tukio lililotokea Clouds leo la mahojiano Kati ya Sabaya DC wa hai na mtangazaji wa chombo hicho ni moja ya vitu vinavyofanywa na mtu huyu mmoja adharani bila utawala kuhoji Wala kukemea. Huyu DC alianza kufanya vurugu Hai akiwa anaambatana na polisi, akaingia kuvamia biashara na makazi ya watu akiwa na silaha Leo hii amenunua kipindi kwenye Televisheni kusafisha au kuongea Yale anayodhani yanamsafisha kuendana na utawala uliopo.

Naomba Takukuru mtuambie alichofanya DC kununua kipindi kwenye chombo cha habari kujadili masuala ya serikali Ni rushwa au siyo rushwa. Kama siyo rushwa well and good lakini Kama ni Rushwa inayolenga kupata upendeleo Basi nategemea hatua zichukuliwe.

Kwa upande wa CCM nadhani huu ni wakati wakuamua njia sahihi yakusonga mbele, mnaweza mkaamua kusonga mbele kwa kutumia mabavu kukandamiza watu au mkasonga mbele kwa kuondoa uonevu na watawala wenye mabavu. Tusione kimya Cha wananchi tukadhani wao wanafurahia dhuluma, tuelewe wananchi wanavumilia kwa sababu hawana uwezo wakuelekeza dola itende haki.

Lakini kumbukeni dharau ya Sabaya inakwenda mbali nakuamthiri RC na hata Waziri wa utawala Bora. Kumjenga mtu mmoja akawa na nguvu kuliko taasisi zinazomsimamia ni hatari kwa mustakabali wa taifa, ipo siku huyu mtu atakuza mtandao wake nakufanya Jambo kubwa zaidi ya tunayoaona adharani leo.

Tanzania siyo nchi yakufuata Wafanyabiashara na SmG usiku wa manane, siyo nchi ya DC kubeba silaha nzito ni nchi ya amani. Na Kama tunaamini ni nchi ya DC kubeba silaha nzito tungeona na wakuu wengine wa wilaya nchini wakifanya hivyo. Hatuoni DC mwingine hata ndani ya mkoa wa Kilimanjaro akifanya haya, je hai Kuna Nini zaidi au DC wake ana Nini anachodhani anaweza kufanya kuliko watu wengine Hadi atumie silaha?
 
Sio uwa kuna maofisa habari wa kila sekta na taarifa zao utolewa nao /kuunganishwa kwenye taarifa ya Msemaji Mkuu wa Serikali?
Hata hivyo pengine labda kuna utaratibu mahsusi kwa mhusika alipewa free airtime /sponsored na/kwa kibali cha Mkuu wake wa Mkoa.
 
Mi najiuliza tu,ule uhuru wa vyombo vya habari kufanya mambo yake uliokuwa unapigiwa kelele unahitaji tuwe tunasikiliza vipindi vinavyotusifia tu? Nadhani kwasababu tulisema tuwe tunajibizana kwa hoja, ni media hiyo hiyo inaweza kutumika kusikiliza upande wa pili. NCHI hii huwa hatuna uvumilivu zaidi ya kutukanana tu. Kama dawa ni hoja kwa hoja tubakihapo kuliko kuattack uwekezaji wa watu, uhuru wa kusikiliza usitoyapenda ni demokrasia pia.

Ukitaka kusikia tu yale uyapendayo, basi zile kelele za friidomu ofu media ni unafiki.
 
Ukisema kanunua kipindi hapo lazima uwe na ushahidi, Clouds wanaweza sema ni mgeni wao walimkaribisha kwenye kipindi, na kutokana na hiki ulichoandika hapa wanaweza kumkaribisha tena akajisafishe coz umemchafua.

Ukitaka solve tatizo lazima uwe na akili zaidi ya alielitengeneza vinginevyo unaweza dhani una solve kumbe ndio unamwagia moto petroli.
 
Watu watakaomsumbua huyu mama kwenye uongozi wake ni Bashiru, Doto, Mwigulu, OleSabaya, Kalemani, Kabudi na team yao yote.

Hawa watu hata mama awape nini bado hawataridhika.
 
kama hujui hata tafsiri ya RUSHWA ni nini ! hukupaswa kuandika ulicho kiandika.

sio kila kitu ni rushwa. Punguza hasira na chuki. tulizana acha kukurupuka.
Tuna fahamu, kuna kada wa chama cha mapinduzi ana fanya kazi clouds. Ndie huwaalika wajinga wenzake kwenda kuongea ujinga clouds.
Ndie alie mkaribisha yule jamaa wa Singida jangili. Na ndie amempa air time huyu jambazi wa kimaasai. Hakuna siri hapo.
 
Awamu ya sita inalo Jambo la kutafakari kuhusu mmomonyoko wa maadili unaoendelea Nchini. Tumewalea watu wachache wameafika mahali wananguvu kuliko Viongozi wa kitaifa. Tunaweza tukadhani tunapambana na wapinzani kumbe tunapambana kuuwa usawa katika jamii.

Tuna vyombo vya dola ambavyo kwa kiasi kikubwa vimeshindwa kutekeleza majukumu yao bila kuelekezwa na Rais au Waziri Mkuu. Tukio lililotokea Clouds leo la mahojiano Kati ya Sabaya DC wa hai na mtangazaji wa chombo hicho ni moja ya vitu vinavyofanywa na mtu huyu mmoja adharani bila utawala kuhoji Wala kukemea. Huyu DC alianza kufanya vurugu Hai akiwa anaambatana na polisi, akaingia kuvamia biashara na makazi ya watu akiwa na silaha Leo hii amenunua kipindi kwenye Televisheni kusafisha au kuongea Yale anayodhani yanamsafisha kuendana na utawala uliopo.

Naomba Takukuru mtuambie alichofanya DC kununua kipindi kwenye chombo cha habari kujadili masuala ya serikali Ni rushwa au siyo rushwa. Kama siyo rushwa well and good lakini Kama ni Rushwa inayolenga kupata upendeleo Basi nategemea hatua zichukuliwe.

Kwa upande wa CCM nadhani huu ni wakati wakuamua njia sahihi yakusonga mbele, mnaweza mkaamua kusonga mbele kwa kutumia mabavu kukandamiza watu au mkasonga mbele kwa kuondoa uonevu na watawala wenye mabavu. Tusione kimya Cha wananchi tukadhani wao wanafurahia dhuluma, tuelewe wananchi wanavumilia kwa sababu hawana uwezo wakuelekeza dola itende haki.

Lakini kumbukeni dharau ya Sabaya inakwenda mbali nakuamthiri RC na hata Waziri wa utawala Bora. Kumjenga mtu mmoja akawa na nguvu kuliko taasisi zinazomsimamia ni hatari kwa mustakabali wa taifa, ipo siku huyu mtu atakuza mtandao wake nakufanya Jambo kubwa zaidi ya tunayoaona adharani leo.

Tanzania siyo nchi yakufuata Wafanyabiashara na SmG usiku wa manane, siyo nchi ya DC kubeba silaha nzito ni nchi ya amani. Na Kama tunaamini ni nchi ya DC kubeba silaha nzito tungeona na wakuu wengine wa wilaya nchini wakifanya hivyo. Hatuoni DC mwingine hata ndani ya mkoa wa Kilimanjaro akifanya haya, je hai Kuna Nini zaidi au DC wake ana Nini anachodhani anaweza kufanya kuliko watu wengine Hadi atumie silaha?
Kiongozi dhaifu bhuteua wasaidizi wajinga. Kwa kweli magu alikuwa rais wa hovyo na aliteua watu wa hovyo kumshauri na kumsifia. Mtu kama bashite, Sabaya, Mwigulu, hapi nk hawana viwango vya kuitwa waheshimiwa
 
Kama intelligence ya nchi ikiangalia hizi incidences kwa 90% angle wataona kesho ya Tanzania Ni ipi. Katika tawala zote ukiona binadamu yupo tayari kuua ili atimize lengo na dhamira yake akijificha kwenye mgongo wa anaowaongoza tambua ipo siku atatamani kuwaongoza wanaomwongoza.

Tulikua na mkuu wa mkoa wa Dsm aliyeaminisha watu bila yeye dar haiwezi kupiga hatua, ameondoka mji umetulia na watu wanafanya bishara na shughuli za kiuchumi na zinakwenda. Kipindi chake kila mtu kwake Ni wakufilisiwa au kusulubiwa na dola.

Huko Kilimanjaro huyu Sabaya alipinganaga na Waziri Mkuu, akapingana na usuluhishi wa Mkuchika kwa sababu ya kumdharau Rc, Leo hii watawala wanamfumbia macho.

Anachofanya sabaya ni kujijengea mfumo nakuuimarisha na akifikia hapo atakuwa na wafuasi kwenye dola kama ambavo anamiliki dola hai na akijiakikishia anao mtandao wakutosha atafanya Jambo lisilotarajiwa.

Hiki anachofanya Sabaya hakina tofauti na walichotengeneza akina Lowasa, isipokuwa mmoja alitumia nguvu ya kiuchumi na kisiasa kujijenga na mwingine anatumia vyombo vya dola kujijenga. Huyu wakutumia vyombo vya dola ni mbaya zaidi kwa sababu anaweza kutumia ushawishi akamilikishwa silaha na Askari ambao atakuwa anawalipa yeye. Askari wote anaotumia Sabaya wanalipwa vizuri, fedha zinatoka wapi? Huu ni mfumo lazima CCM ikubali kuukata la sivyo utakuja kuikata. Ogopa mtu mwenye tamaa ya madaraka

Lastly
Hakuna maridhiano yanayoweza kupatikana kwa Taifa kuwa na viongozi wenye roho za kikatili kama Hawa.
 
Awamu ya sita inalo Jambo la kutafakari kuhusu mmomonyoko wa maadili unaoendelea Nchini. Tumewalea watu wachache wameafika mahali wananguvu kuliko Viongozi wa kitaifa. Tunaweza tukadhani tunapambana na wapinzani kumbe tunapambana kuuwa usawa katika jamii.

Tuna vyombo vya dola ambavyo kwa kiasi kikubwa vimeshindwa kutekeleza majukumu yao bila kuelekezwa na Rais au Waziri Mkuu. Tukio lililotokea Clouds leo la mahojiano Kati ya Sabaya DC wa hai na mtangazaji wa chombo hicho ni moja ya vitu vinavyofanywa na mtu huyu mmoja adharani bila utawala kuhoji Wala kukemea. Huyu DC alianza kufanya vurugu Hai akiwa anaambatana na polisi, akaingia kuvamia biashara na makazi ya watu akiwa na silaha Leo hii amenunua kipindi kwenye Televisheni kusafisha au kuongea Yale anayodhani yanamsafisha kuendana na utawala uliopo.

Naomba Takukuru mtuambie alichofanya DC kununua kipindi kwenye chombo cha habari kujadili masuala ya serikali Ni rushwa au siyo rushwa. Kama siyo rushwa well and good lakini Kama ni Rushwa inayolenga kupata upendeleo Basi nategemea hatua zichukuliwe.

Kwa upande wa CCM nadhani huu ni wakati wakuamua njia sahihi yakusonga mbele, mnaweza mkaamua kusonga mbele kwa kutumia mabavu kukandamiza watu au mkasonga mbele kwa kuondoa uonevu na watawala wenye mabavu. Tusione kimya Cha wananchi tukadhani wao wanafurahia dhuluma, tuelewe wananchi wanavumilia kwa sababu hawana uwezo wakuelekeza dola itende haki.

Lakini kumbukeni dharau ya Sabaya inakwenda mbali nakuamthiri RC na hata Waziri wa utawala Bora. Kumjenga mtu mmoja akawa na nguvu kuliko taasisi zinazomsimamia ni hatari kwa mustakabali wa taifa, ipo siku huyu mtu atakuza mtandao wake nakufanya Jambo kubwa zaidi ya tunayoaona adharani leo.

Tanzania siyo nchi yakufuata Wafanyabiashara na SmG usiku wa manane, siyo nchi ya DC kubeba silaha nzito ni nchi ya amani. Na Kama tunaamini ni nchi ya DC kubeba silaha nzito tungeona na wakuu wengine wa wilaya nchini wakifanya hivyo. Hatuoni DC mwingine hata ndani ya mkoa wa Kilimanjaro akifanya haya, je hai Kuna Nini zaidi au DC wake ana Nini anachodhani anaweza kufanya kuliko watu wengine Hadi atumie silaha?
Alikamatwa na KITAMBULISHO BANDIA CHA USALAMA WA TAIFA MJUNI ARUSHA kesi ikafunikwafunikwa baadaye akapewa u DC wa HAI na kesi ikaishia hapo.

Yawezekana huyo anayo KAZI MAALUM ya Serikali ya ccm.
 
TEAM MBOWE MNAHANGAIKA SANA!

SABAYA NI JEMBE MCHAPA KAZI CHUKI YENU NI KUDONDOKA KWA MWENYEKITI MBOWE!
 
Back
Top Bottom