Ileje
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,793
- 12,238
Takukuru yatangaza vita
Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Dodoma, Eunice Mmari alipoulizwa jana kuhusu madai hayo alikiri kuwa na taarifa za baadhi ya wagombea na mawakala wao kutoa rushwa na kusema taasisi hiyo imesambaza vijana wake katika kila kona ya mji huo.
Alisema tangu juzi usiku, wamekuwa wakizunguka usiku na mchana kwenye mahoteli na vijiwe vinavyoaminika kutumiwa na wagombea na wapambe wao lakini hawajafanikiwa kuwakamata.
Taarifa tunazo tangu jana (juzi), hatujalala mimi na vijana wangu tumekesha kuzunguka kila kona lakini tatizo tunalokumbana nalo ni kwamba wale wanaopokea fedha hizo hawataki kutoa ushirikiano, alisema.
Aliwataka wabunge na watanzania wenye uzalendo na nchi yao kuipatia taasisi hiyo taarifa za siri za watu wanaotoa fedha hizo na wale wanaozisambaza akiwahakikishiwa kwamba majina yao yatalindwa.
Nawaomba wabunge watusaidie katika hili kwa sababu wao ndiyo walengwa kwa kuwa ndiyo wanaopiga kura. Kama ni kufuatwa wao ndiyo wanaofuatwa lakini sisi Takukuru hatutakubali nchi iwakilishwe na wala rushwa, alisema Mmari.
Source: Mwananchi
Katika chaguzi mbalimbali za hivi karibuni rushwa imekuwa ikipigiwa sana kelele lakini hakuna hata mmoja aliyekamatwa na kufikishwa mahakamani!
Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Dodoma, Eunice Mmari alipoulizwa jana kuhusu madai hayo alikiri kuwa na taarifa za baadhi ya wagombea na mawakala wao kutoa rushwa na kusema taasisi hiyo imesambaza vijana wake katika kila kona ya mji huo.
Alisema tangu juzi usiku, wamekuwa wakizunguka usiku na mchana kwenye mahoteli na vijiwe vinavyoaminika kutumiwa na wagombea na wapambe wao lakini hawajafanikiwa kuwakamata.
Taarifa tunazo tangu jana (juzi), hatujalala mimi na vijana wangu tumekesha kuzunguka kila kona lakini tatizo tunalokumbana nalo ni kwamba wale wanaopokea fedha hizo hawataki kutoa ushirikiano, alisema.
Aliwataka wabunge na watanzania wenye uzalendo na nchi yao kuipatia taasisi hiyo taarifa za siri za watu wanaotoa fedha hizo na wale wanaozisambaza akiwahakikishiwa kwamba majina yao yatalindwa.
Nawaomba wabunge watusaidie katika hili kwa sababu wao ndiyo walengwa kwa kuwa ndiyo wanaopiga kura. Kama ni kufuatwa wao ndiyo wanaofuatwa lakini sisi Takukuru hatutakubali nchi iwakilishwe na wala rushwa, alisema Mmari.
Source: Mwananchi
Katika chaguzi mbalimbali za hivi karibuni rushwa imekuwa ikipigiwa sana kelele lakini hakuna hata mmoja aliyekamatwa na kufikishwa mahakamani!
- Nini kifanyike kukomesha rushwa hizi Tanzania?
- Je kuna umuhimu wo wote wa TAKUKURU kuendelea kuwepo au ni sehemu ya ulaji tu?