VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Mngechuna tu. CCM sasa itadhalilika tena. Kuhusu madini,ilitubidi makada tujikaushe na kuwa vigeugeu kuhusu kuyalinda madini. Sheria na mikataba ilipofanyika sirini,makada tuliunga mkono na kushangilia
Wapinzani waliotaka uwazi wa mikataba na usawa wa kisheria walikuwa maadui zetu. Tuliwaponda bila kuwapenda na tuliwataka viongozi wetu chamani waongeze mwendo wa jembe na nyundo. Wapinzani walisema kwa kuhema,tukawakebehi kama watu wa Bahi. Mambo yakawa yalivyo
Sasa,bila aibu hata chembe hata ukubwa wa wembe,tunamshangilia Rais na Mwenyekiti wetu kurekebisha Sheria na kuianika mikataba. Ile ile ya wakati ule. Kwa jambo hili,CCM tukavuliwa nguo na kudhalilika kiuhakika. Lakini,kisiasa inakubalika.
Sasa TAKUKURU mnalenga kutuvua tena nguo wanaCCM. Kuanzia Mwenyekiti wetu hadi kada wa shina,msimamo wetu ni kwamba Escrow haikuwa pesa ya umma. Waliosema za umma tuliwazodoa na kuwashambulia kwa hoja za haja. Tulisema waliochota Escrow wamechota pesa zao. Na waligawa zao.
Wamehujumu vipi pesa zao? Itakuwaje waliogawiwa wote wakiunganishwa nao kama Mushi alivyounganishwa na Melo? Wote ni makada. CCM si itatikisika kuliko miti wakati wa masika? TAKUKURU,mngetuacha tupumue jamani
Bastola ya nini tena jamani!?
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Wapinzani waliotaka uwazi wa mikataba na usawa wa kisheria walikuwa maadui zetu. Tuliwaponda bila kuwapenda na tuliwataka viongozi wetu chamani waongeze mwendo wa jembe na nyundo. Wapinzani walisema kwa kuhema,tukawakebehi kama watu wa Bahi. Mambo yakawa yalivyo
Sasa,bila aibu hata chembe hata ukubwa wa wembe,tunamshangilia Rais na Mwenyekiti wetu kurekebisha Sheria na kuianika mikataba. Ile ile ya wakati ule. Kwa jambo hili,CCM tukavuliwa nguo na kudhalilika kiuhakika. Lakini,kisiasa inakubalika.
Sasa TAKUKURU mnalenga kutuvua tena nguo wanaCCM. Kuanzia Mwenyekiti wetu hadi kada wa shina,msimamo wetu ni kwamba Escrow haikuwa pesa ya umma. Waliosema za umma tuliwazodoa na kuwashambulia kwa hoja za haja. Tulisema waliochota Escrow wamechota pesa zao. Na waligawa zao.
Wamehujumu vipi pesa zao? Itakuwaje waliogawiwa wote wakiunganishwa nao kama Mushi alivyounganishwa na Melo? Wote ni makada. CCM si itatikisika kuliko miti wakati wa masika? TAKUKURU,mngetuacha tupumue jamani
Bastola ya nini tena jamani!?
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam