TAKUKURU kuwabambikizia watu kesi

nyundo2017

JF-Expert Member
Sep 7, 2017
1,439
859


Ukisoma hapa mtuhumiwa alisingiziwa kesi na boss wake ambaye alikuwa ni mkuu wa takukuru mkoa wa rukwa ndugu hamis mwenda kwa ugomvi wao binafsi juu ya mwanamke.

Kwa kutumia cheo chake na kwa kuwatumia rco na mwendesha mashitaka wa mkoa wa rukwa kwa jina Silaji pamoja na jaji mfawidhi aliyestafu mlango kwa pamoja walimshikilia mtuhumiwa polisi kwa muda mrefu na baadae walimfunga mtuhumiwa kwa hila ili kuunga umoja wao.

Chakushangaza mtuhumiwa alifukuzwa kazi na takukuru kwa uonevu kabla hata ya kesi kusikilizwa kama ilivyokawaida yao na baadae aliposhinda kesi hiyo alirudishwa kazini kinyemela tu pasipo kuangalia athari zilizojitokeza na mhusika aliyesababisha hajachukuliwa hatua yeyote.

Pamoja na jaji mfawidhi msatafu mlango kusitafu na mwendesha mashitaka wa mkoa Salaji kuhamishwa na Mkuu wa takukuru mkoa rukwa mwenda kuhamishwa bado kuna watu wameumizwa na watu hawa kwa maana hiyo hata walikohamishiwa hao wawili bado watakuwa na madhara pia.

Watu wameka sana mahabusu kwa hira zao hadi ujio wa kaimu jaji mfawidhi mh. Mkeha na kuzifuta baadhi ya kesi zisizo na mashiko ingawa bado kuna kesi hazina mashiko ziko mahakamani.

Mh Rais Samia kwa huruma zako tunashauri iundwe tume huru kufuatilia kesi za watuhumiwa walioko mahabusu na zinazoendelea kwani ni wazi kwa mahakama hii hakuna haki itakayopatikana hakika.
 
Mbona kama una siri nzito ila unashindwa kuziwasilisha kiongozi, wahusika natamani waje hapa wakusaidie pa kuanzia
 
Af huyo Mwenda ni kama Mwanadiaspora Mwenzangu mkoa fulani nyanda za juu sikuwahi kufikiri kama ni muhalifu kiasi hiki
 
Acha kulia lia duniani hakuna haki,tafuta laki tano vuka mpaka Congo ukawaroge hao watu wafie mbali huko.
 
Back
Top Bottom